Sasa, huu uzalendo unaopigiwa upatu kwenye kila jukwaa ni upi? Au ni ile sala ya mtakatifu shetani ya fuateni niyanenayo, matendo yangu niachieni? Nitakuwa wa kwanza kuishangaa hii serikali ya kuhubiri uzalendo na nitakuwa wa nwisho kuamini kushtakiwa kwa wahusika wote wa escrow katika mahakama mpya ya mafisadi.Kalasinga ni mtu wa kupull string behind the scene!katupatia kweli
nilipigia mistari eneo la rweyongeza advocates firm
Laiti mamlaka ya kuwashtaki wahusika wote na kuchagua majaji wazalendo w kuisikiliza kesi ningelipewa mimi, aminini ningefukua makaburi yote kuusaka ukweli na nisingelikuwa na simile. Mbona wangekuwa na magereza yao wenyewe kama ya guantanamo! Ni wakati wa rais kuwaonyesha wanyonge kile anachokisimamia na kukihubiri na au awalk talks zake katika hili ili liwe funzo kwa wanaofanyia matumbo yao.