Televisheni na Redio hazitaruhusiwa kucheza wala kuonesha kazi za Sanaa bila uhakiki wa BASATA, TFB na COSOTA

Rahma Salum

Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
30
Reaction score
59
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Taasisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) imetoa tamko kuwa, kuanzia tarehe 1/5/2021 Televisheni na Redio hazitaruhusiwa kucheza wala kuonesha kazi yoyote kwenye vituo vyao bila kazi hiyo kuhakikiwa na BASATA (Muziki wa kusikika na kuona/audio na video) na TFB (Filamu), na kusajiliwa COSOTA kwa ajili ya ulinzi wa hakimiliki.

Tamko hilo limeambatana na maelekezo kwa mashirika ya utangazaji (Vituo vya Televisheni na Redio) Tanzania Bara, Wasanii, Waandaaji wa kazi za muziki na filamu na yeyote anayehusika. Juu ya vifungu vya sheria namba 23 ya Mwaka 1984 ya Baraza la Sanaa la Taifa na marekebisho yake ya Mwaka 2019 na kanuni zake za Mwaka 2018.

Vifungu hivyo vinamuelekeza mtu, chama, shirikisho, asasi, chombo cha habari au mtandao wa jamii unaohitaji kusambaza (kuonesha) kazi za filamu au mchezo wa kuigiza utapaswa kujiridhisha kuwa filamu au mchezo husika umepewa ithibati ya uhakiki kutoka Bodi ya filamu na atapaswa kuusambaza kwa kuzingatia alama ya daraja la filamu au mchezo husika.

Aidha, COSOTA imewasisitiza Wasanii, waandaaji na Wamiliki wa kazi za muziki na filamu kuhakiki na kusajili kazi kwa ajili ya manufaa na ulinzi wa kazi zao.

 
Acha tu leo Hamonazi ametoa wimbo yupo na Angel kuna mstari kabisa anasema nikupeleke Zanzibar au kilimanjaro, nimezoea kawaida unanipeleka kwenye mtaro.
 
NAWashauri wafute miziki yote tuwe kama Iran.
 
"If it moves, tax it.
If it still moves, regulate it.
When it stops moving, subsidize it".

President Ronald Reagan, American President, explaining how governments work.
 
Acha tu leo Hamonazi ametoa wimbo yupo na Angel kuna mstari kabisa anasema nikupeleke Zanzibar au kilimanjaro, nimezoea kawaida unanipeleka kwenye mtaro.
Huyo jamaa hapo ndio nimemuona boya sana. Wimbo mzima kaimba vizuri mwishoni kaja kuweka matusi ambayo yanaharibu Wimbo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…