mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,126
- 5,068
Dar es Salaam.
Mahakama ya Wilaya ya Temeke imemuhukumu Mkazi wa Chamanzi, Said Wanie (35) kifungo cha maisha kwa kosa la kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa.
Pia mahakama hiyo imemuagiza mshtakiwa huyo kumlipa mtoto huyo fidia ya kiasi cha Sh500,000.
Kati ya Mei 3, 2020 maeneo ya Chamanzi Wilaya ya Temeke mshtakiwa huyo alimlawiti mtoto huyo huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.
Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi, Anna Mpessa alisema mahakama hiyo imejiridhisha na ushahidi uliotolewa na mtoto mwenyewe pamoja na vielelezo vilivyotolewa na daktari vikionyesha kuwa mtoto huyo amelawitiwa.
Mpessa alisema katika ushahidi uliotolewa na mtoto mwenyewe ulidai kuwa akiwa maeneo ya nyumbani kwao anacheza mshtakiwa huyo alifika na kumwambia alikuwa anaitwa na mtu aliyetambulika kwa jina moja la Musa ambaye ni mlinzi wa Shule ya Sekondari ya Chamanzi.
Alisema mtoto huyo aliieleza mahakama hiyo kuwa aliongozana mshtakiwa huyo mpaka kwenye choo cha shule hiyo na alipoingia ndani alifunga mlango kisha akamvua nguo na kummwagia maji mwili mzima baadaye alianza kumlawiti.
Chanzo: Mwananchi
Mahakama ya Wilaya ya Temeke imemuhukumu Mkazi wa Chamanzi, Said Wanie (35) kifungo cha maisha kwa kosa la kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa.
Pia mahakama hiyo imemuagiza mshtakiwa huyo kumlipa mtoto huyo fidia ya kiasi cha Sh500,000.
Kati ya Mei 3, 2020 maeneo ya Chamanzi Wilaya ya Temeke mshtakiwa huyo alimlawiti mtoto huyo huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.
Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi, Anna Mpessa alisema mahakama hiyo imejiridhisha na ushahidi uliotolewa na mtoto mwenyewe pamoja na vielelezo vilivyotolewa na daktari vikionyesha kuwa mtoto huyo amelawitiwa.
Mpessa alisema katika ushahidi uliotolewa na mtoto mwenyewe ulidai kuwa akiwa maeneo ya nyumbani kwao anacheza mshtakiwa huyo alifika na kumwambia alikuwa anaitwa na mtu aliyetambulika kwa jina moja la Musa ambaye ni mlinzi wa Shule ya Sekondari ya Chamanzi.
Alisema mtoto huyo aliieleza mahakama hiyo kuwa aliongozana mshtakiwa huyo mpaka kwenye choo cha shule hiyo na alipoingia ndani alifunga mlango kisha akamvua nguo na kummwagia maji mwili mzima baadaye alianza kumlawiti.
Chanzo: Mwananchi