Tenda wema uende zako

Tenda wema uende zako

Gordian Anduru

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2021
Posts
369
Reaction score
747
Wafanyakazi wa posta walishangazwa kuona barua yenye anwani inayosomeka “Kwenda kwa Mungu, Baba SLP, Mbinguni”.

Baada ya kujiuliza pa kuipeleka wakaamua kuifungua na kuisoma, ilikuwa imeandikwa “ Kwako Mungu Baba Mimi ni mjane kikongwe kuna vibaka wameniibia shilingi laki moja, mwezi huu sina kabisa hela ya matumizi naomba unisaidie Shilingi Laki moja Mungu wangu nimekwama”.

Wafanyakazi wa posta wakahisi kuwa bibi kachanganyikiwa labda uzee maana huwezi kuandika barua kwenda mbinguni, kwa kumhurumia wakaamua kujichangisha wenyewe ikapatikana shilingi elfu sabini.

Wakaiweka kwenye bahasha na kutuma kwenye anwani yule bibi.

Siku kadhaa baadae wakakuta barua nyingine toka kwa bibi Yule Yule walipoifungua wakakuta imeandikwa. “Kwako Mungu Baba nakushukuru sana kwa kujibu ombi langu, Mwezi umeenda vizuri,

Najua uliniwekea Laki Moja ile wale wafanyakazi wa posta wezi sana wamenichomolea elfu thelathini zangu”
baruahiii.jpg
 
Hao wafanyakazi nao kumbe wanasoma siri za wateja wao.wao walijuaje kama ndani ya bahasha kuna barua yenye maandishi hayo
 
Wafanyakazi wa posta walishangazwa kuona barua yenye anwani inayosomeka “Kwenda kwa Mungu, Baba SLP, Mbinguni”.

Baada ya kujiuliza pa kuipeleka wakaamua kuifungua na kuisoma, ilikuwa imeandikwa “ Kwako Mungu Baba Mimi ni mjane kikongwe kuna vibaka wameniibia shilingi laki moja, mwezi huu sina kabisa hela ya matumizi naomba unisaidie Shilingi Laki moja Mungu wangu nimekwama”.

Wafanyakazi wa posta wakahisi kuwa bibi kachanganyikiwa labda uzee maana huwezi kuandika barua kwenda mbinguni, kwa kumhurumia wakaamua kujichangisha wenyewe ikapatikana shilingi elfu sabini.

Wakaiweka kwenye bahasha na kutuma kwenye anwani yule bibi.

Siku kadhaa baadae wakakuta barua nyingine toka kwa bibi Yule Yule walipoifungua wakakuta imeandikwa. “Kwako Mungu Baba nakushukuru sana kwa kujibu ombi langu, Mwezi umeenda vizuri,

Najua uliniwekea Laki Moja ile wale wafanyakazi wa posta wezi sana wamenichomolea elfu thelathini zangu”
View attachment 1920813
😂😂😂😂🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom