DANIIL MEDVEDEV Vs RAFAEL NADAL
Wababe hawa wanakutana kwenye fainali ya US Open 2019 kwa upande wa wanaume. Moja ya fainali bora kabisa kwa mwaka huu, ubora wao ndio unaifanya fainali hii kuwa bora.
Hapa nataka nimzungumzie kwa ufupi kijana Medvedev, kijana huyu Mrusi mwenye miaka 23 basi bila shaka mwaka 2019 ni bora kabisa kwake. Mwaka huu wa 2019 kijana huyu amefanya mengi sana katika mchezo wa tennis, ameweza kupambana mpaka kushika nafasi ya 5 katika ATP Players, ameweza kupambana mpaka kucheza fainali 4 mfululizo, ameweza kuwatandika vigogo waliokuwa juu yake hapa nawazungumzia kina Novak Djokovick, Thiem Dominic, Tistisipas na wengineo wengi tu. Pia kijana huyu amejitangaza vizuri kabisa, hakuna mdau ama mpenda tennis asiye mjua Medvedev.
Fainali hii anayo kutana na King of Clay hapa namzungumzia Rafael Nadal itakuwa ya pili mfululizo wanakutana kwa mwaka huu. Ya kwanza walikutana Agosti 11 kule Montreal, Canada katika michuano ya Rogers Cup ambapo Medvedev akufua dafu mbele ya mkali Nadal. Hivyo basi fainali hii itakuwa ya kulipiza kisasi kwa upande wa Medvedev wakati Nadal akisaka Gland Slam yake ya pili kwa mwaka huu.
Fainali hii sio ya kukosa kabisa tizama kiwango alichokuwa nacho Medvedev mwaka huu alafu tizama anakutana na nani katika fainali hii, huwezi kosa kama uko serious na mchezo wa tennis. Pindi nikimuona Medvedev huwa najiuliza ukiwatoa Nadal, Djokovick pamoja na Federer ni nani wakumzuia Mrusi huyu nawaza kisha nasema hayupo kabisa. Medvedev ni kijana anae kuja vizuri kabisa akiendelea hivi kama anavyoendelea basi bila shaka mbeleni atakuwa mchezaji mkubwa katika Tennis.