Tetemeko la Ardhi Kintinku

Tetemeko la Ardhi Kintinku

KUTATABHETAKULE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
5,159
Reaction score
5,070
Taarifa mitandaoni zinaeleza kuwa leo tarehe 10 Mei, 2022 saa 9:22 mchana limetokea tetemeko la ardhi Kusini mwa Kintinku. Tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa 4.30 kwenye kipimo cha Ritcher.

IMG_20220510_164619.jpg

Pia soma:
 
Kwa vile nipo mbali na sehemu husika sina taarifa kuhusu madhara yaliyotokea. Tunawaomba waishio maeneo hayo watupe taarifa kuhusu hilo.
Jina lako linafanana na mlima Saranda. Kama upo mbali haraka ya nini kuripoti? Au uonekane wa kwanza kuleta uzi humu? Aliyekupa taarifa alitakiwa akupe details ili uripoti sahihi humu jamvini.
 
Jina lako linafanana na mlima Saranda. Kama upo mbali haraka ya nini kuripoti? Au uonekane wa kwanza kuleta uzi humu? Aliyekupa taarifa alitakiwa akupe details ili uripoti sahihi humu jamvini.
Asante sana Kitonga. Ni kweli jina langu linafanana na mlima Saranda. Ila pia nimeona jina lako linafananafanana na Mlima Kitonga na hilo halinishangazi. Nimeeleza wapi nilipozipata taarifa hizi na pia ipo ramani ikionesha sehemu husika. Jamiiforums inatuomba tupatapo taarifa ambazo watu wangependa kuzisikia basi ni vyema tuzitoe ili wengi wetu wazielewe.
 
Nilihisi kitu kama hicho nikiwa kazini,ila nikaona kama ni mimi peke yangu ndio nimefeel hakuna hata mmoja wetu pale aliegundua kitu...
 
Asante sana Kitonga. Ni kweli jina langu linafanana na mlima Saranda. Ila pia nimeona jina lako linafananafanana na Mlima Kitonga na hilo halinishangazi. Nimeeleza wapi nilipozipata taarifa hizi na pia ipo ramani ikionesha sehemu husika. Jamiiforums inatuomba tupatapo taarifa ambazo watu wangependa kuzisikia basi ni vyema tuzitoe ili wengi wetu wazielewe.
Saw kiongozi. Nipo hapa Ruaha Mbuyuni. Kwema huko Manyoni?

Mbona hukuendelea kutuletea taarifa kamili we agweee??
 
Nilihisi kitu kama hicho nikiwa kazini,ila nikaona kama ni mimi peke yangu ndio nimefeel hakuna hata mmoja wetu pale aliegundua kitu...
Ofisi ipi ulikwepo? Pale shuleni kwako shule ya msingi Saranda au Ofisi ya Mtendaji wa kijiji?
 
Saw kiongozi. Nipo hapa Ruaha Mbuyuni. Kwema huko Manyoni?

Mbona hukuendelea kutuletea taarifa kamili we agweee??
We Mnyalukolo, Mbukwenyi . Nilitegemea hao jamaa wa Kintinku wataleta taarifa zaidi lakini hadi sasa hawajaleta. Nadhani kuna tatizo la mtandao ndo maana hatujapata mrejesho. Asante.
 
Back
Top Bottom