Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 60,050
- 104,466
Ni wapi niliposema najuwa kila kitu? Nimekuuliza hapo badala ya kunijibu unaleta viroja.Kamuulize yeye atakueleza kaibuliwa vipi, kitu usokijua ni bora ukaomba usaidiwe kujua kuliko kujifanya unajua kila kitu.
Kumekucha ni Siri nyuma yake ya uteuzi huu?Wadau maoni yenu please Jaji za Zenji anafit kuja Tz? Maana zamani hata wakuu wa mikoa znz walikuwa wanateuliwa na Rais wa JMT baada ya mabadiliko ya katiba ta SMZ madaraka ya uteuzi wakawa chini ya Rais wa ZNZ na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, sasa kumtoa Jaji aliteuliwa na Rais wa SMZ sio kuingilia Mamlaka ya SMZ?
View attachment 1968490
Huenda hiiPhilemon Sengati ana kiburi kimepitiliza, aliwagomea hadi mawaziri wa kilimo kwenye kutoza mazao km dengu, alikuwa anakaidi amri za mabosi zake.
jamani tuacheni hizi mbishe,CJ ni Muislam
JK ni Muislam
Msajili Wa Mahakama Tz ni Muislam
Uteuzi wa kimkakatiWadau maoni yenu please Jaji za Zenji anafit kuja Tz? Maana zamani hata wakuu wa mikoa znz walikuwa wanateuliwa na Rais wa JMT baada ya mabadiliko ya katiba ta SMZ madaraka ya uteuzi wakawa chini ya Rais wa ZNZ na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, sasa kumtoa Jaji aliteuliwa na Rais wa SMZ sio kuingilia Mamlaka ya SMZ?
View attachment 1968490
Huu uteuzi una mashaka mengi. Naiona rushwa ya cheo ikitamalakiHuu uteuzi wa Siyani umekuja kimkakati au ni mpango uliokuwepo?
Hasa wakati huu ambao hukumu ya kesi ndogo ilikuwa inasubiriwa tar 19.10.2021, Siyani akiwa kama muhusika mkuu kwenye kesi iliyojaa siasa kama ile napata mashaka.
Nilimkubali sana alivyosikiliza kesi ndogo ya Mbowe, alikuwa kama refarii haswa, upande mmoja ukiweka objection anauliza upande wa pili wanaonaje.
Then wakijibu anarudi kwa upande wa waliotoa objection kama wanakubaliana na hoja ya upande wa pili, wakikataa, jaji anaangalia sheria inasemaje, then anaupa haki upande unaostahili kesi inaendelea kusikilizwa.
Sijui kama wataipangia kesi jaji mwingine, if yes, napata ukakasi na huu uteuzi kama sio wa kimkakati, kumuondoa huyu aliekuwa anaenda na sheria/haki halafu wamrudishe kama yule wa mwanzo kuwafundisha jamhuri nini cha kufanya, fingers crossed.
Haya maandishi ya kizungu wananchi wengi hatuyaelewi.
Baada ya Uteuzi wa Jaji Kiongozi Mpya Siyani Wakishirikiana na Mtendaji Mkuu wa Mahakamq Prof: Elisante wananchi tunaimani kuwa sasa Matumizi ya Lugha ya Kiswahili katika kutoa haki za wananchi kuanzia Mahakama za Wilaya hadi Mahakama za Rufaa yataharakishwa kwa masilahi ya wananchi wa Tanzania.
Sasa lugha ya kiSwahili tufanye tathmini inaongoza katika kuwasilisha na kutumika katika nini kuliganisha na lugha zingine za kibantu labda inaongoza katika kueneza dini na kuimba lakini inapokuja suala la taaluma ipo nyuma sana hivyo ijipange kukopa na kutohoa maneno ya kitaaluma toka ktk lugha za kigiriki, kilatini, kiarabu, kiEnglish, kifaransa n.k ili tusije kuwa tunapotoka ktk kuwakilisha elimu na maana husika za kitaaluma.French is a Romance language.
Ndio wasomi. Si mlikuwa mnasema waislam hawana wasomi. Vp sasa
Mbona kwenye kesi ya mauaji ya akina Zombe na wenzake kesi alisikiliza jaji kiongozi wa wakati huo (jina limenitoka)?Tukimsikiliza Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu tunapata picha kuwa majukumu ya jaji kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania ni nafasi ya kiutawala na kiutendaji zaidi kuhakikisha Mahakama zinapata waajiriwa wa kutosha, vitendea kazi, kutatua changamoto zinazojitokeza, kufukuzia bajeti na stahili za wafanyakazi kama mahakimu wafawidhi, majaji n.k
Hivyo jaji Kiongozi kutumika mahakamani kusikiliza kesi, kwa Jaji Kiongozi itakuwa ngumu maana yupo zaidi kusimamia taasisi kama msaidizi na mshauri wa Jaji Mkuu
27 Jan 2020
JAJI KIONGOZI ELIEZER MBUKI FELESHI " HAKUNA URASIMU KUFUNGUA MASHAURI, UNAWEZA KUSIKILWA SIKU HIYO HIYO"
Uongozi wa mahakama umezungumza na wanahabari kwa lengo la kueleze mafanikio ya muhimili huo muhimu ambapo pamoja na mambo ya kupunguza idadi za kesi ambazo hazijapagiwa kusikilizwa, umetangaza mpango wa kujengwa kwa jengo la mahakama kuu Dodoma. Jaji Kiongozi Eliezer Mbuki Feleshi aliwapa wanahabari wasaa wakuuliza maswali ambayo pengine yanahitaji majibu ya kina.
Source : Global TV online