TEUZI: Rais Samia amteua Jaji Mustapha Siyani kuwa Jaji Kiongozi, Sophia Mjema kuwa RC Shinyanga

TEUZI: Rais Samia amteua Jaji Mustapha Siyani kuwa Jaji Kiongozi, Sophia Mjema kuwa RC Shinyanga

Jicho la tatu...
Kesi ya Mbowe imeleta shida sehemu...
Itabidi atafutwe Jaji mwingine ili alete Suluhu..
Hapo ndipo umuhimu wa Katiba Mpya unapoonekana
Bila shaka atakuwa jaji wa pili kubadishwa katika kesi hii, au atakuwa na uwezo wa kuendelea nayo. Ufafanuzi tafadhali, au huyu ni Siami mwingine?
 
Jaji Siyani ni Mfano mzuri kwa Majaji wengine.
ni mtu mtenda haki na mpenda haki, ni mtu asiye penda uonevu, asiye penda majungu wala fitina ni mtu mwenye maono,
mchapa kazi asiye choka.
bado kijana ana nguvu ya kuleta mabadiliko.
Hakika ataisafisha mahakama na itaboreka zaidi.
Ila Zandramo hapendi haki na hapendi kuona haki ikitendeka.
 
Mkuu zandrano umekuwa mzalendo wa kukipigania kiswahili kuliko hata wenye dhamana kama vile BAKITA au TUKI.

Nakuunga mkono, Matumizi ya Lugha ya kiswahili ni Muhimu sana ktk kutoa haki za watanzania.

Sheria ilipitishwa Na Bunge kuwa Ruksa sasa Kwa Majaji wetu Na mahakimu wetu kuandika Na kutoa hukumu Kwa lugha ya kiswahili lkn cha kushangaza ukifika mahakamani hadi leo bado hukumu zinatolewa Kwa lugha ya kiingereza!! Kweli wananchi wengi wanakerwa sana Na hali hii!!

Inaonekana wazi Muhimili wa Mahakama hauko tayari kutumia lugha ya kiswahili kutoa haki ZA wananchi, kinacho fanyika ni kuwahadaa tu, sielewi kwa nini Na Kwa masilahi ya nani?!

Wananchi wanaomba Lugha ya kiswahili itumiwe Na Majaji Na mahakimu ktk kutoa haki zao.
Hayati JPM angekuwa bado hai naamini mchakato wa kutafasiri sheria zingine kutoka lugha ya kingereza kwenda kiswahili unge kuwa umekamilika, ila kwa sasa zoezi la kutafasiri sheria mbalimbali unasuasua!!! yaaani ni kama vile hautakiwi ukamilike haraka!!!
hii inaonyesha wazi kuwa kuna watu hawaoni umuhimu wa jambo hili la haki kutolewa kwa lugha ya kiswahili.
Kama SADC wameamua kutafasiri sheria zao kutoka lugha ya kiswahili kwenda kingereza pia wameamua kuweka kumbukumbu za vikao vyao vyote kwa lugha ya Kiswahili sembuse Mahakama!!
Kwakweli hii ni Kero ambayo inapaswa ishughulikiwe haraka iwezekanavyo.
 
Comments kama hizi za kidini hazipaswi kutolewa na mtu yeyote anae elewa mambo. Ni chembe chembe za kurutubisha bomu la religious conflicts. Tutafute historia ya mataifa yaliyopitia hii adhia watuambie na tujifunze. Uteuzi wa Mh Raisi unazingatia uweledi na sifa za mteuliwa bila ya dini yake. Hivi, leo tukianza kuhesabiana kuwa huyu dini gani tutafika kweli. Think twice before posting such a thug post
Hizi kazi zinapaswa kuombwa na watu wenye sifa......wafanye interview publicly kama Kenya vile hii teuwa teuwa huleta maneno.....
mchawi katiba hapo
 
Kala dodo?
Sophia mjema kala dodo, baada ya yule wa kisarawe hadi sasa temeke kuwa na shingo ngumu ya kuolewa, hiyo ndio ilikuwa nafasi yake.....tulimsutua humu toka mwaka jana......watu wakapiga domo humu balaaa
 
Uwaga Simpendi Sengati Kwa Sababu anaongea Kwa Sauti ya Juu, Kakaza Mishipa utadhani anagombana na Mtu. Acha arudi Udom akafundishe Sasa
 
Wadau maoni yenu please Jaji za Zenji anafit kuja Tz? Maana zamani hata wakuu wa mikoa znz walikuwa wanateuliwa na Rais wa JMT baada ya mabadiliko ya katiba ta SMZ madaraka ya uteuzi wakawa chini ya Rais wa ZNZ na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, sasa kumtoa Jaji aliteuliwa na Rais wa SMZ sio kuingilia Mamlaka ya SMZ?

View attachment 1968490
Udini na ukabila wa chifu h mbona unatisha sana? Ni yeye au ni mzee wa msonga?
 
Hongereni wateuliwa wote ....JK tenda haki utaheshimika milele umetufungua macho wengi wetu....kesi Mbowe ukivyoendesha kwa haki
 
Yaani wameona kesi ya Mbowe haina umuhimu wanataka kuanza upya huku kila siku wakiongelea haki mahakamani...zimebaki siku ngapi si wangesubiri atoe hukumu harafu ndio wateuane kama atabadilishwa ni kweli swala la PGO limewaumbua..
 
Pongezi Jaji Siyani, Hayati Rais Magufuli alikuamini, Rais Samia anakuamini. Itende haki.

Bila shaka Rais Samia ataendelea kutekeleza ahadi yake ya kuongeza watumishi kwenye Mahakama zetu na kujali maslahi yao. #mamayukokazini

E-xjHaAWQAcVblq.jpg
 
CJ ni Muislam
JK ni Muislam
Msajili Wa Mahakama Tz ni Muislam

Mkuu acha kuendekeza udini, usiangalie nafasi za hao wateule 3 au 4 tu halafu ukahitimisha.
Mimi ni mkiristu lkn naweza kukwambia kuwa ukiangalia kiuhalisia ktk mhimili wa Mahakama wakristu ndio wengi zaidi, angalia idadi ya Majaji, Wasajili, Watendaji, Mahakimu n.k, viongozi na ambao sio viongozi.
Mimi napenda sana uwiano ktk nafasi ZA uongozi wa nchi yetu kama anavyo fanya Rais Samia maana Uwiano huimarisha umoja Na mshikamano wa Taifa letu.
Taifa letu haliwezi kujengwa Na watu wa aina moja tu bali watanzania wote.
Kazi iendelee.
Mungu azidi kumbariki Rais wetu mpendwa Samia.
Anatuongoza vyema sana
 
Back
Top Bottom