TFF, Benchi la Ufundi la Taifa Stars huko CHAN 2021 nimeshamaliza Kazi kwa Kikosi hiki Namibia leo na Guinea Wiki ijayo wanakufa!

Umetisha mkuu hasa hapo kwa Faridi Mussa
 
Huyu kocha wa namibia naoa alibet hii mechi...sasa ndio substitution gani ile? Unamtoa mtu ambaye ndio anapeleka mashabulizi kwa wapinzani!!
 
Katika nafasi ya Ibrahim Ame acheze Dickson Job, ya Erasto Nyoni acheze Feisal Salum na ya John Boko acheze Adam Adam. Tutashinda msihofie.
Kuhusu Farid ni kama ulivyosema, uchawi kweli noma. Kwa hiyo hilo goli ndo basi tena!?
 
Umetisha mkuu hasa hapo kwa Faridi Mussa
Endeleeni Kunichukulia poa tu. Kuna Watu walidhani natania na wengi wao walikuwa wanataka isitokee kama nilivyosema ili waniumbue sana tu.
 
We jamaa nomaa, hebu tutabirie na game ya tarehe 27 je tutamuweza Guinea?
Tatizo lenu Members wa JF mna dharau halafu ni Wanafiki mno ila wengine tumezaliwa tayari tunajiamini na tuna uhakika na kile tunachokifanya.
 
Tatizo lenu Members wa JF mna dharau halafu ni Wanafiki mno ila wengine tumezaliwa tayari tunajiamini na tuna uhakika na kile tunachokifanya.
Shida ni kwamba humu JF kila mtu anajifanya mjuaji hata kama hana alijualo. MKUU,ILA MIMI NILISHAKUELEWA SANA KWENYE ENEO LA SOKA..

Utasikia mwanaJF anasema "ushirikina na soka wapi na wapi"?, mara Oooh " usilete imani za kijinga hapa!" au "kama uchawi una msaada kwenye soka si Tanzania ingeshabeba World Cup, na timu za Sumbawanga zingekuwa zinatesa Ligi ya Mabingwa Afrika?" Basi mi nabaki nawaangalia tu.

Cha ajabu,jitu hilo hilo unakuta linatoka familia ya washirikina, mwanasiasa au mwanasoka mahiri linayemkubali ndo mshirikina no.1, bado yule Askofu,Mchungaji,Padre na Shehe wake. Mi huwa nayaangalia tu.
 
Halafu kuna Watu utawasikia wanasema kuwa Brazil hakuna Uchawi wakati hakuna Watu wanaojua Kuroga japo wana Vipaji vya Soka kama Brazil.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…