Kichwa Kichafu
JF-Expert Member
- Apr 13, 2017
- 44,855
- 189,385
Habari,
TFF msicheze wala kuleta utani juu ya mashabiki wanaoleta vurugu viwanjani kwa namna yeyote ile pale inapothibitika tukio kufanyika.
Nimeshangazwa sana na mashabiki wa Simba SC leo kuanza kupiga mashabiki waliokuwa hawa-support timu yao Simba SC.
Ili tukio limewahi kutokea kwa klabu zote kubwa nchini kupiga mashabiki wapinzani na mlitoa onyo na adhabu japo si kali kama mna mpango wa kukomesha hizi tabia.
Pia katika mashindano ya mpira mashabiki wamekuwa na kasumba ya kurusha chupa za maji na takataka viwanjani kupiga wachezaji wakati wanashangilia.
Haya yote TFF mkiwa na huruma mtalea tabia chafu na huko mbele itakuwa ngumu kukomesha kama msipoanza mapema kwa kuchukua adhabu kali bila kujali ni timu gani imeleta vurugu.
Ni heri kukosa mapato kwa baadhi ya mechi Ila adhabu ichukue mkondo wake la sivyo huko baadae tutajilaumu na tutakuwa tumechelewa.
Angalia ligi zilizoendelea ambako siku zote tunatamani kufika huko hakuna mambo hayo zaidi ya kupambana na ubaguzi wa rangi.
Pamoja na yote kwenye ubaguzi wa rangi sheria zilikuwa kali hata kufungiwa mashabiki kabisa sasa sisi huku bongo tunajipagua kwa kupigana wenyewe kwa wenyewe.
TFF msiogope wala msiwe wanyonge sheria zinavyokuwa kali amini amini nawaambiwa huu ujinga utakoma mara moja.
Nawasilisha Mzee Mkoloni.
Cc: Kichwa Kichafu.
TFF msicheze wala kuleta utani juu ya mashabiki wanaoleta vurugu viwanjani kwa namna yeyote ile pale inapothibitika tukio kufanyika.
Nimeshangazwa sana na mashabiki wa Simba SC leo kuanza kupiga mashabiki waliokuwa hawa-support timu yao Simba SC.
Ili tukio limewahi kutokea kwa klabu zote kubwa nchini kupiga mashabiki wapinzani na mlitoa onyo na adhabu japo si kali kama mna mpango wa kukomesha hizi tabia.
Pia katika mashindano ya mpira mashabiki wamekuwa na kasumba ya kurusha chupa za maji na takataka viwanjani kupiga wachezaji wakati wanashangilia.
Haya yote TFF mkiwa na huruma mtalea tabia chafu na huko mbele itakuwa ngumu kukomesha kama msipoanza mapema kwa kuchukua adhabu kali bila kujali ni timu gani imeleta vurugu.
Ni heri kukosa mapato kwa baadhi ya mechi Ila adhabu ichukue mkondo wake la sivyo huko baadae tutajilaumu na tutakuwa tumechelewa.
Angalia ligi zilizoendelea ambako siku zote tunatamani kufika huko hakuna mambo hayo zaidi ya kupambana na ubaguzi wa rangi.
Pamoja na yote kwenye ubaguzi wa rangi sheria zilikuwa kali hata kufungiwa mashabiki kabisa sasa sisi huku bongo tunajipagua kwa kupigana wenyewe kwa wenyewe.
TFF msiogope wala msiwe wanyonge sheria zinavyokuwa kali amini amini nawaambiwa huu ujinga utakoma mara moja.
Nawasilisha Mzee Mkoloni.
Cc: Kichwa Kichafu.