Kataa Rushwa
JF-Expert Member
- May 15, 2015
- 728
- 765
Ushahidi wa idadi ya kadi haupo ndiyo maana marefa walisakwa na kutumika kutumia mashimo.Hebu pitia rufaa yenyewe na unipe majibu sahihi ili tuanzia hapo.
1. Je ni kweli mchezaji huyo alikuwa na kadi 3 za njano?
2. Unajua kanuni zinazoendesha ligi kuu 2016/2017?
3. Unaamini kuwa kila klabu ilikuwa na mwakilishi wakati wa kikao cha kupitia kanuni hizo kabla ya ligi kuanza na walisaini na kila mmoja ana nakala hiyo?
Mubashara!Kagera apewe jasho lake simba wa maonyesho abaki na povu lake
Ndo hapo Kazi ni kutafuna tuIvi? Naulizia awa TFF website yao ipo ''''active''''kweli au hata''''blog'''' wanayo kweli
MubasharaNaunga mkono hoja kwa maana ya marekebisho ktk msimu ujao. Haipendezi timu kupewa ushindi wa mezani.
Ni kweli pia kuwa kama Simba angeshinda hii mechi huku Kagera akiwa na mchezaji mwenye kadi 3 inaonekana asingeonekana na hivyo kosa lisingeadhibiwa. Kanuni irekebishwe ili unapochezesha mchezaji mwenye kadi 3 unyang'anywe tu point hizo hizo tatu hata kama hapewi mtu yeyote, otherwise hakuna faida ya kuwa na adhabu ya kadi!
Lakini hiyo ni marekebisho yajayo kwa sasa hivi hakuna namna, ni TFF kuamua kwa mujibu wa kanuni iliopo na ushahidi uliopo mbele yao.
Huku kuzungazunguka ni kutaka kuficha au kuharibu ushahidi uliopo ambao unaonyesha Fakhi ana kadi 3!
Kwenye issue ya Haji Manara, alichofanya hakina tofauti na alichofanya Salum Mkemi kutoa povu kabla ya uamuzi wa Kamati ya Masaa 72, nimeshangaa sana unashindwaje kuiomba TFF iwaadhibu wote.
Ndolanga alisema hivyo kasahau enzi zake?"...TFF inaweza kuwa miongoni mwa taasisi mbovu zaidi hapa Tanzania...."
Ndolanga
Upande wangu upi? Manara alipaswa afunge bakuli lake hadi maamuzi yafanywe. Huwezi kuupepeta wakati vyombo vya maamuzi viko jioni huko ni kuleta ushawishi au vitisho na kwenye mazingira ya namna hiyo haki haiwezi kupatikanaNadhani umeongea kwa kulalia upande wako. Manara ametetea haki yake. Tatizo kubwa hapa ni TFF,tangu aingie Malinzi aliigeuza TFF kuwa kambi ya Yanga.Hili halina ubishi,tumeona maamzi ya marefa tangu misimu miwili iliyopita yakilalia upande wa kuisaidia Yanga. Hilo jambo limepelekea kuwa na timu mbovu ya taifa. Matokeo unayajua.Makocha walichagua wachezaji wa yanga badala ya wachezaji wa timu ya taifa. Haya unayolalamikia leo ni matokeo ya TFF ya upande ule. Dawa ni hii,TOA MALINZI hapo arudi kagera.
Mwenzetu hebu tuelimishe unachojua au nawe umenihukumu bila kujua?Mkuu unachokiandika hukijui, usihukumu kitu ambacho hukijui
Ukiwagusa mbogoyo inya mapembeSimba wa kitabuni bana
Vurugu na utovu wa nidhamu utafikiria kanywa chang'aaAlichokisema msemaji wa Simba, ni uvunjifu wa Amani.
Wote ni kuchukuliwa hatua kwa kuingilia uhuru wa vyombo vya kutoa maamuziRutashubanyuma....na ni vipi kuhusu upande wapili wa bandiko lako..?kumbuka kuna msemaji wa Yanga aliongea pia na akataja TAKUKURU...CYBER CRIME...TCRA...POLISI....nk
Kwanza walikuwa time barred.Tatizo lililopo hapa hapa ni watu kutazamana huyu Yanga huyu Simba so hata ukitoa maamuzi SAHIHI ILA yakaiumiza SIMBA Basi SIMBA watakuja Na lawama huyu yanga . Ilitufike tufuate kanuni Na SHERIA za mpira . mfano tuanzie Na malalamiko ya SIMBA kwamati ya masaa 72 je SIMBA walikuwa Na sifa kupeleka malalamiko Na Na kamati kujiridhisha kwamba hakuna kanuni imevunjwa kwa maana Hayo malalamiko ya SIMBA yapo ndani ya Masaa 72? Kama kamati ya Masaa 72 ilikaaa baada ya Masaa 72 kupita Basi Maamuzi Na kamati hiyo ni batili tukianzia hapo hatutafika hukuwalikofika . haijalishi hiyo kamati INA wajumbe wengi wa SIMBA au Yanga , wahaya au wachaga kama wanafuata kanuni hiyo ndio utamaduni wa Tz.
Sidhani ni ukilema wake wa ngozi bali ni majigambo na vitisho vya mtapatapa na maji haachi kutika!Huyu Manara anajivunia kwa sababu ni zeruzeru. Haiwezekani anaanza kutugawa kwa makabila yeti. Watanzania hatujawahi kugawanywa kwa makabila
TFF ni dhaifu sana walipaswa kwa wakati angelimwa barua ajieleze kwanini anaingilia uhuru wa vyombo vya kikatiba vya utoaji wa hakiHuyu manara achunguzwe kuhusu kauli yake anakoenda siko kabisa anatuhumu ukabila jambo sio la kweli kabisa. Wasimwache hivihivi
Teh! Teh! Teh!NINACHOFURAHI NI KUWA YALE YA LIGI DARAJA LA KWANZA MWAKA ULE WA GEITA NA POLISI TABORA SASA YAMEHAMIA KWENYE VPL 2016/2017. HAPA SIMBA PALE KAGERA SUGAR HUKU YANGA. NAMMIS MTU MMOJA ALITAJWA TAJWA SANA KWENYE LILE SAKATA HUWA NAMSIKIA PIA KWENYE NYIMBO ZA WAZEE WA NGWASUMA ANAITWA YUSUPH KITUMBO.... NATAMANI KUMUONA
Iko sheeeeda na hii yote watu wanapofanya kazi kutumika na tumbo street hawawezi kuwa na busara hata punje kidogoKinachoshangaza na kuleta hasira ni TFF hawajui ni mchezaji yupi mwenye kadi na yupi hana mpaka kumuita mchezaji na kumhoji.
Ndolanga alisema hivyo kasahau enzi zake?
Sorry, kabla hata ya maamuzi ya mwanzo simba kupewa point tatu Salum Mkemi mjumbe wa Yanga alifanya conference ili iwej,,,Tofauti huwezi kuiona kama huchambui hoja zangu
Utaratibu hautekelezeki kwa sababu kumbukumbu aidha zimepotea au wameziharibu makusudi. Sasa hizo taratibu utazitekeleza vipi kama hujui kama kweli mchezaji husika ana hata kadi moja ya njano achilia mbali tatu!