TFF kuweni na busara

TFF kuweni na busara

karim mtila

Member
Joined
Jan 14, 2015
Posts
16
Reaction score
34
Leo nataka kuizungumzia mamlaka inayosimamia mchezo wa miguu hapa nchini.

TFF ya karia kwa hakika imepata mafanikio kadhaa kama vile kushiriki Afcon Senior na junior, CHAN nk.Lakini pia kuboresha soka la wanawake.

Doa kubwa ambalo Rais Karia asipoangalia litamletea matatizo ni hii Issue ya kufungiafungia watu ovyo.

Sasa kila baada ya mwezi utaona taarifa ya mtu kufungiwa.Yaan sasa hivi ukisema kitu kidogo tu kuhusu TFF unafungiwa, hii ni ishara mbaya ya uongozi wa karia.

Najua maamuzi haya hayatoki moja kwa moja kwa karia lakini kwa mamlaka aliyonayo anaweza kuongea na wahusika wawe na busara. Sawa wanahukumu kwa mujibu wa kanuni lakin busara itumike.

Ile Issue ya kiongozi wa Lipuli kweli alikosea. but na wao TFF walikosa pia, Why pesa ya misimu miwili nyuma hawakulipa afu pesa kidogo tu, Kwa hasira wakamfungia yule jamaa wenyewe wanakula tu kuku.

Hii kamati ya maadili ijitafakari upya, Haya mambo hayana nafasi awamu hii ya Mama Samia.
 
Wanafungiana kwa hofu mwili nyumba atagombea uongozi TFf mbinu ya blatter kitambo sana ndio maana wanampa kifungo kirefu...
 
Ila ni lazima watz tujifunze ustaarabu, mtu anaweza kuwa anadanganya hadharani kwa maksudi ili kufurahisha mashabiki wake tu, alichokuwa anafanya Mwakalebela hasahasa kudanganya kuhusu inshu ya Morrison.
 
Back
Top Bottom