Mohamed Mbelwa
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 507
- 272
Na. Chiki Mchoma.
+255 712 885 999
Ni kama utata wa dereva wa boda boda au tax.
Pale ambapo ulimwambia utashukia sehemu fulani halafu mkifika sehemu hiyo anakwambia huko mbele siendi shukia hapa tulipokubaliana.
Mwingine hata umwambie nitakuongeza pesa basi yeye atajenga dhana kuwa una nia Ovu na wala siyo ile uliyoonesha awali.Huwezi kuzuia fikra za Mtu.
Yawezekana Simba haikuwa na makubaliano kama ya dereva tax au wa boda boda na TFF lakini ni dhahiri TFF inataka kuonesha kuwa imefikia tamati ya kushirkiana na Simba katika jambo hili la Kitaifa ambalo katika Wafaidika wakuu na TFF wamo.
Najenga dhana kuwa inawezekana kuwa kosa la Simba ni kule kusema tamaa yao ilikuwa ni kufika Robo Fainali na ambayo tayari wameshafika na sasa wameshamalizana na TFF ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiisaidia Simba kwa misingi ile ile ya Utaifa kwanza.
Simba imekuwa kwenye Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika na imekuwa inavuka hatua kwa hatua na TFF ilikuwa na Msaada sahihi na wa nia njema ambao si wao tu ila Nchi zote zenye timu zilizo Klabu Bingwa Afrika kupitia vyama vyao vya Soka vimekuwa vikisaidia Timu zao zilizo kwenye hatua hiyo.
TFF inataka kukwepa hoja ya Viporo vya Simba kwa kuilazimisha Simba kucheza kesho dhidi ya JKT.
Unajiuliza iwapo Simba itacheza kesho dhidi ya JKT kisha keshokutwa mchana ikasafiri kwa Masaa matano mpaka Dar es Salaam ikapumzika kisha Ijumaa ikafanya Mazoezi ambayo kimantiki hayatakuwa na tija yoyote kwa mechi ya Jumamosi dhidi ya TP Mazembe sijui hili ni kwa manufaa ya nani.
TFF kupitia Bodi ya ligi wangeweza kugonga hodi kwa Mkurugenzi wa Michezo Bw. Ammy Ninje na kumuuliza juu japo uungwana wa hilo.
Hili la iwapo Simba ikaibua majeruhi (hatuombei na hata TFF haiombei) au ikapata uchovu (fatique) utakaoipa timu ubora dhaifu wa mchezo wao dhidi ya Mazembe ninyi mtakuwa na nafasi kubwa ya kulaumiwa.
Zipo faida nyingi ambazo TFF inazijua kuwa zitakuwa zake moja kwa moja iwapo Simba itapewa nafasi ya kujiandaa vizuri kwa mechi hiyo inayokuja.
TFF hii ndiyo itakayoendelea kupata sifa ya mafanikio ya Vilabu vyake.
TFF hii ndiyo itakayopata Sifa ya Mafanikio ya Ligi yake.
TFF hii ndiyo itakayoendelea kupata Sifa ya hapo baadae Vilabu kuongezeka kwenye ligi za CAF.
TFF hii ndiyo itakayoendelea kupata 10% ya kila fedha ambayo Simba itapata kwa kuvuka kila hatua na kuzitumia pesa hizo kwa maendeleo ya Soka Tanzania.
Fikiria kuanzia hatua ya Makundi TFF imepata zaidi ya Milioni 200 kupitia mafanikio ya Simba kutoka CAF.
Al Ahly walikuwa na viporo si chini ya saba.
JS Saoura, As Vita nao walikuwa na viporo si chini ya saba...tatizo liko wapi??..
Ni kweli TFF inataka kukwepa lawama za Viporo huku ikipoteza mambo muhimu kabisa kwa Taifa kuelekea mechi za CAF..??
TFF tafadhalini sana...Msichoke kuisaidia Simba kwa manufaa ya Taifa.
Haijalishi walisema walitaka kufika Robo Fainali ya Klabu Bingwa hivyo nanyi Mjitosheleze kuwa Inatosha kuipa nafasi Simba ya kujiandaa.
Lawama mnazozikimbia zinaweza kuwaandama maradufu.
Chiki Mchoma.
Fanani.
Sent using Jamii Forums mobile app
+255 712 885 999
Ni kama utata wa dereva wa boda boda au tax.
Pale ambapo ulimwambia utashukia sehemu fulani halafu mkifika sehemu hiyo anakwambia huko mbele siendi shukia hapa tulipokubaliana.
Mwingine hata umwambie nitakuongeza pesa basi yeye atajenga dhana kuwa una nia Ovu na wala siyo ile uliyoonesha awali.Huwezi kuzuia fikra za Mtu.
Yawezekana Simba haikuwa na makubaliano kama ya dereva tax au wa boda boda na TFF lakini ni dhahiri TFF inataka kuonesha kuwa imefikia tamati ya kushirkiana na Simba katika jambo hili la Kitaifa ambalo katika Wafaidika wakuu na TFF wamo.
Najenga dhana kuwa inawezekana kuwa kosa la Simba ni kule kusema tamaa yao ilikuwa ni kufika Robo Fainali na ambayo tayari wameshafika na sasa wameshamalizana na TFF ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiisaidia Simba kwa misingi ile ile ya Utaifa kwanza.
Simba imekuwa kwenye Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika na imekuwa inavuka hatua kwa hatua na TFF ilikuwa na Msaada sahihi na wa nia njema ambao si wao tu ila Nchi zote zenye timu zilizo Klabu Bingwa Afrika kupitia vyama vyao vya Soka vimekuwa vikisaidia Timu zao zilizo kwenye hatua hiyo.
TFF inataka kukwepa hoja ya Viporo vya Simba kwa kuilazimisha Simba kucheza kesho dhidi ya JKT.
Unajiuliza iwapo Simba itacheza kesho dhidi ya JKT kisha keshokutwa mchana ikasafiri kwa Masaa matano mpaka Dar es Salaam ikapumzika kisha Ijumaa ikafanya Mazoezi ambayo kimantiki hayatakuwa na tija yoyote kwa mechi ya Jumamosi dhidi ya TP Mazembe sijui hili ni kwa manufaa ya nani.
TFF kupitia Bodi ya ligi wangeweza kugonga hodi kwa Mkurugenzi wa Michezo Bw. Ammy Ninje na kumuuliza juu japo uungwana wa hilo.
Hili la iwapo Simba ikaibua majeruhi (hatuombei na hata TFF haiombei) au ikapata uchovu (fatique) utakaoipa timu ubora dhaifu wa mchezo wao dhidi ya Mazembe ninyi mtakuwa na nafasi kubwa ya kulaumiwa.
Zipo faida nyingi ambazo TFF inazijua kuwa zitakuwa zake moja kwa moja iwapo Simba itapewa nafasi ya kujiandaa vizuri kwa mechi hiyo inayokuja.
TFF hii ndiyo itakayoendelea kupata sifa ya mafanikio ya Vilabu vyake.
TFF hii ndiyo itakayopata Sifa ya Mafanikio ya Ligi yake.
TFF hii ndiyo itakayoendelea kupata Sifa ya hapo baadae Vilabu kuongezeka kwenye ligi za CAF.
TFF hii ndiyo itakayoendelea kupata 10% ya kila fedha ambayo Simba itapata kwa kuvuka kila hatua na kuzitumia pesa hizo kwa maendeleo ya Soka Tanzania.
Fikiria kuanzia hatua ya Makundi TFF imepata zaidi ya Milioni 200 kupitia mafanikio ya Simba kutoka CAF.
Al Ahly walikuwa na viporo si chini ya saba.
JS Saoura, As Vita nao walikuwa na viporo si chini ya saba...tatizo liko wapi??..
Ni kweli TFF inataka kukwepa lawama za Viporo huku ikipoteza mambo muhimu kabisa kwa Taifa kuelekea mechi za CAF..??
TFF tafadhalini sana...Msichoke kuisaidia Simba kwa manufaa ya Taifa.
Haijalishi walisema walitaka kufika Robo Fainali ya Klabu Bingwa hivyo nanyi Mjitosheleze kuwa Inatosha kuipa nafasi Simba ya kujiandaa.
Lawama mnazozikimbia zinaweza kuwaandama maradufu.
Chiki Mchoma.
Fanani.
Sent using Jamii Forums mobile app