TFF na Bodi ya Ligi sitisheni kwa muda matumizi ya uwanja wa Sokoine Mbeya

TFF na Bodi ya Ligi sitisheni kwa muda matumizi ya uwanja wa Sokoine Mbeya

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
33,092
Reaction score
96,127
Nimetoka kuangalia mechi ya mtoano, Kombe la Shirikisho la Azam muda si mrefu kati ya Tanzania Prisons vs Polisi Tanzania, na ambako Polisi Tanzania wamefanikiwa kusonga mbele kwa ushindi wa goli 2 kwa 0 dhidi ya Tanzania Prisons.

Kiukweli uwanja umeharibika vibaya kiasi cha kudhani labda wachezaji wanacheza kwenye jaruba la kupandia mpunga (kwa wakulima wa zao la mpunga watanielewa).

Ni aibu uwanja kama huu kuendelea kutumika ukiwa katika mazingira mabovu kiasi hiki! Na pia ni aibu kwa Serikali kuendelea kuruhusu CCM kuvimiliki hivi viwanja kinyume kabisa na matakwa ya Watanzania tulio wengi, huku ikishindwa kuviboresha! Badala yake inakusanya tu mapato, na kuyatumia katika matumizi yao binafsi!

Nashauri viwanja vyote ambavyo CCM imevikwapua baada ya Nchi kuingia kwenye mfumo wa Vyama Vingi, virudishwe kwenye Halmashauri zetu! Ili viweze kuendelezwa kwa manufaa ya Watanzania wote.
 
Viwanja Vimebadilishwa Dhima Yake Vimekuwa Vinajali Mikutano Ya Kisiasa Na Si Michezo.

Kuna Matukio Mengi Huwa Yanashangaza Sana Kama Siku Moja Kuwe Na Ratiba Ya Mkutano Sambamba Na Mchezo Kuchezwa.

Maajabu Mchezo Utapelekwa Mbele Na Mkutano Utapewa Kipaombele. Yaani Wakusanyike Wakiharibu Kiwanja Then Mechi Ndio Ichezwe.

Kwa Hali Hiyo Hata Ukarabati Hatuwezi Tegemea Kufanyika Na Hata Ikifanyika Si Ya Kiwango Chake.
 
Ukitoa Kiwanja cha Manungu Complex, kinachofuatia kwa ubora ni Sokoine Mbeya.

Na hivi karibuni kuna mpango wa kuweka VAR, ndo lengo kuu kwa sasa, kwani hukusikia kauli ya Waziri Mwigulu?
 
Nimetoka kuangalia mechi ya mtoano, Kombe la Shirikisho la Azam muda si mrefu kati ya Tanzania Prisons vs Polisi Tanzania, na ambako Polisi Tanzania wamefanikiwa kusonga mbele kwa ushindi wa goli 2 kwa 0 dhidi ya Tanzania Prisons...
Hawawezi kuufungia wanamuogopa tulia
 
Halmashauri ya jiji ijichange ijenge uwanja. Timu zimekuwa nyingi hapo.
Kweli kabisa timu zimekuwa nyingi sana na zinaenda kuongezeka zaidi bora halmashauri ya jiji wajiongeze ili timu ziachane kabisa na uwanja wa Sokoine
 
Nimetoka kuangalia mechi ya mtoano, Kombe la Shirikisho la Azam muda si mrefu kati ya Tanzania Prisons vs Polisi Tanzania, na ambako Polisi Tanzania wamefanikiwa kusonga mbele kwa ushindi wa goli 2 kwa 0 dhidi ya Tanzania Prisons...
Yanga mnaogopa nini sokoine?
 
Jibu ulichoulizwa mechi na mbeya kwanza yanga walichezea kwenye uwanja wako? Usipanue mdomo kuongea usichokijua kijana ni bora ukae kimya kutunza heshima yako
safari njema

16CE80A1-F10E-46BE-A69F-A0DA51B62348.jpeg
 
uendelee kutumika mpaka utopolo wacheze na wao kule mbeya
Simba, azam na kmc walishamaliza kibarua chao kule bado uto

Yanga ya msimu huu inapiga nje ndani! Ikifungwa, basi ni sare. Hivyo haiwezi kuogopa kucheza viwanja vya nje.

Tatizo ule uwanja umefikia kiwango cha mwisho kabisa cha ubora! Kiukweli haufai kuchezea hata mashindano ya bonanza.
 
Halmashauri ya jiji ijichange ijenge uwanja. Timu zimekuwa nyingi hapo.

Naunga mkono hoja! Tena ikiwezekana Halmashauri zote Nchini zifanye kama walichofanya wenzao wa Geita.

Kuna uwanja wenye ubora wa hali ya juu sana kule unakaribia kumalizika, kwa ajili ya timu yao ya Geita Gold FC.
 
Nilikuwa Natazama hiyo mechi
mwenyewe Nilikuwa najihisi Aibu sana
mpaka Najiuliza hivi Viongozi Wana tazama vizuri tu nahawana Aibu
Hapa Ilikuwa DK 20 tu
sasa Kipindi cha pili ilikuwa Majanga majanga
IMG_20220215_163156_5_1644931945569.jpg
 
Nilikua naangalia hiyo mechi hii nchi inashida sana nimeshangaa uwanja ule unatumikaje kwenye mashindano yanayotambulika kama haya!!!

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app

Halafu mechi imerushwa live! Yaani ni aibu kwa TFF, Bodi ya Ligi, CCM na Serikali yake. Ni bora wakaufungia tu kwa muda.
 
Back
Top Bottom