Thabo Bester maarufu 'Mbakaji wa Facebook' na Dkt. Nandipha Magudumana wakamatiwa Arusha Tanzania. Wafahamu kwa undani wapenzi hawa

mbona hamjafafanua vizur inaonekana mwamba ana profile ya hatari na ya kutuletea hapa jukwaani namna alivyokuwa akitekeleza huo ubakaji na uuaji na picha zake pia ila hapa naona mnatangaza kikawaida sana
Mimi hata siwaelewi maana wanaongea ongea vitu vya kusadikika hawatoi profile kamili ya huyu jamaa ipoje, ana matukio mangapi, ameua watu wangapi na amebaka wangapi, history yake ni ipi.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Ila wanawake wa kizazi hiki hawanaga akili hata wasome. Tena waliosoma ndio changamoto mara mbili. Huyu Dada anajua kabisa jamaa ni convicted felonist hata kama ni mwanaume ambaye alishawahi date nae before ila kwasasa ana rekodi mbaya ya uhalifu.

Hii hali inaitwa Hybristophilia ukisoma utaelewa ni ujinga ujinga wanawake wanapenda kufanya ili wajisikie vizuri.


Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Please weka Aya maana kusoma reply ndefu bila aya inachosha macho.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
VIPI WALIOMPIGA RISASI TUNDU LISSU na KUMTEKA MO wamewapata au mpaka zamu ya Makachero wa South afrika?
[emoji23][emoji23][emoji23]wewe unaongelea waliomchapa risasi tundulissu, je wale walimfanyia ukatili dokta ulimboka nusu ya kumuua akavimba mwili mzima, kisa kutetea masilahi ya madaktari. Ulisikia popote wameongelewa tena. [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Najiuliza huyu hamlifu amepitaje katika borders zetu inamaana hatuna ukaguzi wa kutosha. Hatuna facial recognition system ambazo zinaweza mtambua mhalifu hata kama si wakwetu.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Wewe unaongea vitu gani wewe?!

1. Wameshiriki kumtorosha mhalifu hatari jela.

2. Huyo dada ametumia profession yake ya udaktari kufoji taarifa muhimu za vipimo juu ya mwili ambao anajua wazi si wa muhusika.

3. Huyu dada kwasasa anakuwa ni mhalifu sababu ya kushirikiana na mhalifu ambaye anajua wazi kuwa jamaa ni hatari na ana matukio hatari.

4. Amekuja kwenye mipaka ya taifa jingine yaani Tanzania na kumvusha huyu mhalifu huo ni uhalifu pia sababu mbali na kwamba anasafirisha mtu hatari ila anadanganya mamlaka zetu za mipaka juu ya identity ya muhusika.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Unawasifu bure. Huyu walisham-trace aliko na wakapewa tu taarifa. Hawakufanya lolote special
 
Huyu watabadilishana na askari wa B4 aliywtorokea south

Wasauzi wanamtaka Thabo na sisi tunamtaka soja wetu aliyepo kwao

Ngoja tuone mifumo ya haki jinai (criminal justice system) ya nchi hizi mbili zipo huru kiasi gani kuachiwa kufanya kazi zake .

Mfumo huru wa haki jinai unataka mamlaka zinazotuhumu watuhumiwa kufikishwa ktk vyombo husika uhamiaji, polisi kisha kupelekwa mbele ya mahakama na sheria kufuata mkondo wake.

Ndiyo maana mawaziri wa Afrika ya Kusini jenerali Bheki Cele waziri wa polisi na Bw. Ronald Lamola waziri wa sheria pamoja na vyuo vya mafunzo (magereza) wanesema serikali ya Afrika ya Kusini imetuma ujumbe mzito wa maafisa kuja Tanzania kuona namna gani wanaweza kuwapata wapenzi hawa wawili ktk uhalifu huku wakisema kuwa ushiriki wa raia wa Mozambique Zakaria Alberto ni suala lingine mtambuka pengine hana uhusiano wa kiuhalifu na Thabo Bester au Dr. Nandhipha Magudumana.

Kuhusu suala la askari polisi wa Tanzania anayetuhumiwa kuhusika na kufuja bilioni 4 za mfuko wa maziko wa jeshi la Polisi la Tanzania bado kama kawaida ya mfumo wa haki jamii wa Tanzania.

Upande wa serikali yetu Tanzania 'ukikamatwa' mtuhumiwa hupotea ndani ya mfumo wa haki jinai bila vyombo vya habari au jamii na jamaa kupata mrejesho vyombo vinafanya kazi kesi husika kwa namna ipi, uchunguzi umefika hatua gani wala yepi wanayafahamu baada ya mahojiano n.k .

Kwa maneno mengine mfumo wa haki jinai Tanzania wanafanya kazi zao kwa usiri na kufunikafunika bila kutoa taarifa za kina kwa umma wa Tanzania hata wa kimataifa siyo tu kuhusu Thabo Bester au askari polisi wa Tanzania aliyeko Afrika ya Kusini wana mpango gani mkono mrefu wa sheria kumfikia.


 
Nimeweza kuelewa hapa kwamba inabidi extradiction ifanyike kwa mfumo wa sheria bila kuwepo na veto za maamuzi nje ya mfumo wa mahakama

Lakini kwa namna dola yetu ilivyojimilikisha haki ya kuishi na kufanya maamuzi kwa niaba ya maisha utasikia jamaa kassfirishwa huko
 
Hii ni mbaya sana yaani unaratibu mauji ya mtu asiye na Hatia Kwa kuchoma gereza Ili tuu wewe utoroke gerezani.

Kuna mashaka sana na security appatus za Afrika Kusini.

Reference: Thabo Bester and Spouse Dr Nandipha Magadugula.

=======

Tanzania Police have confirmed the arrest of South African prison escapee Thabo Bester and his accomplice Dr. Nandipa Magudumana and one other person by the name of Zakaria Alberto.

In a short statement released by the Police Spokesperson David A Misime, Tanzania Police said they are finalizing, “other international and national procedures” for the case.

Thabo Bester, a serial rapist, scammer, and murderer was confirmed to have escaped Mangaung Prison in South Africa in March 2023 after a viral Twitter picture that showed him shopping. It was later learned that Bester had escaped prison in May 2022 in a ploy that involved fake suicide.

Prison cell where Bester was kept had caught fire only for his corpse to be found burnt beyond recognition. Bester was pronounced dead, only for the news to resurface on social media that he was living large with South African celebrity Doctor, Nandipa Magundumana.

Reports show it was a complex scheme that involved Dr Nandipa Magundumana who collected the burnt corpse from prison, claiming she was the wife of Thabo Bester.

Confirming the arrest of Thabo Bester, South Africa Minister of Justice and Correctional Services Ronald Lamola, says he is expecting to be in Tanzania on Sunday, April 09, 2023, to follow up on the case.

“We have confirmed with all relevant authorities in Tanzania which include the national Police in Tanzania and Interpol that fugitives have been processed in the Tanzania criminal justice system,” said Lamola in a press statement.
 
Hao ni majasusi wa dunia.

Mbaya kuua mtu ili wewe uokoke, mbaya zaidi mbele za Mungu pia.

All in all polisi wa tz wako vizuri, naogopa kusema CONGRATULATIONS.

Angesogea hapo kwa Uhuru asingekamatwa mpaka afe kweli kweli.
 
... SA walifuta adhabu ya kunyonga adhabu pekee aliyostahili Bester! Angekatiwa hiyo adhabu na ikatekelezwa inavyopaswa bila figisu shida zote hizi za kuhangaika naye zingeshasahaulika zamani. Adhabu ya kunyonga bado ina umuhimu mkubwa duniani.
 
Hao ni majasusi wa dunia.

Mbaya kuua mtu ili wewe uokoke, mbaya zaidi mbele za Mungu pia.

All in all polisi wa tz wako vizuri, naogopa kusema CONGRATULATIONS.

Angesogea hapo kwa Uhuru asingekamatwa mpaka afe kweli kweli.
Hiyo ni kazi ya Interpol, ndiyo wanaotoa descriptions na ndiyo wanao ongoza msako lakini arresting hufanywa na askari wa nchi husika (aliyokamatiwa) hata taarifa hutolewa na nchi ambapo mharifu amekamatiwa.
Wakati mwingine inaweza isiwe interpol lakini ikawa ni joint mission
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…