mabuba
Senior Member
- Dec 5, 2006
- 133
- 90
Thamani tena hakuna, yameachwa nje,
Usiri tena hakuna, yameachwa nje,
Aibu tena hakuna, yameachwa nje,
Ustaarabu tena hakuna, yameachwa nje.
Balehe ilipofika, yalitunzwa hakika,
Binti aliyefiki, elimishwa pasi taabika,
Kuyatunza bila kukimbilia, aibu akaja sononeka,
Aibu tena hakuna, yameachwa nje.
Umri ukifika, chakula mtoto chake,
Baba naye afaidika akiwa mahala pake,
Madodo yanapukutika, mengi kwa makeke,
Thamani tena hakuna, yameachwa nje.
Wadada na wamama, sasa wameyaachia,
Wajidai yamesimama, winchi wameyapigia,
Hata yaliyo mraba, pembe tatu yajiitia,
Usiri tena hakuna, yameachwa nje.
Uchina wameyaendea, kuyatia hamirani,
Ukubwa wameyatakia, ilikuleta tafrani,
Madodo twakimbilia, hata yaliyokuzimuni.
Ustaarabu tena hakuna, yameachwa nje.
Yameachwa nje, wenyewe waita usasa
Wazi wayaanike, hata mbele ya ibada
Waenda kifua mbele, pasi kuona karaha
Yameachwa nje, wenyewe waita usasa
Na mengine mistari, mingi imeshamiri
Wapo wanaodiriki, kuyaanika ukweni
Maradhi yametamaraki, usia nawapeni
Na usasa jihadhari, kubaya utawapelekeni
Yameachwa nje, wenyewe waita usasa
Usiri tena hakuna, yameachwa nje,
Aibu tena hakuna, yameachwa nje,
Ustaarabu tena hakuna, yameachwa nje.
Balehe ilipofika, yalitunzwa hakika,
Binti aliyefiki, elimishwa pasi taabika,
Kuyatunza bila kukimbilia, aibu akaja sononeka,
Aibu tena hakuna, yameachwa nje.
Umri ukifika, chakula mtoto chake,
Baba naye afaidika akiwa mahala pake,
Madodo yanapukutika, mengi kwa makeke,
Thamani tena hakuna, yameachwa nje.
Wadada na wamama, sasa wameyaachia,
Wajidai yamesimama, winchi wameyapigia,
Hata yaliyo mraba, pembe tatu yajiitia,
Usiri tena hakuna, yameachwa nje.
Uchina wameyaendea, kuyatia hamirani,
Ukubwa wameyatakia, ilikuleta tafrani,
Madodo twakimbilia, hata yaliyokuzimuni.
Ustaarabu tena hakuna, yameachwa nje.
Yameachwa nje, wenyewe waita usasa
Wazi wayaanike, hata mbele ya ibada
Waenda kifua mbele, pasi kuona karaha
Yameachwa nje, wenyewe waita usasa
Na mengine mistari, mingi imeshamiri
Wapo wanaodiriki, kuyaanika ukweni
Maradhi yametamaraki, usia nawapeni
Na usasa jihadhari, kubaya utawapelekeni
Yameachwa nje, wenyewe waita usasa