Thamani ya Maisha ni furaha,sio pesa au kitu chochote.

Thamani ya Maisha ni furaha,sio pesa au kitu chochote.

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,340
Reaction score
4,659
Leo nilikuwa na bando la kuchezea nimejikuta naangalia video za vichekesho/vijana wanaoitwa machawa Baba Levo,Mwijaku na Huyu Doto Magari nimeona jinsi gani hawa jamaa wanavyoishi kwa ujanja ujanja kwa kutumia vinywa vyao kuzusha misamiati,kujichekesha hovyo na kutoa maneno ya kufurahisha jambo ambalo linawafanya kuwa maarufu.

Nikakumbuka kumuangalia Haji Manara alipokuwa Msemaji wa Simba na zile kauli zake za kubeza na kukejeli watu walikuwa wanaenjoy na kucheka sana,niliona umaarufu mkubwa kwake kupitia talanta ya kubwabwaja.

Video zikanipeleka mbele zaidi nikamuangalia jamaa Ahmed Ally anavyoongea hapo nikabaini kuwa jamaa anajijenga na kujibrand kupitia mdomo wake,kauli zake ni mtu kama mchekeshaji hivyo inawafanya watanzania wengi wamuangalia,Ally Kamwe naye vile vile woote hawa wanaingiza Sanaa ya uchekeshaji na utani.

Nimegundua kuwa Watu wengi kwa sasa wamejawa stress hivyo wanategemea mitandao ya kijamii kujiliwaza huku wengine wanatumia gap kuingiza pesa zaidi.

Furaha ni jambo la msingi watanzania wanaridhika ukiweza kuwadanganya na kuwachekesha.

ILA MWAMBIENI BABA LEVO NA MWIJAKU WAACHE KUOMBA HOVYO
 
Back
Top Bottom