"Zakumi, post: 29975965, member: 12016"]Wakati Mwalimu Nyerere alipokuwa hai, kubadilisha katiba ilikuwa ni kama kufanya njama za kufuta legacy yake. Hivyo hakuna aliyejaribu jambo hilo bila kupata baraka zake.
Mkuu kuna wakati namwelewa Mwalimu Nyerere hasa kuhusu katiba
Mwl alipochukua nchi ni kama mtu aliyekadhiwa kijiji kisicho na shule
Kazi ya kwanza ilikuwa kujenga utaifa, kisha kuwaunganisha watu.
Tunaweza kutokubaliana na sera zake nyingi lakini ukweli utabaki pale pale yapo aliyoyafanya tusiyoyaona na tusiyoyajua ndiyo yanatuweka tuwe kama tulivyo
Nchi ikipata uhuru ilikuwa na makabila 120 na dini mbali mbali.
Kazi ya kuunganisha watu haikuwa rahisi, ilihitaji mwelekeo na kuvumiliana
Leo miaka 50 tunaona matatizo Kenya na kwingine ambako makabila si zaidi ya 30
Nigeria imekuwa katika mapinduzi kuanzia Nandi Azikiwe hadi leo hii.
Katika miaka 50 tu iliyopita nchi hiyo haikuwa na utulivu licha ya utajiri wa mafuta, watu na rasilimali nyingine. Tunaona tofauti za udini na ukabila 'in black and white'
Ukitaka kuona matatizo yaliyokuwepo na ambayo kama Mwalimu asingekuwa imara yangetuacha baya ni ''1964 Mutiny', askari hawakujua wanataka nini
Kwamba sasa mzungu kaondoka ni wakati wao, jaribio lililoshindwa
Kuundwa kwa Azimio la Arusha ilikuwa ni sehemu ya suluhu ya ''Africanization'
Hivyo Mwl alihitaji katiba itakayompa madaraka makubwa ili kukabili upinzani uliotishia utaifa. Hilo kama ni kosa au la ni suala la mjadala
Hata hivyo miaka mingi baadaye Mwl alionekana kuridhika na uwezo wa watu kuhimili vishindo vya siasa za upinzani. Tena ukianzia ndani ya chama chake
Upinzani ukianza ali 'set tone nzuri' sana. Unakumbuka aliposema 'mtu abebwe kuna kosa gani? Unakumbuka aliposema maandamano yana matatizo gani
Ni 'tone hiyo' ndiyo iliwazuia waliofuata kukubali siasa za ushindani bila kuhasimiana
Tukitaka katiba itakayokidhi mahitaji na wakati wa sasa, ni lazima legacy za Ujamaa, Chama kimoja na Azimio la Arusha viwekwe kando.
Haya mambo yamewekwa kando siku nyingi sana.
Ujamaa haupo ulifutika wakati wa Mwinyi , Mkapa akapigilia msumari na akina JK wakasawazisha tu
Azimio la Arusha lilipigwa mweleka kule Zanzibar siku nyingi na ndilo chimbuko la ubadhirifu na ufujaji wa mali za umma. Chama kimoja kilifutwa baada ya upinzani
Hata hivyo CCM ni wazuri sana wa kutumia hoja za ujamaa, Azimio na chama kimoja pale ambapo masilahi yao yanapokuwa matatani
Ni kama wanavyomtumia Mwalimu pale wanapohitaji kujenga hoja na si kumuezi
Ukiwakusanya CCM katika kamati kuu , Halmashauri kuu na makada wazoefu ukauliza nini itikadi ya chama, nakuhakikishia utapata itikadi tofauti zaidi ya 100 kwa saa 1.
Hakuna anayeweza kueleza nini chama kinasimamia
Pamoja na legacy za mwalimu, CCM ni chama cha wanasiasa wa kulipwa. Katiba ya kweli itawafanya CCM kupoteza nguvu na kukosesha kazi watu waliozoea kupata ulaji kupitia CCM. Sababu ya CCM kuvumiliana, sio kuonyesha upevu wa kisiasa. Bali kusubiriana hili wale kwa zamu
Absolutely! Ni chama ambacho ima unasubiri muda wako au unataka masilahi yako yalindwe
Sababu kubwa ya kuipiga vita rasimu ya Warioba na kutotaka kuzungumzia katiba ni hofu ya kupoteza madaraka, nadhani si kukosa nguvu haipo hata muda huu.
Nguvu ya CCM imebaki katika kulindwa na dola ni si wanachama
Rais Kikwete aliwaambia wazi, ni lazima chama kipendwe na si kulindwa