The Best FIFA Football Awards 2019: Messi atwaa tuzo ya Mchezaji bora, Klopp awa Kocha bora

The Best FIFA Football Awards 2019: Messi atwaa tuzo ya Mchezaji bora, Klopp awa Kocha bora

Halafu ndugu yangu vigezo vyote alivyoshindia Messi kwa mujibu wako ni hivyo hivyo walitumia UEFA. Messi anacheza mpira europe vipi kule ashindwe kabla ya miezi miezi miwili leo awe mshindi. utasema UEFA wamekosea na mimi nitasema FIFA wamekosea.
Sio kweli vigezo vya UEFA sio sawa na vigezo vya FIFA.
UEFA wanaangalia mashindano ya UEFA tu lakini FIFA wanaangalia mashindano yote.
Pia hawaangalii umechukua nini kama timu wanaangalia umefanya individually
 
Sidhani kama tunatofautiana sana, FIFA wamekuwa hawaeleweki katika formula yao kwa maana kukiwa na makosa mengi hata mengine yataulizwa. Sasa ukiangalia top voted players mwaka huu majina utakuta Mohd Salah na Sadio Mane wameshika nafasi ya 4 na 5 lakini hawa wachezaji hawako kabisa katika 11 players of FIFA. Hakuna ubishi wa uwezo wa Messi tatizo kama UEFA wameangalia UEFA na Nation league walimuonea Messi sababu hakushiriki Nation league. ikiwa FIFA wanatizama kufunga sana magoal na kusaidia team basi mwaka jana angechukuwa Mo Salah. alipewa Modric kwa sababu alichukuwa alisaidia UEFA Madrid hakuwa mfungaji bora leo tunasema hapana Messi kafunga magoal mengi na assist. angepwa golden boot sio as best last season.
Ahahahaha we jamaa Modric na Salah msimu uliyopita alikua bora sana Salah kweli?
Angalia performance ya modric UEFA msimu uliyopita na kombe la dunia afu uje hapa na hizo statistics zako
 
Ningeomba unijibu swali langu
Hivi Modric mwaka jana ilikua ni individual au Team performance?

Kwangu thats was a big mistake kumpa uchezaji bora Modrid, he ddnt deserve kubeba ile tuzo mwaka jana, hakuwa na kiwango bora cha kubeba ile tuzo

kwa last year ile tuzo Mohamed Salah alistahili na sio Modric, nadhani nitakuwa nimekujibu vizuri.

Note: sijataka kuzungumzia kama ni team perfomance au individual perfomance kuz sikuafiki matokeo yale japo wapiga kura ndio wenye maamuzi.

Kuna muda yatupasa kukubali kuwa saa nyingine wapigaji wa hizi kura nao wana mapenzi yao.

Kama umeona zile graph ambazo fifa wametoa Messi kawapita kwa mbali sana Virgil na Ronaldo.
 
Modric alikua bora kuliko CR7 na Messi. Mpira alioupiga ndani ya World Cup ni waheshima kabisa. Wakati alipokua akilitawala duara Messi alikua mtalii uwanjani anazunguka tu.

Mpira mchezo wa takwimu mzee baba, Je modric ni kiungo mkabaji au mshambuliaji?

Kama ni kiungo mshambuliaji, Je alikuwa na assist ngapi kwenye UCL, La liga na World Cup last season?

Kama ni kiungo mkabaji, Je alipokonya mipira mara ngapi kwenye hizo competition zote?

Je alipiga accurate pass ngapi? Unaposema alikuwa anatawala dimba la kati uwe na takwimu pia, kama huna takwimu utakuwa mbabaishaji, Kwa Worldcup kwangu Pogba alicheza vizuri sana than Modric na bila kupepesa macho kabisa nakiri kwa kusema Kylian Mbappe ndio alikuwa mchezaji bora wa mashindano.
 
Sidhani kama tunatofautiana sana, FIFA wamekuwa hawaeleweki katika formula yao kwa maana kukiwa na makosa mengi hata mengine yataulizwa. Sasa ukiangalia top voted players mwaka huu majina utakuta Mohd Salah na Sadio Mane wameshika nafasi ya 4 na 5 lakini hawa wachezaji hawako kabisa katika 11 players of FIFA. Hakuna ubishi wa uwezo wa Messi tatizo kama UEFA wameangalia UEFA na Nation league walimuonea Messi sababu hakushiriki Nation league. ikiwa FIFA wanatizama kufunga sana magoal na kusaidia team basi mwaka jana angechukuwa Mo Salah. alipewa Modric kwa sababu alichukuwa alisaidia UEFA Madrid hakuwa mfungaji bora leo tunasema hapana Messi kafunga magoal mengi na assist. angepwa golden boot sio as best last season.

Naungana na wewe kabisa na hata post yangu kabla ya hii nimekubali kabisa kuwa last season Mohamed Salah alistahili kupewa ile tuzo na sijui walitumia kigezo gani kumpa Modric, wapiga kura ndio wanajua hilo.

Tukija kwenye perfomance ya mchezaji kwa mtazamo wangu ni kwamba pamoja na mchezaji kutobeba makombe doesnt mean hakuperfom vizuri, kuna muda wachezaji wanakuwa kwenye ubora sana ila timu wanazochezea zinakuwa kwenye viwango vibovu ndio maana nikasema PFL msimu uliopita waliopiga kura walifanya sahihi kabisa, pamoja na liverpool kutobeba uefa ila Virgil alikuwa bora ndio maana akapewa ile tuzo na hata msimu ule mwingine pamoja na De Bruyne kuwa kwenye ubora ila ubora wake haukumfikia Mohamed Salah na ndio maana alipewa tuzo ya uchezaji bora wa EPL
 
We ndio haujui na umeropoka.
UEFA inaangalia sana sana club bingwa ulaya.
Wanatizama je umechukua club bingwa ulaya ama laah?
Kama wanaangalia hadi team ya taifa messi ni Latino sio European inamaana watachukua takwim za Copa America walete Uefa?!
Uefa wanatizama uchukuaji vikombe.
Ndio maana VVD ameweza Kuwa mchezaji bora kwa vigezo vya kuchukua kombe la club bingwa ulaya.
Lakini km wangekua wanatizama over all performance bila kuchukua kombe basi messi angestahili .
Lakin kwasababu wanatizama makombe UEFA basi messi hiko kigezo kakosa.
Tukija kwa FiFa best player wanatizama performance nzima ya mchezaji.
Na ukiangalia hakuna mchezaji alomzidi messi sio ktk league wala uefa.
We jamaa ktk league Laliga wamemchambua league ilivyoisha ameshinda magoli ya faulo (free kick ) yanafika 13.
Nitajie mbuzi yeyote aliyefanya hvyo.
Ktk laliga hiyo hiyo ameshinda magoli ya kuiokoa barca ya comeback 10+,nitajie kunguni yeyote aliyefanya hivyo.
Halafu km kweli unaufatilia mpira messi toka acheze uefa kuna zile rates za performance ktk mechi.
Messi amekuwa akipata rate ya 8.0% mpk nusu fainali alipotolewa akawa amepata rate ya 6%.
Inamaana hakuna mchezaji alo maintain kiwango kama messi.
Hata van dijk ameshindwa kufanya hilo.
Messi achaneni naye ninyi achaneni naye kabbisa.
Huu msimu ni wake.
Na ballon d'or watampa tu.
Hizi nondo kama kuna mpinzani atakayetaka akupinge hakika anapenda ubishi.
 
Kwahiyo unataka kuniambia Modric alikuwa na kiwango bora kuliko CR7 na MESSI?

Na unataka pia kuniambia WESLEY alikuwa na kiwango bora kuliko MESSI mwaka 2010? Kwa lipi na kipi alichofanya?

Je unafahamu kuwa Makombe ni overall perfomance ya team mzima na sio mchezaji mmoja?

Je unakubaliana nami kuwa unaweza ukawa na wavunja kuni na kubeba makombe ila kazi yao ikawa ni kuzuia na kusubiri penalty kama GREECE au PORTUGAL?

Je unajua kuwa tuzo hupewa kwa kuzingatia overall perfomance ya mchezaji na sio overall perfomance ya team?

Tatizo wengi wetu tunachanganya kati ya team perfomance na individual perfomance na pia tunashindwa kuelewa kuwa tuzo ya uchezaji bora wa Dunia ni individual perfomance na sio team perfomance.

Narudia tena, Nje ya kubeba UCL kwa msimu huu VIRGIL is nothing, ni sawa na KOULIBALY tu, Bernado Silva alikuwa na msimu bora kuliko VIRGIL kwa individual perfomance.
Nashindwa kuelewa, kwa maelezo yote haya wao hawaelewi sehemu ganiiii????
 
Hivi kuna watu bado mnazitilia maanani kabisa kiasi hizi tuzo mpaka mnamwagana mapovu hapa?

Hizi tuzo zilishapoteza maana siku nyingi sana... Binafsi niliacha kuzichukulia serious hizi tangu mwaka 2012.

Kabla ya hapo ndio tulikuwa tunaona mshindi akiapatikana kwa uhalali ambapo kilichokuwa kinaamua ni vigezo vya kimpira na hata malalamiko yalikuwa sio mengi.

Siku hizi tuzo hizi zinatolewa kwa misingi ya kisiasa na kibiashara na wala sio mpira tena. Vigezo vya kimpira vinachukuliwa kwa juu juu tu na havina uzito kama jinsi ambavyo vigezo vya kibiashara vinapewa uzito kwenye maamuzi.

Sasa ya nini mtu ukae unatunisha misuli ya shingo kwa jambo ambalo linaendeshwa kisiasa,kibiashara na utashi wa watu binafsi!?

Kama kweli hizi tuzo zingekuwa haziendeshwi kibiashara zaidi wala kisiasa, yaani kama kinachozingatiwa ni football facts mtu kama Bernardo Silva alikuwa sio wa kukosa kwenye shortlist. Lakini cha ajabu hata kwenye 5 bora tu hayumo, sasa si ni upuuzi huo?

Hao mabwana wawili tunaendelea kuwaona wakipokezana hii tuzo mpaka wanauacha huu mpira haijalishi wameshinda goli moja,wameshinda kombe la mbuzi,wamecheza mbili au wametoa assist pekee tu. Sababu tuzo hiyo ipo kwa ajili yao, wengine wataendelea kuwa escorts tu.
 
CR7 kabaniwa...
Vikombe kashinda n juve na timu ya taifa kaisaidia kutwaa kombe.
 
Takwimu za Messi zimeletwa hapa za msimu mzima, kipi kinawashinda kuleta takwimu za Virgil hapa ili tuone?

Yaani mtu anaesubiri kupiga vichwa na tackling eti apewe uchezaji bora wa Dunia? Acheni mambo yenu bwana.

Hivi unajua kuwa beki wa kati toka dakika ya kwanza hadi mpira unaishi anaweza asikimbie hata kilometre 3? Na wakati viungo wakabaji na washambuliaji wanakimbia zaidi ya kilometre 7 uwanjani?

Mabeki na makipa watengenezewe tuzo zao, hawastahili kushindanishwa na viungo pamoja na washambuliaji hata siku moja, kazi wanayofanya ni ndogo sana compared na viungo na washambuliaji.

Ni upumbav* wa kiwango cha SGR kumlinganisha VVD na hata SADIO MANE kwa takwimu za uwanjani na hata PFL kabeba kwa bahati tu, ile tuzo alitakiwa apewe Raheem Stearling na sio VVD, kuna muda matatizo ya nje ya uwanja yanamuhukumu Raheem.

Afu kumbukeni kuwa Mohamed Salah alibeba PFL na kumwacha De Bruyne ambae alikuwa anapigiwa upatu wa kuwa mchezaji bora so hata hii FIFA wako fair kabisa na La Pulga alistahili
Mkuu, mimi kazi yangu kukupa LIKE tu.
 
Naungana na wewe kabisa na hata post yangu kabla ya hii nimekubali kabisa kuwa last season Mohamed Salah alistahili kupewa ile tuzo na sijui walitumia kigezo gani kumpa Modric, wapiga kura ndio wanajua hilo.

Tukija kwenye perfomance ya mchezaji kwa mtazamo wangu ni kwamba pamoja na mchezaji kutobeba makombe doesnt mean hakuperfom vizuri, kuna muda wachezaji wanakuwa kwenye ubora sana ila timu wanazochezea zinakuwa kwenye viwango vibovu ndio maana nikasema PFL msimu uliopita waliopiga kura walifanya sahihi kabisa, pamoja na liverpool kutobeba uefa ila Virgil alikuwa bora ndio maana akapewa ile tuzo na hata msimu ule mwingine pamoja na De Bruyne kuwa kwenye ubora ila ubora wake haukumfikia Mohamed Salah na ndio maana alipewa tuzo ya uchezaji bora wa EPL
Umevuruga hapo kwenye team peromance haipo bali ni ndividual.....
 
Mpira mchezo wa takwimu mzee baba, Je modric ni kiungo mkabaji au mshambuliaji?
Kama ni kiungo mshambuliaji, Je alikuwa na assist ngapi kwenye UCL, La liga na World Cup last season?
Kama ni kiungo mkabaji, Je alipokonya mipira mara ngapi kwenye hizo competition zote?
Je alipiga accurate pass ngapi? Unaposema alikuwa anatawala dimba la kati uwe na takwimu pia, kama huna takwimu utakuwa mbabaishaji, Kwa Worldcup kwangu Pogba alicheza vizuri sana than Modric na bila kupepesa macho kabisa nakiri kwa kusema Kylian Mbappe ndio alikuwa mchezaji bora wa mashindano.
Pogba mtoe kwa waliokiwasha WC iliyopita.
Modric
Mbappe
Hazard
Hawa wajomba saluti sana kwao aisee..!!
 
Mane anacheza namba ngapi na salah anacheza Namba ngapi ???
Ngoja kidogo niweke sawa. ikiwa majina ya Mane na Salah wamekuwa voted juu ya wote kasoro wale watatu bora basi kwa nafasi zao ni lazima wawepo top 11. Mane na Salah ni kama wingers kushoto na kulia sasa iweje mbappe ambaye hakupata vote kabisa awe top 11. Hazard alikuwa number 9 katika list lakini kapachikwa kama kiungo wa kati ili Adidas wafurahi. huwezi kuwa shule high score number 4 halafu akaja mwingine number 12 shuleni akachaguliwa kimkoa wewe 4 usiwepo.
 
Wengi mnachanganya sana mambo, tuzo ya UEFA inaangalia mashindano ya UEFA tu, lakini tuzo za FIFA zinaangalia individual performance tokea msimu unavyoanza kuanzia July 2018 hadi June 2019.
Sasa angalia stastics za messi individually na VVD.
Individual performance Messi aliwazidi wote ila ka ni team performance VVD alimzidi Messi.
Hapo hawaangalii umechukua makombe mangapi, inaangaliwa wewe individually umefanya nini.
Nimesoma katika site zao kwa kuangalia criteria zote zinafanana tofauti ni 2 tu kubwa. UEFA wanaocheza ndani ya Europe iwe club au team ya taifa uzuri wa UEFA kura zinapigwa na waandishi wa habari na makocha team zilizoshiriki UEFA champions league. Sasa FIFA wanasema wachezaji wanaocheza kokote tatizo la FIFA kura zinapigwa na makocha na captain wa team zote za Taifa sio club. Hapa ndio inakuja shida kwa mfano ni rahisi mtu kama captain wa team ya Tanzania kupiga kura kwa mapenzi na huu ni mfano tu ila UEFA wanaopiga kura niwale wanaoshiriki katika mechi za champions league makocha na waandishi wa habari kwa hapa nawapa uzito UEFA. tatizo la FIFA hawana mashindano mengi kuwapa makocha na captain wa taifa kupiga kura sio sawa labda baada ya mashindano ya world cup maana wanakuwa washiriki ndio maana siku zote nominees wanakuwa walewale tatizo nani anapiga kura? UEFA washiriki na FIFA sio washiriki kwa maana makocha na captains. unategemea nini kocha na captain wa South Sudan atachaguwa.....
 
ubora au kiwango bora cha mchezaji unakipima kwa njia gani?
haiwezekani mlinzi wa kati (van virgil) na kiungo mshambuliaji (bernardo silva) wafanane kiuwezo.

kwa hoja zako wewe ina maana zidane, luis figo, cannavaro laiti kama wangelicheza soka nyakati hizi basi wasingelistahili kushinda tunzo za mchezaji bora wa dunia kwa sababu hawafikii ubora walionao messi na ronaldo hususani kwenye ufungaji wa magoli.

unasema hujui alichokifanya wesley sneijder mwaka 2010, brother mbona unaleta utani wa makusudi.
Kwa kutazama kwako stats za Ronaldo na Messi zinalingana na hao uliowataja hapo juu?
 
kama itatokezea messi amefunga magoli 100 na assist 50 bila ya kushinda kombe hata moja kwa hoja yako wewe anapaswa kupewa tuzo ya mchezaji bora wa dunia.

kwa hoja yako kama itatokezea liverpool wamecheza msimu mzima bila ya kuruhusu kufungwa mechi hata moja huku wakibeba ubingwa bado van virgil hatostahili kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa sababu amezidiwa na messi kitakwimu za magoli.

nilikuwa sijakuelewa brother.
Taraaatibu umeanza kuelewa, YES atastahili Messi.

Kwasababu ameonesha uwezo wake binafsi haswa, kama pia akatokea Mane au Salah ktk hayo mataji waliyoshinda, juhudi kubwa zaidi imetokea kwake, mfano labda uweze binafsi wa Mane ni 80% au Contribution ya Salah ni 80% ya kuchukua hizo tuzo basi atastahili badala ya Messi.

Mchango wa Liverpool kuchukua ubingwa ulijawa na watu wengi pale Liver na sio uwezo wa huyo jamaa.

Hivi ndivyo nilivyowaelewa wadau walivyozungumza humu ndani.
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya individual perfomance na team perfomance, ubora wa VVD ni matokeo ya team perfomance bt ubora wa Messi ni matokeo ya individual perfomance, kama hujanielewa hapa basi huwezi kunielewa daima.

Yes, Zidane na Kaka wangecheza kipindi hiki wangekuwa na uwezekano mdogo sana wa kuchukua mchezaji bora wa Dunia, hiki kitu ambacho wanafanya Ronaldo na Messi nakiri hakijawahi kushuhudiwa toka Dunia iumbwe (achana na enzi za mpira ambao offside hazikuwepo) nazungumzia toka zianze zama za modern football
Mtu kapeleka UEFA 3 Bernabeu, tena kwa misimu kufuatana, sio mtu wa kawaida huyu.

Hao wote aliowataja si wacheza Bernabeu, kuna mtu anayefika rekodi ya Ronaldo hapo? Mbona kuna mambo tunazungumza utafkiri hatuyajui?

Messi na Ronaldo wapo level nyingine, walau tuseme Maradnona angeweza kuchuana nao.
 
nilichogundua brother unamchukia sana van virgil,
akifanya vizuri messi na ronaldo ni individual perforamance ila anachokifanya van virgil na wachezaji wengineo nje ya messi na ronaldo ni team performance.
Mimi nilifikiria pia hii tuzo alipaswa kuibeba virgil ila baada ya kumsoma huyo jamaa hii tuzo anapaswa kuipokea mtu aliyefanya nini basi naunga mkono hoja yake kuwa ni kweli kwa msimu ulopita Messi alistahili.

Nilikuwa nafatilia huu uzi post kwa post, ukishaelewa tu juhudi za mtu binafsi na juhudi ya timu ktk kuleta mafanikio basi utaweza kumwelewa jamaa kiundani.
 
Mkuu messi ni playmaker wa team.
Anachezesha team anapandisha na kushusha mipira.
Yeye ndiye anayeifanya team icheze.
Kazi aliyo nayo messi ni nzito kaka acha maskhara.
Na messi ndiye mkandarasi wa barca km unavyomzungumzia modric mkandarasi wa realmadrid .
VVD mchango atakaouonesha hautafananisha na mchango ambao messi atauonesha.
Kwasababu VVD hakabi peke yake ana backline inamaana akizingua wengine watakaba.
Ila messi yeye ndiye playmaker akizingua yeye team nzima imezingua.
Nadhan ushapata utofauti hapo.
Ndio maana messi anastahili zaidi.
Hivyo hivyo Mkuu, wataelewa tuu.
 
Back
Top Bottom