The Citizen ndilo Gazeti linalostahili kuungwa mkono na pongezi toka kwa wananchi

The Citizen ndilo Gazeti linalostahili kuungwa mkono na pongezi toka kwa wananchi

Citizen na Mwananchi ni magazeti yanayomilikiwa na Agakhan yenye makao yake Kenya.Kipindi hiki tumeshuhudia vyombo vya habari vya Kenya vikiwa mbele kuhusu mgombea wa uraisi Bwana Lissu vikimpamba na kumpa Airtime.
Hamtaki aandikwe wa kupambwa hata kidogo ?!. Wivu wa kike huo
 
Katika mchakato huu wa uchaguzi, vyombo vya habari, hasa magazeti yamekua yakikemewa kwa kuonesha upendeleo kwa CCM, na ni ukweli. Pamoja na mazingira hatarishi ya kufanya kazi zao, baadhi ya vyombo hivi vimejitahidi kutoa habari zinazotoa uwanja sawa kwa vyama vyote na kuripoti matukio nyeti yanayozua mjadala mtandaoni.

Chombo cha kwanza kinachostahili pongezi ni Gazeti la The Citizen - na nitatoa mifano.

Katika nakala yake ya tarehe 13/08/2020, ndio gazeti pekee lililoripoti habari ya njama za Tume ya Uchaguzi kuwa na mpango wa kuengua wagombea wa upinzani, na hii habari ilikua katika kurasa zake za mbele. Isome hapa.

Pia hili gazeti na kidogo, Mwananchi ndio magazeti pekee yalithubutu kuweka habari za Lissu kwenye kurasa zake za mbele. Mfano ni nakala ya tarehe 11/08/2020, ambalo waliripoti habari ya Lissu kutolipa kisasi. Soma hapa. Pia, the Citizen ndio gazeti pekee lililoripoti ujio wa Lissu nchini, Lissu kuteuliwa na Chama chake na Lissu kwenda kuchukua fomu Dodoma na kuziweka habari zote front page.

Kama mtakumbuka, ni gazeti pekee lililorepoti Habari ya Msajili wa vyama vya siasa kutanga kukifungia ACT Wazalendo

Ukiondoa Habari za siasa, gazeti la The Citizen pia, ndio gazeti pekee lililoripoti habari ya TCRA kuweka kanuni mpya, na kwenye hiyo Makala ikaweka mawazo mengi tu ya wakosoaji wa serikali. Pia ni gazeti lililorepoti Habari ya TCRA kuvitaka vyombo vya kimataifa kuomba leseni ili kufanya kazi na vyombo vya ndani ya nchi. Pia iliripoti habari ya Tume ya Uchaguzi kuengua mashirika kuu yasiyo ya kiserikali (NGOs) katika mchakato wa kusimamia uchaguzi.


Na Habari zengine nyingi sana. Mwananchi pia imejitahidi, ila nahisi The Citizen, limekua more objective, nahisi labda ni kwa sababu la kiingereza ndio maana watawala hawahangaiki nalo. The Guardian, limekua gazeti la hovyo kusema ukweli. Hata Habari zao hazina depth, sijui ni aina ya waandishi wao. Yaani inasikitisha, The Guardian ya enzi zile za Mengi wakati wa JK, ndio lilikua moto kweli, sa hizi limekua too shallow.

Leo pia kama mmegundua magazeti binafsi takribani yote yameripoti Habari ya kanisa la TAG kutaka uchaguzi wa huru na haki. Hili ni la kupongezwa pia, nilitegemea kama kawaida yao wangemuweka JPM kama cover story. Ni ujumbe mzuri mnatuma kwa wananchi nawapongeza na kuwapa moyo muendelee kuwa hivyo. Tuwape support tununue magazeti yao, kama tunavyowakosoa wakionyesha upendeleo.
Walishindws kulielewa tu sasa umefanya kosa kuwashtua.
 
Naunga mkono hoja.

Kiukweli, media za Tanzania, na waandishi wa Tanzania kwa sasa tunapitia kipindi kigumu sana cha trying moments, hata hao Citizen na Mwananchi, wao wanaweza kuonyesha hii objectivity wanayoonyesha kwasababu MCL ni kampuni tanzu tuu ya The Nation Media Group, hivyo hawategemei survival kutoka serikali yetu, hivyo angalau ndio the only independent main stream media in Tanzania.

Uhuru wa Habari Tanzania: Je, Vyombo Viko Huru? Je, Waandishi wa Habari wako huru? Wanathaminiwa?.

Media kuikosoa Serikali: Je, Tanzania tuna Strong Media au Strong Journalists wenye Uwezo huo?

Uchumi wa Magufuli: Sekta Binafsi ina-Suffer. Yalianza Maduka, Yakafuata Mashirika, Sasa ni Zamu ya Media Ina-suffer!

Je, Tanzania tuna Media Freedom kubwa kuliko UK na US? Tushuhudie kitachompata Julian Assange wa WikiLeaks! Tujifunze kwake
P
Huyu ndiye Pasco wa zamani, black aliita black... Ila huyu Pasco wa sasa mmmmh...
 
Huyu ndiye Pasco wa zamani, black aliita black... Ila huyu Pasco wa sasa mmmmh...
Human beings are not static, they are dynamic, and hence, they change with time, Pasco wa sasa ni Pasco Kada!.
P
 
Katika mchakato huu wa uchaguzi, vyombo vya habari, hasa magazeti yamekua yakikemewa kwa kuonesha upendeleo kwa CCM, na ni ukweli. Pamoja na mazingira hatarishi ya kufanya kazi zao, baadhi ya vyombo hivi vimejitahidi kutoa habari zinazotoa uwanja sawa kwa vyama vyote na kuripoti matukio nyeti yanayozua mjadala mtandaoni.

Chombo cha kwanza kinachostahili pongezi ni Gazeti la The Citizen - na nitatoa mifano.

Katika nakala yake ya tarehe 13/08/2020, ndio gazeti pekee lililoripoti habari ya njama za Tume ya Uchaguzi kuwa na mpango wa kuengua wagombea wa upinzani, na hii habari ilikua katika kurasa zake za mbele. Isome hapa.

Pia hili gazeti na kidogo, Mwananchi ndio magazeti pekee yalithubutu kuweka habari za Lissu kwenye kurasa zake za mbele. Mfano ni nakala ya tarehe 11/08/2020, ambalo waliripoti habari ya Lissu kutolipa kisasi. Soma hapa. Pia, the Citizen ndio gazeti pekee lililoripoti ujio wa Lissu nchini, Lissu kuteuliwa na Chama chake na Lissu kwenda kuchukua fomu Dodoma na kuziweka habari zote front page.

Kama mtakumbuka, ni gazeti pekee lililorepoti Habari ya Msajili wa vyama vya siasa kutanga kukifungia ACT Wazalendo

Ukiondoa Habari za siasa, gazeti la The Citizen pia, ndio gazeti pekee lililoripoti habari ya TCRA kuweka kanuni mpya, na kwenye hiyo Makala ikaweka mawazo mengi tu ya wakosoaji wa serikali. Pia ni gazeti lililorepoti Habari ya TCRA kuvitaka vyombo vya kimataifa kuomba leseni ili kufanya kazi na vyombo vya ndani ya nchi. Pia iliripoti habari ya Tume ya Uchaguzi kuengua mashirika kuu yasiyo ya kiserikali (NGOs) katika mchakato wa kusimamia uchaguzi.


Na Habari zengine nyingi sana. Mwananchi pia imejitahidi, ila nahisi The Citizen, limekua more objective, nahisi labda ni kwa sababu la kiingereza ndio maana watawala hawahangaiki nalo. The Guardian, limekua gazeti la hovyo kusema ukweli. Hata Habari zao hazina depth, sijui ni aina ya waandishi wao. Yaani inasikitisha, The Guardian ya enzi zile za Mengi wakati wa JK, ndio lilikua moto kweli, sa hizi limekua too shallow.

Leo pia kama mmegundua magazeti binafsi takribani yote yameripoti Habari ya kanisa la TAG kutaka uchaguzi wa huru na haki. Hili ni la kupongezwa pia, nilitegemea kama kawaida yao wangemuweka JPM kama cover story. Ni ujumbe mzuri mnatuma kwa wananchi nawapongeza na kuwapa moyo muendelee kuwa hivyo. Tuwape support tununue magazeti yao, kama tunavyowakosoa wakionyesha upendeleo.
Haya ni magazeti ya Kenya, yaliletwa na Mkapa enzi hizo. Kwao hayawezi kuandika habari za uchonganishi zisizokuwa na mizania. Wakenya siku zote huwa hawatutakii mema. Wangefurahi sana kama na sisi tungaliyapata kama wanayoyapata kwenye chaguzi za huko kwao.

Kuna haja baadaye sheria zetu zikarekebishwa kutoruhusu magazeti yanayomilikiwa na makampuni ya nchi za nje ku operate nchini kwetu. Au na sisi turuhusiwe kuanzisha magazeti yetu nchini Kenya.
 
Haya ni magazeti ya Kenya, yaliletwa na Mkapa enzi hizo. Kwao hayawezi kuandika habari za uchonganishi zisizokuwa na mizania. Wakenya siku zote huwa hawatutakii mema. Wangefurahi sana kama na sisi tungaliyapata kama wanayoyapata kwenye chaguzi za huko kwao.

Kuna haja baadaye sheria zetu zikarekebishwa kutoruhusu magazeti yanayomilikiwa na makampuni ya nchi za nje ku operate nchini kwetu. Au na sisi turuhusiwe kuanzisha magazeti yetu nchini Kenya.
Seriously?? Kwamba unataka sasa magazeti yote yawe yanasifu tu kama mengine??
 
Seriously?? Kwamba unataka sasa magazeti yote yawe yanasifu tu kama mengine??
Nimesema hatutaki magazeti ya nchi nyingine kuchapishwa nchini kwetu. Mbona sisi nchi hizo hazituruhusu kufanya hivyo kwao?
 
Nimesema hatutaki magazeti ya nchi nyingine kuchapishwa nchini kwetu. Mbona sisi nchi hizo hazituruhusu kufanya hivyo kwao?
Clearly, hujui sheria za nchi yako. Mswada wa vyombo vya habari uliopitishwa 2016 umedhibiti umiliki wa vyombo vya habari kutoka nje nchini. Kabla ya huo mswada, National Media Group ndio ilikua inamiliki Mwananchi kwa asilimia kubwa, ila kwa sasa chombo kinamilikiwa na Mtanzania. National Media ina stale 49%. Sasa unavyosema hivo you don't make sense.

Pili, kabla hujaleta hoja ni vizuri ufanye utafiti, la sivyo unaishia kupotosha. Aliekuambia sheria za Kenya haziruhusu uwekezaji wa vyombo vya habari kutoka nchi ngeni ni nani? Hata Uganda, pamoja na udictaror wao wanaruhusu ni kuwa tu soko la media Kenya lipo very competitive, na hamna mwekezaji aliejitokeza kufanya biashara hiyo, ila hawajakatazwa. Acha kupotosha!!!
 
Back
Top Bottom