The earth is flat and is not rotating

Newton's first law of motion inasema "an object at rest stays at rest and an object in motion stays in motion with the same speed and in the same direction unless acted upon by unbalanced force" hii kitu inajibu swal la kwanza vizur sana
 

mkuu kuna article moja nlishawai kuisoma inasema the earth isn't perfect sphere instead it's hollow at it's center na huko center ya dunia kuna intelligent and civilized race ya viumbe waitwao AGHARTHA (giant fellas human like structure), inadaiwa kuwa katika POLE mbili za dunia(north and south pole kuna gates za kuingilià huko na ndio maana NASA hawaruhusu ndege yeyote kupita katka poles za dunia kwa kuhofia siri zilizofichwa na mataifa ya wababe kufichuliwa, sasa hapa leo tena zinakuja hizi habari za the earth is flat sijui round
daaah dunia ina mambo ya uongo sana itafika siku tutaambiwa dunia ni imaginary place of Almighty so we are not real objects, we are nothing, we are just thought Almighty
(i'm sorry if this's gigantic post to my fella believers)

.made in mby city.
 
Kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa dunia ipo kama Chapati!???
 
1. Dunia huzunguka jua hilo halikwepeki, Kisayansi, Kilojikia na hata kimaarifa ya jamii. Kuhusu mfano wako wa Ndege. Umeshawahi kuona nzi au mdudu yeyote arukaye akiwa ndani ya gari/basi linalotembea!?? Huwa anaruka as if basi limesimama, hii inamaana kwamba yule mdudu akiwa ndani ya basi anakuwa yupo ndani ya space ya basi, hivo basi linatembea na ile space yake na vyote vilivyomo. Ndivyo ilivyo kwa Dunia na ndege.

2. Kuhusu Dunia kuwa kama chapati, napingana pia nawewe. Mfano mdogo tu, hapo ulipo hebu Anglia horizon, zipo katika umbo gani!?? Straight or curved!??
 
hongera mleta mada umewafanya watu wakasome jografia upya, sisi watanzania hatuna utamadun wa kujisomea ushahid upo hata ukupitia baadh ya post.
 
Reactions: Nzi
Kiranga njoo umalize huu ubishi naamini unayajua haya mambo
 
Last edited by a moderator:
Nahisi umesahau kuwa earth sio perfect sphere, na pia dunia ikiwa inazunguka ina move pamoja na vitu vilivyo kwa atmosphere yake.
 
ninaposoma madai ya mtu kuwa DUNIA INAZUNGUKA JUA, basi wala sina haja ya kucomment katika uzi kama huo,, mtu kama huyo anahitajika kurudi darasa la tatu.
 
ninaposoma madai ya mtu kuwa DUNIA INAZUNGUKA JUA, basi wala sina haja ya kucomment katika uzi kama huo,, mtu kama huyo anahitajika kurudi darasa la tatu.

Usikubali elimu ya darasa iwe funguo ya kukufunga usifikiri kinyume na ulivyofundishwa.
ki.ukweli elimu ya darasani imefisha uwezo wa kufikiri wa watu wengi sana.
jitahidi kujifunza kutokana na mazingira huku ukirejea uliyofundishwa darasani mkuu na kupata hitimisho lililotokana na kufikiri kwako.
 

Hakuna jipya hapo, nadharia za dunia bapa zilikuwapo toka zama, lakini katika dunia ya leo ndugu yangu na maendeleo ya sayansi na teknolojia mpaka kiganjani kwako unaweza kupata satellite za dunia hii na hata sayari zingine, binadamu ameweza kunyambua mpaka formation ya jua lenyewe, vilivyomo na safari zake, bado watu wanaibua theories zilezile za enzi hizo na kujaribu kuzilinda kwa ngao zilezile za kijima, dunia ni bapa na jua linazunguka dunia?! inahitaji moyo mgumu sana kushadadia nadhari kama hizo katika miaka ya 2000!
 

bado nasisitiza sayansi,technologia au elimu nyingine yoyote isitumike kuwa switch kuondoa haki yako ya kibinadam ya kuhoji na kujiuliza maswala. dunia umbo lake hakuna anayetoa kwa usahihi ndiyo sababu kuna maelezo tofauti.
dunia kuzunguka bado kuna maswali ambayo wengone tunajiuliza ili tupate majibu.
mimi sayansi sio mbadala ya ubongo wangu. mtazamo wangu sayansi kwa kiwango kikubwa imefisha uwezo wa binadam kuitazama dunia katika mapama yake ya kimfumo kwa kumega mifumo yenye utendaji unaoingiliana kana kwamba kila mfumo unajitegemea
 

Unachosema ni sahihi kabisaa, sasa hebu tuweke siasa pembeni (somo tunaloliweza sana watanzania), baada ya kushirikisha ipasavyo akili yako, nini msimamo wako katika somo tajwa hapo juu?
 
Jaribu kufanya utafiti wa kina.Kisha naomba majibu ya maswali yafuatayo.
1.Unaelezeae picha za dunia ziizopigwa toka angani?
2.Sayari zote tukiziangalia kwa telescope zinaonekana za mviringo.Kwa nini dunia pekee iwe ndo tambarare?
3.Unaelezeje kuhusu kutofautiana kwa usiku na mchana katika sehemu mbali mbali duniani kwa kutumia dhana ya dunia tambarare?
4.Umeshawahi kukaa pwani ukaangalia jinsi meli inayoondoka inavypotea katika upeo wako wa macho?Haipoteagi ghafla.Kinaanzaga kiwiliwili alafu mwisho kabisa ndo kilele kinapotea.Unaelezeaje kuhusu hili?
5.Unaelezeaje kuhusu kivuri cha mviringo cha dunia wakati wa kupatwa kwa mwezi?

Falsafa ya dunia ni tambarare ni ya kizamani sana na imeshapitwa na wakati.
 

Mtu kama huyu muulize kwanza elimu yake ni ipi na katika mwaka uliopita wote kasoma vitabu vingapi na vipi.

Mtu anabisha dunia haiendi kwa sababu ya mwendo wa ndege wakati dunia inakwenda na atmosphere yote pamoja na ndege?

Haya ndiyo matatizo ya kuamini kila neno la biblia kama ukweli mtupu.
 

Unataka kuniambia Anga nalo linazunguka?
 
Unataka kuniambia Anga nalo linazunguka?

Anga linaenda na dunia kama vile ukiwa kwenye ndege inayokwenda kasi na kukubeba unavyoweza kukaa na kurusha shilingi halafu ukaidaka mkononi palepale. Hata kama ndege inaenda 1000 km/hr, ile shilingi haiendi kuanguka nyuma ya ndege, kwa sababu na yenyewe ina kinetic energy ya mwendo wa ndege.

Hivyo hivyo, anga linaenda na dunia, lina kinetic energy inayofanya anga la dunia liende na dunia, halafu gravity inafanya anga libaki lilipo.

Unapoangalia suala la dunia kuzunguka jua unatakiwa kuangalia dunia na anga lake, siyo dunia kwa kuanzia ardhi tu.
 

Upande mmoja nakubaliana na wewe hasa mfano , lakini nikifikiria nje ya ndege huu mfano ngumu sana , Ila itanibidi nisome zaid , shukran
 
Upande mmoja nakubaliana na wewe hasa mfano , lakini nikifikiria nje ya ndege huu mfano ngumu sana , Ila itanibidi nisome zaid , shukran

Kanuni za fizikia ndani ya ndege na nje ya ndege ni zile zile, hazibadiliki.
 
Mfano ukirusha hiyo shiling ukiwa nje ya ndege itadondoka hapo hapo?

Kaa kwenye kiti, rusha juu shilingi kwa sekunde tatu, uone kama itapeperuka kwa kasi ya mwendo wa dunia kulizunguka jua108,000 km/hr ( that's 30 km/second) na kutua km 90 kutoka ulipo au itatua umbali usiozidi mita chache kutoka ulipo.

Ukirusha shilingi nje ya ndege kutoka kwenye ndege kwa sekunde chache shilingi ita accelerate na kinetic energy ikiyotoka nayo kwenye ndege, baada ya hapo itakuwa haipati tena kinetic energy kutoka kwenye ndege itaanguka kwa kufuata nguvu za uvutani wa dunia.

Physics ya form one.

Tatizo tunaongeza wanafunzi aekondari, lakini elimu inashuka.

Au labda elimu inapanda tunajibizana na watoto wa darasa la nne :s .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…