Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Safi sana vijana kazi nzuri kabisaDk 88 eve 1-3 cityView attachment 730738
Tunawaua manyumbu hawana uwezo wa kupambans na citizens,CTID.UMEUSOMA msimamo wa Ligi Kuu England? Umeiona Manchester City? Inatisha kinoma. Imecheza mechi 31, imeshinda 27, imetoka sare tatu na imepoteza mechi moja tu.
Kwa rekodi hizo, ni dhahiri Man City inaposhuka uwanjani, kitu kikubwa unachokitarajia ni ushindi. Na sasa imebakiza ushindi mmoja tu, kutangaza ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu.
Ndio Man City bado mechi moja tu. Kitu kizuri wakati inasubiri kushinda mchezo mmoja, mechi yake ijayo itacheza na mahasimu wao wakubwa, Manchester United huko Etihad.
Kipute hicho kitafanyika Aprili 7 na swali lililopo je, Man United inayonolewa na Jose Mourinho itakubali kufanywa ngazi na Man City ya Pep Guardiola na kutangaza ubingwa wa ligi hiyo?
Ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Everton umeifanya Man City kusubiri kushinda kwenye mechi moja tu ijayo kujibebea ubingwa huo, kwani hapo itakuwa imewekwa pengo la pointi kufikia 19, huku mechi zitakuwa zimebaki sita, ambazo hata ikifungwa zote na timu zinazoikimbiza ikishinda zote, itakuwa imeongeza pointi 18 tu, moja ya pungufu pengo lililopo.
Mchezo ujao wa Man City itacheza na Man United na hilo ndilo linalozidisha utamu wa mchezo huo mmoja unaosubiriwa na mastaa hao wa Guardiola ili kuubeba ubingwa. Man United iliichelewesha Man City kutangaza ubingwa mapema baada ya kuichapa Swansea City 2-0 huko Old Trafford juzi Jumamosi.
Nahodha wa Man City, Vincent Kompany amesema kubeba ubingwa wa Ligi Kuu England mbele ya Man United hiyo ina maana kubwa sana kwa mashabiki wake maana itakuwa kama vile imebeba ubingwa wa dunia. Man City itakuwa bingwa wa England kwa mara ya tatu katika kipindi cha miaka sita ya karibuni kama itabeba pointi zote tatu kwenye wikiendi ijayo.
Kompany alisema akili yao kwa sasa imeielekeza kwa Liverpool, ambayo itachuana nayo Jumatano usiku kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya na baada ya hapo itawaza namna ya kuichapa Man United ili kubeba taji lake la pili msimu huu baada ya taji la Kombe la Ligi.
Tumefanya vizuri hadi kufika hapa, lakini kwa sasa tunawaza mechi yetu ya Jumatano baada ya hapo tutadili na Man United Jumamosi. Sisi tunafanya mambo yetu mechi kwa mechi. Itakuwa kitu kikubwa sana kwa mashabiki wetu, nimeishi hapa Manchester kwa muda mrefu, hivyo nafahamu mambo yanavyokuwa.
Manchester United ina siku saba za kujiandaa, lakini sisi tunahitaji muda wowote ule na kwa sasa tunachohitaji ni kuwa fiti kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.”
Man City ni timu ya 10 kwenye historia ya Ligi Kuu England kufunga kila timu katika ligi kwa msimu husika tangu Man United ilipofanya hivyo kwa mara ya kwanza msimu wa 2010-11.
Chanzo:mwanaspoti
Wakuu wakuuu soon tunauwasha asee
poleni sana ...hii naifananisha na kwamba umeingia kambi ya jeshi halafu jamaa wako uwanjani halafu unajisaidia mbele yao kinachofuata .....Kila lakher kwetu, naona mfumo wa leo ni 3-6-1
Hahah!! Aisee asante sana mkuu huu moto wa hawa vijana sio kabisapoleni sana ...hii naifananisha na kwamba umeingia kambi ya jeshi halafu jamaa wako uwanjani halafu unajisaidia mbele yao kinachofuata .....