The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

Manchester City wanakaribia kukamilisha ununuzi wa pauni milioni 75 kwa ajili ya winga raia wa Algeria Riyad Mahrez, mwenye umri wa miaka 27, kutoka Leicester City. (Mail)

Manchester City wamekataliwa kumnunua mchezaji wa kiungo cha kati wa Napoli Jorginho kwa pauni milioni. Klabu hiyo ya Ligi kuu ya Italia (Serie A ) wanataka walipwe pauni milioni 52 kwa mtaliano huyo mwenye umri wa miaka 26, na wanakabiliwa na ushindani kutoka upande wa Chelsea. (Mirror)

Manchester City wako tayari kukamilisha mkataba na Paris St-Germain kwa ajili ya mshambuliaji wa timu ya Monaco mwenye umri wa miaka 19 Kylian Mbappe.

Mfaransa huyo alikuwa katika timu ya PSG kwa mkopo msimu uliopita lakini mabingwa hao wa Ufaransa huenda wakalazimika kuvunja mpango wao wa kumsaini (Manchester Evening News)

Mlinda lango wa Manchester Joe Hart, mwenye umri wa miaka 31, amebadilisha mawakala wake baada ya kutupwa nje ya kikosi kitakachoiwakilisha England katika michuano ya Kombe la Dunia. (Mail)
 
Riyad Mahrez ni supersigning ya msimu huu kwa upande wa Etihad . Mahrez tunamunderrate sana na wachezaji kama Sane na Sterling wajiandae kucompete kwenye first eleven. Riyad anafungia kutoka mbali, na anafunga sana kwa kupiga mashuti baada ya dribles tofauti na wachezaji wengi ambao hufunga kwa kutumia open chances kama za one on one situation with a goal keeper. Vilabu vikubwa vijiandae tu na huo moto wake!
 
Mechi za kirafiki
Mabingwa watetezi wa ligi ya Uingereza Manchester City wataelekea nchini Marekani kwa ziara ya ambayo itashirikisha mechi za kirafiki dhidi ya wapinzani wao wa Uingereza Chelsea na Liverpool.
Klabu hizo tatu zitaungana na klabu za Manchester United, Arsenal na Tottenham katika mchunao huo wa mabingwa wa kombe la kimataifa
Shindano hilo la kila mwaka pia litashirikisha mabingwa wa Uhispania, Itali, Ufaransa na Ujerumani -Barcelona, Juventus, PSG na Bayern Munich - pamoja na Benfica na Atletico Madrid.

Liverpool itakabiliana na klabu zote mbili za Manchester katika kipindi cha siku tatu, huku Chelsea ikichuana na wapinzani wao wa London Arsenal katika mji wa Dublin Agosti mosi.
Mabingwa watetezi wa kombe la FA Chelsea watakabiliana na Manchester City katika kombe la Community Shield katika uwanja wa Wembley mnamo tarehe 5 Agosti.
Wiki mbili kabla ya mechi hiyo Chelsea itasafiri maili 17,982- magharibi mwa Australia ili kuchuana na Perth Glory.


Mechi za kirafiki kabla ya msimu wa ligi ya Premier kuanza:

Arsenal

14 Julai: Boreham Wood 0-8 Arsenal (Meadow Park)

26 Julai: Arsenal v Atletico Madrid (Singapore Sports Hub)

28 Julai: Arsenal v Paris St-Germain (Singapore Sports Hub)

1 Agosti: Arsenal v Chelsea (Aviva Stadium, Dublin)

4 Agosti: Arsenal v Sevilla (Friends Arena, Stockholm)
 
 
walijipatia kibondewao wakupiga 8
 
manchester city vs livarpool saa 6 usiku lazima tulipize kisasi kwa liverpool


Baada Ya Kusubiri Ulipize Kwenye Champion League wewe unataka Ulipize Kwenye Preseason?

Kwenye CL ulifungwa na Wachezaji 14 (11 + 3 subs)... Sasa Kwenye Hii Mechi Ya Preseason Wewe subiri Ukawafunge Wachezaji 22 (11 First Half + 11 Second Half) wengi wao Ni Vijana Wa Academy wanaotayarishwa Kutolewa Kwa Mkopo.
 
subili tuone tusipowafunga leo epl itaanza tu
 
Munaweza Mukatufunga Hata Goli 6... Hoja yangu Ni Kwanini Musitusubiri Champion League ili mulipize Kisasi badala Yake Munataka Kulipiza Kisasi Kwa Mechi za Tour?
Munaweza Mukatufunga Hata Goli 6... Hoja yangu Ni Kwanini Musitusubiri Champion League ili mulipize Kisasi badala Yake Munataka Kulipiza Kisasi Kwa Mechi za Tour?
Munaweza Mukatufunga Hata Goli 6... Hoja yangu Ni Kwanini Musitusubiri Champion League ili mulipize Kisasi badala Yake Munataka Kulipiza Kisasi Kwa Mechi za Tour?
subili epl ndipo tutawapa dozi maana champions league atutakutana mlichezea bahati amtafika mbali
 
subili epl ndipo tutawapa dozi maana champions league atutakutana mlichezea bahati amtafika mbali

Bahati Wakati CL tulikupiga Nje Ndani? Kuna Bahati gani Ya Kukupiga Mara 2 nje ndani?
Na Kwenye EPL nilikupiga! Kwahiyo Nimekupiga Vipigo 3 mfululizo badala Yake unaita Bahati?
Halafu kipigo cha Leo sikihesabu Kuwa tumekufunga Kwani ilikuwa tunapigisha Watoto jaramba tu!

Hivi Nikuulize, Liverpool Kumfunga Man City Ni Jambo la ajabu????
 
wale ni madogo subilini epl tuwaoneshe kazi
 
Arsenal itaanza ligi wikiendi hii kwa kuwakaribisha Manchester City nyumbanbi kwao, Emirates. Ikumbukwe kuwa Arsena wameshindwa kuwafunga Manchester City katika michezo 5 ya hivi karibuni kwa kufungwa michezo 3 na kutoa sare 2. Kwa hiyo, Arsenal itakuwa na mlima mrefu wa kupanda ikiwa chini ya kocha wake mpya, Unai Emery.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…