The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

UEFA have announced all Champions League and Europa League games next week have been postponed due to ongoing coronavirus pandemic.


The postponement also applies to UEFA Youth League, with further decisions on when these matches take place "to be communicated in due course".

As a consequence of the postponements, the UCL and UEL quarter-final draws scheduled for 20 March have also been postponed.
 
UEFA have announced all Champions League and Europa League games next week have been postponed due to ongoing coronavirus pandemic.


The postponement also applies to UEFA Youth League, with further decisions on when these matches take place "to be communicated in due course".

As a consequence of the postponements, the UCL and UEL quarter-final draws scheduled for 20 March have also been postponed.
Dah
 
MAAMUZI MAGUMU!
HATMA YA UBINGWA WA LIVERPOOL KUPITIA MBINU HIZI.

LICHA ya kusimamisha Ligi Kuu England kwa wiki tatu hadi Aprili 3 mwaka huu, vichwa vinawauma mabosi wa bodi ya EPL, kutokana na kutakiwa kuja na majibu ya nini kitafanyika iwapo virusi vya Corona vitaendelea kuitesa nchi hiyo.
Hadi sasa hakuna jibu la moja kwa moja linalotolewa na mabosi hao ambao wanatarajiwa kufanya kikao cha dharura wiki hii, kuhusiana na nini kitafanyika ikiwa tatizo la Corona litadumu kwa muda mrefu maana Ligi Kuu England haina kanuni inayoeleza hatua gani zitachukuliwa iwapo ligi itavunjika.

Lakini, wachambuzi wa soka la England wamekuja na aina nne za uamuzi mgumu ambazo vigogo hao wanaweza kuchagua moja.

UAMUZI WA KWANZA:
Kuvunja Ligi
Huu ni uamuzi unaowakera zaidi mashabiki wa Liverpool waliokuwa wanaamini huu ni mwaka wao na baada ya mechi 29 msimu huu wanaongoza ligi kwa tofauti ya pointi 25 mbele ya Manchester City inayoshika nafasi ya pili na wanahitaji mechi mbili tu kutwaa ubingwa wao wa kwanza baada ya miaka 30.
Lakini, kwa mujibu wa uamuzi huu uliowekwa mezani na Makamu Mwenyekiti wa West Ham, Karren Brady, kwa upande wake anashauri ligi ivunjwe na kila kitu kianze upya kuwe hakuna bingwa wala timu ya kushuka daraja, hii ni nzuri kwa timu yake inayoshika nafasi ya 16 ikiwa na pointi 27 na wastani mzuri wa mabao kulinganisha na timu zilizo chini ya mstari wa kushuka daraja.
Uamuzi huu unaiathiri zaidi Liverpool inayokaribia kutwaa taji la Ligi Kuu kwa mara ya kwanza baada ya miaka 30, lakini pia uamuzi huu utaiathiri Leicester City ambayo ipo kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

UAMUZI WA PILI:
Kumalizia MECHI
Huu ndiyo uamuzi ambao mabosi wa EPL, wanaona hauna utata kila timu na itapata inachostahili, kupitia uamuzi huu wanataka kusubiri na kumaliza ligi kivyovyote na hata kama tatizo la virusi vya Corona litachukua muda mrefu kiasi gani, lakini vikiisha tu ligi imaliziwe ndipo msimu mpya uanze.
Lakini, ili hili litokee lazima michuano ya Euro 2020 isifanyike ili kutoa nafasi kwa klabu kucheza mechi za ligi wakati wa kiangazi, maana kama michuano hiyo ikiwapo wachezaji watajiunga na timu zao za taifa na hawatapata nafasi ya kucheza soka katika ngazi ya klabu.

UAMUZI WA TATU:
Ligi kuisha hapa
Kama tatizo la Corona lisipomalizwa mapema basi mashabiki wengi wa Liverpool wanataka uamuzi huu ambao ni kumaliza ligi katika hatua hii na kuwapa ubingwa huku. Norwich City, Aston Villa and Bournemouth zikishushwa daraja.
Uamuzi huu unainufaisha zaidi Liverpool ambayo itapata ubingwa ambao inastahili, lakini unaziumiza timu nyingi, kuanzia zile zitakazoshushwa daraja wakati zikiwa na nafasi bado ya kupamba na kubaki Ligi Kuu hasa kutoka na ukweli kuwa tofauti kati ya timu ya 18 na ya 17 na 16 ni mabao tu.
Lakini pia timu ambazo zinapambana kutafuta nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya, Manchester United, Wolves na Sheffield United zitaathiriwa na uamuzi huu kwa sababu bado zina nafasi ya kuingia nne bora kama ligi ikiendelea, lakini ikimalizwa hapa basi hawatashiriki michuano hiyo mwakani.

UAMUZI WA NNE:
Kuongeza idadi ya timu
Ili kuepusha kelele ya timu zitakazoshuka daraja na pia kuiwezesha Liverpool kutwaa ubingwa ambao imeupigania sana msimu huu, basi Bodi ya Ligi inaweza kuamua hakuna kushusha timu daraja na kuipa ubingwa Liverpool.
Na ili kuzipa haki zile timu ambazo zimekuwa na msimu bora Ligi Daraja la Kwanza, timu za Leeds na West Brom zipewe nafasi ya kupanda daraja, hii itamaanisha kuwa msimu ujao utakuwa na timu 22 badala ya 20, huku kila timu ikifurahi, japokuwa zile za timu zinazowania nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa zitalia lia tu.

Ndugu mwanamichezo nini maoni yako?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
LONDON ,ENGLAND.
MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Tammy Abraham amepewa jezi namba 9 ya klabu hiyo akiirithi kutoka kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina, Gonzalo Higuain.
Kwa sasa jezi hiyo inasemekana ni kama vile ina mikosi. Washambuliaji wengi wanaovaa jezi hiyo pale Chelsea katika miaka ya karibuni wamefeli. Alvaro Morata, Fernando Torres, Radamel Falcao, ni miongoni mwa mastaa ambao wamefeli katika jezi hiyo.
Kuna laana au mikosi mingi ambayo imekuwa ikihusishwa na soka.

1.AARON RAMSEY NA VIFO VYA VIGOGO.
Kiungo wa zamani wa Arsenal ambaye katika dirisha hili ametua katika Klabu ya Juventus kwa uhamisho wa bure. Ramsey alijulikana na mkosi wake wa kufunga mabao ambayo yaliambatana na vifo vya watu wengi maarufu. Mwanamuziki maarufu wa kike duniani, Whitney Houston alifariki mwaka 2012 saa chache baada ya Ramsey kuisaidia Arsenal kuichapa Southampton. Lakini pia Mwigizaji maarufu, Alan Rickman alifariki siku moja baada ya staa huyu wa Wales kuiwezesha Arsenal kuichapa Liverpool. Miongoni mwa watu wengine maarufu ambao walifariki baada ya Ramsey kufunga mabao yake ni pamoja na Steve Jobs, Osama Bin Laden, Muammar Gaddafi, Rubin Carter, Paul Walker, Robin Williams na David Bowie.

2.JEZI NAMBA 9 YA CHELSEA

Abraham aliyekulia katika kikosi cha vijana cha Chelsea ana kazi ngumu ya kuondoa mkosi katika jezi namba 9 ya Chelsea. Sio jezi nzuri kuikimbilia ukizingatia washambuliaji mahiri wanakwenda pale na sifa lukuki lakini wanashindwa kuonyesha makali yao wakivaa jezi hii. Gonzalo Higuain licha ya makali yake lakini alifunga mabao matano tu na jezi hii kuanzia Januari mwaka huu.
Kabla ya hapo mastaa wakubwa kama Alvaro Morata, Fernando Torres, Radamel Falcao na Mateja Kezman wote walivaa jezi hii lakini bila ya mafanikio yoyote. Abraham amezungumzia kuhusu mkosi huo kwa majigambo makubwa huku akisema: “Nimesikia upuuzi kuhusu jezi namba 9. Niko hapa kucheza soka langu na kujaribu.

3.MKOSI WA KUPIGA PICHA NA DRAKE.
Mamilioni ya mashabiki wa muziki duniani kote wanatamani kupiga picha na rapa maarufu wa Canada, Drake.
Hata hivyo, kwa sasa watu wameanza kujifikiria mara mbili kupiga picha na Drake. Imeibuka tabia ambapo kila unapopiga picha na rapa huyu unaelekea kushindwa katika mchezo unaoshiriki. Mastaa wengi wa soka wamejikuta wakichemsha katika hili na mmojawapo ni kiungo wa Manchester United ambaye alipiga picha na Pogba saa chache kabla ya Manchester United haijachapwa na Wolves 2-1 Kombe la FA.
Staa wa Arsenal, Pierre Emerick-Aubameyang ni mhanga mwingine ambaye alipiga picha na Drake dakika chache kabla Arsenal haijachapwa na Everton. Bondia maarufu wa Uingereza, Anthony Joshua naye alifanya kosa hilo kwa kupiga picha na Drake na kudundwa na bondia kutoka Mexico, Andy Ruiz. Wakati akipiga picha hiyo Joshua alionekana kukejeli mkosi huo lakini alijuta baadaye.

4.MIZIMU YA WARUMI BIRMINGHAM.
Inadaiwa Uwanja wa Soka wa Klabu ya Birmingham City ulijengwa katika ardhi ya mizimu ya Kirumi. Inadaiwa Klabu ya Birmingham imekuwa na mikosi mingi. Msimu wake wa kwanza katika Ligi Kuu uliiona timu hiyo ikishuka daraja. Katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia jukwaa lao kubwa liliungua moto. Winga wa zamani wa Birmingham, Barry Fry alijaribu kuukomboa uwanja huo kutoka katika mikosi kwa kutumia fomula yake binafsi. “Tulimuita mtu mmoja aje kuondoa mikosi katika uwanja huo na akatuambia kuwa njia pekee ya kuondoka mikosi katika uwanja huo ilikuwa kukojoa kila pembe ya uwanja. Mimi sio mtu ninayeamini mambo hayo lakini baada ya miezi mitatu nilikuwa tayari kujaribu kitu chochote kile kwahiyo nilikwenda na kukojoa katika kona zote za vibendera. Ilinichukua muda. Haikuwa rahisi.”

5.PAKA ALIYEUAWA KLABUNI RACING.
Klabu ya Racing ya Argentina ilikuwa moja kati ya klabu zenye mafanikio katika Bara la Amerika Kusini miaka ya 1960. Lakini baada ya kutwaa ubingwa wa Mabara wa Amerika Kusini na Kombe la Intercontinental mwaka 1967 kila kitu kilibadilika. Inadaiwa hili lilitokana na kundi la mashabiki wa timu pinzani ya Independiente kuvunja geti na kuingia Uwanja wa Racing na kufukia paka saba waliouwawa.
Kwa muongo mmoja uliofuata miaka ya 1970 klabu hiyo haikuchukua taji lolote. Mbaya zaidi Racing ikashuka daraja mwaka 1983. Kwa hiyo ili kukomesha laana au mkosi huo, Racing iliamua kufukua na kuwaondoa paka hao marehemu lakini waliweza kuondoa mizoga sita tu.
Mwaka 1998 Racing ilitangazwa kufilisika na mwaka mmoja baadaye ilimuita mchungaji kwa ajili ya kufanya maombi. Iliichukua Racing mpaka mwaka2001 kurudi katika hali ya kawaida na mwaka 2002 ilichukua ubingwa wa Argentina kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1966.

6.JEZI NAMBA 7 KLABUNI MANCHESTER UNITED.
Sio tu Chelsea ambao wanaonekana kuwa katika mkosi na jezi namba 9. Pale Manchester United jezi namba 7 imeanza kuonekana kuwa tatizo baada ya kutamba kwa muda mrefu klabuni hapo.
Wakongwe kama Bryan Robson, David Beckham, Cristiano Ronaldo na George Best waliivaaa jezi hii kwa mafanikio. Lakini tangu Cristiano Ronaldo aondoke katika dirisha kubwa la majira ya joto mwaka 2009 jezi hiyo ni kama vile imeachiwa mkosi na laana.
Mastaa wengi waliovaa jezi hiyo wameishia kutukanwa na mashabiki. Wanakuja Old Trafford wakiwa mastaa wakubwa lakini wanachemsha vibaya klabuni hapo. Baadhi yao ni Michael Owen, Alexis Sanchez, Memphis Depay na Angel Di Maria. Wakati fulani staa wa kimataifa wa Ecuador, Antonio Valencia alikacha.

7.MZIMU WA BAYER LEVERKUSEN.
Katika miaka ya 1990 na miaka ya 2000, Klabu ya Bayer Leverkusen ilijulikana kama ‘WANAUME WANAOKARIBIA’ kutokana na tabia yao ya kukaribia makombe lakini wanaambulia patupu.
Wengine waliwatania kwa jina la the Neverkusen Men. Miaka ya 1997, 1999, 2000 na 2002, Bayer Leverkusen ilimaliza katika nafasi ya pili Bundesliga. Mwaka 2000 ilihitaji pointi moja tu kutwaa ubingwa wa Ujerumani lakini ikaambulia patupu.
Miaka miwili baadaye ilipoteza uongozi wa pointi tano ambazo zilikuwa zinawapeleka katika ubingwa lakini ikapoteza mechi mbili kati ya tatu za mwisho na hivyo kuiruhusu Borussia Dortmund kutwaa ubingwa. Huo ndio mwaka ambao staa wa kimataifa wa Ufaransa, Zinedine Zidane alifunga bao la ushindi nchini Scotland katika pambano la Ligi ya Mabingwa wa Ulaya. Ukiwa Leverkusen wenyewe wanaamini kwamba hii sio bahati mbaya ya kawaida. Wanaamini kuna laana ambayo inawatafuna.
Hawaijui.

8.MZIMU WA GUTTMANN NA BENFICA.
Hii ni moja kati ya laana maarufu katika soka. Kocha maarufu wa zamani wa Hungary, Bela Guttmann aliondoka Porto mwaka 1959 na kujiunga na wapinzani wao maarufu Benfica. Mara baada ya kujiunga na klabu hiyo ilitwaa mataji mawili mfululizo. Baada ya kutamba katika soka la ndani la Ureno, Guttmann pia alikomesha utawala wa Real Madrid kwa kutwaa ubingwa wa Ulaya. Mara baada ya mafanikio hayo aliomba klabu hiyo imuongezee mshahara kutokana na pato la klabu hiyo kukua lakini katika namna ya kushangaza klabu hiyo ilimwambia HAPANA.
Hapo ndipo Guttmann alipoweka laana kubwa kwa klabu hiyo ya Ureno huku akisema:
“Sio kwa ndani ya miaka hii mia, kuanzia sasa Benfica kamwe haitatwaa ubingwa wa Ulaya.”
Ni kweli. Ni nusu karne sasa Benfica bado inasubiri ubingwa wa Ulaya. Ilipoteza fainali za Ulaya miaka ya 1963, 1965 na 1968 baada ya Guttmann kuondoka klabuni.

Chanzo:Gazeti laMwanaspoti
 
City boys mlikuwa wapi kufanya vitu ka hivi kabla mechi hazijabaki chache mkononi saa hii tungelikuwa tunaongea mengine. Sasa pamoja na maushindi ya kishindo namna hii bado ni Kama tunaendesha baiskel ziwani kwa mbio za ubingwa huu.
 
Hivi mnajua kama Fabinho alicho fannya jana ilikuwa ni ukumbusho wa siku ileeee,

mmeikumbuka ee..

warning; msimweke bravo tena hyo siku ya siku
 
1st goal. De brune
1593117214153.gif
 
Back
Top Bottom