The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

Goli la KDB unaweza kuombea mkopo ....

Hata hivo Chelsea tumewazidi kila kitu ,yaani ilikuwa swala la muda tu kufunga goli ...

Nafasi ya grealish ilikuwa goli lile...

Mpaka 1HT Chelsea hawana shots on Target ,corner ,Wala chance created ...
.
Tumerudi kipindi cha pili na nguvu ile ile ...3 point mhimu ...

Sioni Tena game ya kututisha aisee ...Bado Liverpool aje etihadi ...
 
Sasa gap ni point 13 bt kama liver atashinda kipolo chake basi gap litakuwa point 8
 
Uzi huu Bwana yani pain killer unajiongelesha tu yani dah mpaka huruma[emoji23][emoji23][emoji23]
Wee jamaa unajitoa akili si bure, na usichokijua ni kwamba mshabiki wapo na hatuna presha...na hamna haja ya kupost hovyo hovyo kama nyie kwenye nyuzi zenu maana timu yetu sio mbovu kama zenu ivyo huwa sanasana tunapost MATCHDAYS TU...sio kam nyie kutwa comments kibao maana nikujadili vipigo na makosa ya wachezaji wenu daily sasa city hawan hizo mambo!
 
Kwa hiyo Uzi mzima unaona comment yangu tu ,au macho yako hayaoni πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Mkuu kwem?...naona jan ze blauz wamepotean kama kawaida yao, nilipotea kidog maana natumiaga PC kuingilia JF imekuf HDD nimnunua smart ndo nimerud mitambon kama kawida.
 
Chelsea wakitangulia kupata goli basi mechi imeisha hii.
Mkuu hii match ilinitisha sio kwamba chelsea walikuwa wanaupiga mwingi kuliko city hapana bali nilihisi itaisha droo maana nafasi nyingi sana zilikuw zinapotea kwa kina sterling na grealish...kiukwel striker anahitajika namim naon watu wakulenga ni wawili tu hapo Either HAALAND...ambaye tayari ameshaweka wazi msimamo wake kuwa hataki uhamisho kipindi hiki cha winter anataka iwe majira ya sammer na ukiconnect dots juu ya pep kutotak kusajil striker majira haya hadi june inamaan ishaeleweka dogo amezamiria kutua wapi.




OR huyu dogo wa fiorentina DV9...nimemfuatilia ni mtu kwelikweli na uzuri hajademand pesa kubwa vyanzo vinasem anapatikan kwa Β£41m tu na ata mshahara wake sio mkubwa huyu ni aina ya wachezaji wanaowez pokea wage ata Β£150,000 per week kitu ambacho kwa haaland ni kigumu yule ni wa Β£300+ per week na jamaa ana balance ,control na physique maana ni mref kazidiw kidog sana na haaland hivyo hata goal za header atatusaidia sana ila tofauti yao ni kwamba haaland tayar ameshaprove yeye ni worth player kwenye BIG STAGES tofauti na huyo dogo...pia kiumri Eerling ana 21yrs huyo dogo ana 23yrs at this moment waachane na huyo kane maan mwaka huu anagonga 29 hivyo anawez ingia kweny mfumo wetu ila hatutodum nae kama ilivyokuwa kwa aguero maana atakuw na misimu kama mitatu yakuchez kweny kiwang tofauti na hao wawili hapo. Kwa jinsi nilivyoangalia clip za huyo Dusan Vlahovch ni hatari pia ni wapili kwa magoli kule italy naamini kabisa ataufaa sana tukimkosa haaland ukizingatia na vilabu vikubwa kama madrid vinammezea mate pia.

Huyu ndo DUSAN VILAHOVICH dogo fundi wa kufunga kiukweli...





 
Mkuu kwenye kiungo hatuna sana huitaji maana rodri kafit vyem tu japo nilisoma source moja huko UK mahali kuwa mwezi june mwaka huu ferinandinho mkataba wake utaisha hivyo kuna mascout wa city wanamfuatilia kevin philips wa leed na endapo board itamwacha ndinho asepe huyo dogo atachukuliwa asaidiane na rodri pale dimbani pia itakuwa poa maana huyo dogo hana jina kubwa sana hadi asumbue kuja kutokea benchi pale city.
 
Yaani huyu Pep kwake EPL ni ligi ya kawaida.
Mwisho wa siku mumekubali wenyew wazee wa darajani kwamba Pep ndio njia ya kweli na uzima kuelekea kwenye ubingwa wa Epl...maana mechi ya kwanza mlikosa shoot on-target ata moja kwa dakik 90 na hii ya maruduiano mumepata on-target 1 na corner 1 tu, polen sana fan boys wa darajan...

 
Naon wamempa hadi man of the match....hatari sana huyo kiumbe!!!

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…