The Official Azam FC Thread

mbo
na mimi hii link kwenye simu yangu siipati?
 
lazima wakaze maana wapo home,na kama kawaida yao utakuta viingilio bure basi mashabiki teleee.
Kipindi cha pili ni kufa na kupona
 
Zanzibar Spice najua unatumia simu ya Shem wako.Sisi tunatumia vineo vya hela yetu,Ila poa tu ,tujuze matokeo
 
Hapa Azam lazima watumie wing kwa mbio,ili watumie mfumo wa kaunta atak,ili kuwapunguza kasi jamaa kujazana kwao
 
TV Nationale 2 Tunisie tazama live Wataniya 2 live online | Tunisie 14

Dakika ya 22'' Yallah! Yallah! huyu Coulibaly wa Esperance hatari sana !
Dakika ta 23'' Krosi ya Esperance inangonga mtambaa wa juu wa goli la Azam!
Dakika 25'' Jamaa wanaweka pressure kubwa kwa Azam FC lakini wachezaji wa Azam FC wametulia hawababaiki
Dakika 29'' Manula anadaka shuti kali la shambulizi la Esperance
Dakika 31'' Hawa jamaa Esperance wanacheza kwa kukamia mpira upo half ya pitch ubabe wa Azam FC tu
Dakika 44'' Hongera kwa wachezaji wa Azam FC hasa safu ya ulinzi pamoja na kipa Aishi Manula ni jihadi kwenda mbele Esperance hawaamini wanayoona!
Dakika 45'' shuti! Aishi Manula anaokoa inakuwa kona
Dakika 45 + 1 Mpira ni mapumziko

Studio TV Nationale 2 : Yaahni Yaahni hawa Azam FC ni wagumu mno mashambulizi yote tuliyofanya kipindi cha kwanzan hakuna bao, Inshaallah !ngoja tuone kipindi cha pili

Dakika 47 Goal kwa Esperance kutokana na adhabu ndogo , lakini naona pia watazamaji walitumia ''Laser Beam/Light'' kuuwa macho ya Aishi Manula!

Esperance 1 - Azam FC 0
 
shot on target esp 6 azam 0
corner 8 0
Hili ni tatizo kwa Azam,maana second half hawa jamaa hawatarudi hivyo
Lazima wazidishe presha,na azam ni wabovu saana kwenye presha za muda mrefu.
Na ukiangalia kwa hali hiyo ni kwamba strikers hawana majum,wapo wapo tu,na kati pamepotea kwa kuwa msaidizi wake inabidi arudi chini kusaidia ulinzi.Ni tatizo kubwa saana.
Inahitajia style ya Haruna Niyonzima,ili kurejesha uhai kati na kuweza kupanda mbele kwa kasi na kurudi kwa kasi
 
aisee mkuu unareport vizuri kweli,yaani kama vile watu wapo uwanjani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…