HANS POPPE: AZAM WATAKULA JEURI YAO
Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema Azam FC inalazimika kuvuna matunda ya ukaidi wao kwa kwenda kucheza ‘bonanza’ Zambia na kuacha Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ikiendelea.
“Hatukatai Azam na Yanga kupewa muda wa maandalizi wa mashindano yao ya Afrika, lakini huko nyuma walikwishakosea kwa kwenda kucheza bonanza na kuacha ligi,”.
“Matokeo yake sasa wanazidi kulundikiwa mechi za viporo na kupoteza ladha ya ligi, kama wasingekwenda Zambia, wasingekuwa na viporo vingi, ila kwa kuwa walikaidi mawazo ya timu nyingine, sasa wacheze Ligi,”amesema Hans Poppe.
Na sasa Azam FC ipo kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na Aprili 10 watamenyana na Esperance ya Tunisa Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Pili.
Wakiwa wanahitaji muda mzuri wa maandalizi, Azam FC watalazimika kucheza mechi za Kombe la TFF na za Ligi mbili katika wiki ambayo watacheza na Esperance.
Simba SC ndiyo inaongoza Ligi Kuu kwa sasa ikiwa na pointi 57, ikifuatiwa na Azam na Yanga zenye 50 kila moja, lakini Wekundu wa Msimbazi wana mechi tatu zaidi ya wapinzani wao hao kwenye mbio za ubingwa (24-21).
Source: Kwa Hisani Kubwa ya Bin Zubeiry HANS POPPE: AZAM WATAKULA JEURI YAO | BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE
Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema Azam FC inalazimika kuvuna matunda ya ukaidi wao kwa kwenda kucheza ‘bonanza’ Zambia na kuacha Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ikiendelea.
“Hatukatai Azam na Yanga kupewa muda wa maandalizi wa mashindano yao ya Afrika, lakini huko nyuma walikwishakosea kwa kwenda kucheza bonanza na kuacha ligi,”.
“Matokeo yake sasa wanazidi kulundikiwa mechi za viporo na kupoteza ladha ya ligi, kama wasingekwenda Zambia, wasingekuwa na viporo vingi, ila kwa kuwa walikaidi mawazo ya timu nyingine, sasa wacheze Ligi,”amesema Hans Poppe.
Na sasa Azam FC ipo kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na Aprili 10 watamenyana na Esperance ya Tunisa Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Pili.
Wakiwa wanahitaji muda mzuri wa maandalizi, Azam FC watalazimika kucheza mechi za Kombe la TFF na za Ligi mbili katika wiki ambayo watacheza na Esperance.
Simba SC ndiyo inaongoza Ligi Kuu kwa sasa ikiwa na pointi 57, ikifuatiwa na Azam na Yanga zenye 50 kila moja, lakini Wekundu wa Msimbazi wana mechi tatu zaidi ya wapinzani wao hao kwenye mbio za ubingwa (24-21).
Source: Kwa Hisani Kubwa ya Bin Zubeiry HANS POPPE: AZAM WATAKULA JEURI YAO | BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE