The one thing - Mafanikio ya kila kitu

The one thing - Mafanikio ya kila kitu

Travis Walker

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2017
Posts
323
Reaction score
334
Habari, natumai ni wazima nyote. Mimepamiss hapa Jamii Forums kwasababu nina muda mrefu sija post chochote na inatokana na maisha na ubize ila sio shida leo nimekuja na kanuni ya "The one thing". Hivi karibuni nimesoma kitabu kinaitwa hivyo "The one thing". Waandishi ni "Gary Keller" na "Jay Papasan".

Katika kitabu nimejifunza jambo moja muhimu sana na ndio nimeona bora kushare nanyi hapa. Jambo ambalo nimejifunza ni kwamba ili ufanikiwe katika maisha na utoboe ni lazima ufanye kitu kimoja mpaka ukimalize, bila ya kutengeneza muingiliano na kitu kingine. Yaani unatakiwa kufocus na kitu kimoja tu mpaka kiishe. Kama biashara deal na hiyo moja mpaka ikupe faida. Faida za kufanya jambo moja ni kama zifuatazo
1. Unapata muda wa kujifunza vizuri jambo hilo kuliko kama ungelifanya na kuacha njiani.
2. Unakuwa na mipangilio mizuri juu ya jambo hilo.
3. Unakuwa una enjoy the process kwasababu kuna progress moja tu unayo ifuatilia.

Madhara ya kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja
1. Kukosa umakini na ufanisi mzuri kwasababu akili inakuwa inachoka sana.
2. Kukosa muda wa kutosha katika managemnet.
3. Ni rahisi kukata tamaa iwapo vyote viwili havitofanikiwa kwasababu ya kuhisi umepoteza muda na nguvu nyingi.
4. Inachukua muda mrefu zaidi kukamilisha mambo mengi lakini jambo moja linachukua muda mfupi.
5. Iwapo financial resource ni chache upo uwezekano wa vyote kufeli

Niambie rafiki, katika mwaka 2022 ni lengo gani moja tu ambalo ungependa kulikamilisha?
Jee unaweza kulitaja tukupe ushauri wa kutoboa nalo?

Thanks
 
Binafsi naamini katka kufanya Mambo mengi maana ukifanya Jambo moja tu binadamu wanapenda kuiga mwisho wa siku utaigwa hatimae kugawana wateja lakn ukiwa na mishe nyngi wakikaba huku unatoboa na kwing
 
Binafsi naamini katka kufanya Mambo mengi maana ukifanya Jambo moja tu binadamu wanapenda kuiga mwisho wa siku utaigwa hatimae kugawana wateja lakn ukiwa na mishe nyngi wakikaba huku unatoboa na kwing
Ndio mkuu ila the one thing haijamaanisha maisha yako yote ufanye jambo moja bali imemaanisha fanya moja mpaka liishe na lifanikiwe ndipo uanze jengine
 
Mkuu iko kitabu kama ni pdf msaada please nitakuweka kwenye historia ya maisha yangu if kitanipa what i need
 
Katika maisha yetu hasa sisi wa Africa one thing its hard to implying bro...

Mambo ni Mengi muda mchacheee.
1. Some
2. Ujenge
3 Usomeshe
4 Uzazi
5.Kumiliki Cari

Vyote hivyo vinaitaji mpunga mrefu

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Katika maisha yetu hasa sisi wa Africa one thing its hard to implying bro...

Mambo ni Mengi muda mchacheee.
1. Some
2. Ujenge
3 Usomeshe
4 Uzazi
5.Kumiliki Cari

Vyote hivyo vinaitaji mpunga mrefu

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Unaweza kuamua kufanya jambo moja tu na likakuwezesha kufanya hayo mambo yote

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom