The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

Tabasamu,

Ndugu yangu msitake wacha awe hoja ya mazungumzo yetu hapa kwa sababu hata kama katumwa na CCM bado hawezi kuvuta vichwa vilivyomo humu.. Sio kazi ndogo hata kidogo!
Ila nawakumbusheni tu kuwa hata nyie mngepata taabu sana kuwafahamisha CCM, chama tawala ikiwa maswali yenu ni kama yafuatayo. nanukuu hapo juu:-
Mtu akisema leo anajiunga na CCM ni corrupt na anategemea mianya ya corruption to make the ends meet. Hao waliomo ni opportunists ambao hawezi kutoka kwa sababu njaa itawaua. Kama siyo corrrupt na opportunist huwezi kuacha kuhoji suala la Richmonduli na hilo la Buhemba watu kukausha dhahabu zetu halafu wananchi wanahamishwa tena eneo jingine kusudi jamaa wapewe tena vile wanajua Buhemba imejaa dhahabu.

Hawa CCM pia wataanza kudai ushahidi na kadhalika hali kila kitu kipo wazi.
Tujaribu kusaidiana na tuache kutazama nani muulizaji!.. yes, wananchi wanaweza kabisa kujiunga na upinzani na kuna kila sababu za wananchi kuwaunga mkono against CCM. Lakini tusije kuwa kama wa-Iraq ambao leo wanapambana na USA hali wakifahamu kuwa wao wenyewe hawapatani, kila kikundi kina malengo yake na kuna viongozi ambao ni hatari zaidi...
Binafsi kama ningekuwa Mu-Iraq kusema kweli ningekaa nje ya lingo la siasa na kuomba Mungu tu.
Hii ndiyo hali tunayoizungumzia!.. Freeman anajitahidi kiasi chake sana tu ila kuna haya maswali ambayo wengi wanashindwa kujitokeza kama vile wengi wasivyofahamu mchanganyiko wa siasa nchini Iraq.
Je, Unajua ya kwamba ktk makundi ya Iraq ni vigumu sana kuwepo suluhu?.. Kurdish (North) by majority ni Sunni lakini sio Waarabu.. Shia (east and south) by majority ni Waarabu sio Kurdish na Sunni (central and west) ni waarabu.kwa hiyo leo ugonvi wao upo ktk madhehebu bado kabisa halijaibuka la makabila kwani mauaji ya Kurdish yalifanywa na Waarabu chini ya Saadam which makes Shia muslim part of it. Hiyo sinema nyingine part 3.
Tunataka sana kumuondoa CCM na hizo sera zake feki, lakini kwa UWAZI wa malengo ya utawala wenyewe utakao replace CCM.
Kwa mtazamo wangu Wacha na Mzee Mwanakijiji wote bado wanadai kuwepo kwa upungufu wa viongozi kusimama kama Martin Luther King, Mandela na wengine aliowataja Quarz.. wala tusiende mbali niliwapa mifano ya Mtikila na Seif Hamad wa enzi hizooo......Uongozi kwa VITENDO sio MANENO.
 
Hakuna kitu kinachonipita akili yangu kama kutojibu hoja kwa kujifanya kujibu hoja! Maneno ya kebehi na dharahau yanaweza kuvutia hisia lakini hayashindi hoja. Je upinzani wa Tanzania jinsi ulivyosasa unaweza kukabidhiwa nchi nzima kuiongoza? Jibu langu ni HAPANA HAPANA HAPANA!! Je CCM jinsi ilivyosasa inaweza kuongoza nchi yetu jibu ni NDIYO NDIYO NDIYO! Je CCM na matatizo yake yote na mapungufu yake yanayoweza kujaza vitabu inastahili kupewa uongozi wa nchi jibu ni HAPANA HAPANA HAPANA, Je upinzania namapungufu yake yanayoweza kujaza juzuu wanastahili kupewa uongozi wa nchi jibu ni HAPANA HAPANA HAPANA!! Nitafafanua.

Chama cha Mapinduzi ni chama ambacho kimelewa madaraka na viongozi wake wengi wamebweteka na vyeo vyao na kutokana na chama hicho kukita katika kila kona ya maisha ya Watanzania basi viongozi hao hawaoni haja ya kulitumikia Taifa letu jinsi ile inapaswa! Pamoja na hayo yote, CCM imeweza kufanya mambo ambayo Watanzania wanayathamini licha ya kujua udhaifu mkubwa wa Chama hicho. Unafikiri viongozi wote wasomi walioko CCM hawajui udhaifu wa chama chao au ni sisi wewe kwenye Jambo Forum ambao ndio tuna akili zaidi kuliko Mtanzania yeyote?

Wengi wa wanachama wa CCM ambao wamepima upinzani na chama tawala wamechagua chama tawala. CCM inafanyiwa mabadiliko toka ndani, toka viongozi waliopo ndani, na toka wanachama waliondani. Hawasubiri wakosoaji walio nje kujiunga nacho ndio waanze kufanye mabadiliko!! CHADEMA, CUF, TLP na wenzao hawawezi kusubiri watu wajiunge nacho ndio waanze mabadiliko!!

Kuna watu wanajifanya wanajua historia hapa, bila ya shaka wanaijua historia ile inayowafaa wao na matakwa yao! Martin Luther King Jr hakuwa mwanasiasa, na kilichomsukuma sio haja ya kuwa na cheo cha kisiasa. Alisukumwa na imani yake!! Soma maandiko yake ya "Barua toka Jela ya Birmingham"!

Wanamtolea mfano Abraham Lincoln, nani aliwaambia Lincoln alikuwa mpinzani wakati alipotia sahihi "tangazo la kuwekwa huru" kwa watumwa kusini mwa Marekani? Je unajua hata tangazo lake halikuwafungua watumwa wote? Lincoln, alifanya mabadiliko hayo akiwa Rais wa Marekani! Kwa kifupi, kama kuna mtu anayeweza kuleta mabadiliko makubwa katika Tanzania si Mbowe, si Lipumba, si Mrema, ni Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!

Mmemtaja Mandela, Mandela alileta mabadiliko makubwa zaidi alipokuwa kifungoni au alipotolewa nje? Nitawaacha mfikiri nina maana gani hapo!

Quarz anadai ati siwezi kuwa mkosoaji tu na sitoi masuluhisho ya aina yoyote. Inaonekana hujafuatilia maandishi yangu. Mimi ni mkosoaji mkubwa wa serikali ya Kikwete, nilipigia kelele suala la Mahita kabla ya watu wengi kulipigia kelele, niliungana na wengine kupigia kelele suala la Richmond bila haya (na nikaitisha kuondolewa kwa Msabaha), nilipigia kelele mambo mengi ambayo wasikilizaji wangu wanayajua! Leo nikisimama na kusema kuwa licha ya kelele zangu CCM bado ni chama pekee kinachoweza kuongoza Tanzania watu wanadhani nimejigeuka! Hata kidogo. Mimi sina maslahi katika Upinzani, sina maslahi na CCM (sio mwanachama). Maslahi pekee niliyonayo ni yale yanayohusu Tanzania nzima na siyo chama au kikundi fulani cha watu! Ni kwa sababu hiyo siwezi kutetea kuikabidhi hatima ya Tanzania kwa watu wasio na nia wala uwezo wa kuongoza Taifa alimradi ati ni wapinzani na wao pia wanaichukia serikali ya CCM. Nina madhaifu mengi, lakini ujinga wa kisiasa sio mojawapo!

Nimetoa mapendekezo ni nini upinzani ufanye ili ujiweke mahali pazuri pa kushinda watu wanadhani ninawaletea husuda! Kama wao wanasubiri watu wajiunge nao ndio waanze kujiimarisha, basi waendelee kusubiri!! Anzeni kujiimarisha wenyewe msisubiri hisani ya CCM! CCM haina mpango wa kuwaimarisha wala haina nia ya kuona mmeungana!! Papa mkaange kwa mafuta yake!

Kuhusu hilo la kunitakia nifie huku huku niliko, wala halinitishi kwani nikifa au nikiwa hai mimi ni mali ya bwana, na nitakufa kama Mtanzania, kama nitafia kwenye ardhi ya wazazi wangu au ugenini!! Anyway, nakutakia wewe na wenzio muishi maisha marefu na ya afya, na muweze kuitumikia nchi yetu kwa kujituma zaidi kuliko wale ambao wamefanya hivyo hadi sasa.

Wabillah Tawfiq!
 
Somahapo juu!!! Naona huyu jamaa hana mchango wowote wa kuleta kwa Watanzania. Bora aishi huko huko aliko, afie huko. Elimu yake haijamkomboa. Ana mawazo mafinyu mno! Sijui hata historia hakuisoma?

Duh!
I am sorry, but this does NOT describe the Mzee Mwanakijiji I have come to know since joining these arena.

Kama haya ndio majibu ya ki-chadema kwa hoja zake, mtazidi kutuchosha.
 
Mwanakijiji: Sikumbuku ni wapi na lini wapinzani wamewahi kuomba. kutaka au kutamani CCM iwaimarishe! We are not that naive; don't put your words in our mouth.
 
Duh!
I am sorry, but this does NOT describe the Mzee Mwanakijiji I have come to know since joining these arena.

Kama haya ndio majibu ya ki-chadema kwa hoja zake, mtazidi kutuchosha.

Sasa hapa ndipo shida inapoanza, mtu akiwa na jibu tofauti anaambiwa anajibu ki-chadema. Jamani lazima muelewe kuwa humu tunatoa mawazo yetu sio ya chadema hata kama baadhi yetu ni wanachama wa chadema. Kama alivyosema Mkandara, tuangalie hoja, sio nani katoa hiyo hoja. Shambulia hoja, usimshambulie mtu, ebo!
 
Kwa wale wanaosema vyama vya upinzani vidai kwanza katiba, nakubaliana nao. Ili ni vizuri kutambua kuwa mabadiliko makubwa kama ya katiba hayawezi kuachiwa vyama vya upinzani pekee, ni ya wananchi wote isipokuwa watawala ambao wanaridhika na mfumo uliopo kwa kuwa unawanufaisha. Actually, ukiangalia kwa makini mabadiliko ya katiba katika sehemu nyingi hayakuongozwa na vyama vya upinzani. Vinara wa mabadiliko ya katiba Kenya walikuwa maaskofu, wasomi, civil society groups. Vyama vya upinzani vilitumika tu kama vehicle ya kutekeleza haya mabadiliko. Tusikwepe majukumu. Sote tunawajibika. Kwa hiyo lugha ya 'wao wana..' inabidi iachwe, tuongelee 'sisi tuna..' in as so far as mabadiliko ya katiba yanahusika.
 
Politics is a dity game, For you to win you need to know how to play better than your opponemnts. ITS AS SIMPLE AS THAT!
 
DUA,
Mtazamo kwamba siasa ni mchezo mchafu ni hatari, wanasiasa na viongozi wa sasa ndio wa chafu, siasa si mchezo mchafu. Ikiwa unakubali kwamba siasa ni mchezo mchafu, fahamu uchafu hauna mipaka!Tukianza mashindano ya uchafu tutaliangamiza taifa badala ya kulisaidia.

Ikiwa kwenye uchaguzi wa jimbo yalifanyikia mapinduzi ya "kijeshi" CHADEMA na wangejibu? Tungekuwa tunamsaidia mtanzania? Nimesema yalikuwa ni mapindui ya kijeshi kwa kuwa chaguwa la wati lilipinduliwa akawekwa kiongozi mwengine akisindikizwa na magari ya ffu wenye silaha za moto! Je je haya si mapinduzi ya kijeshi?

Ikiwa tutaendekeza uchafu wa CCM na kuwajibu kwa uchafu zaidi tutafika wapi? Silaha pekee ni nguvu ya umma, kuaamsha waliolala kwa miaka 45 na huo ndio utakuwa mwanzo wa utungu!!
 
Mfano mdogo tu, kule USA Bush alishinda kwa kuwatumia majaji wa high (Republicans) court kumtangaza kuwa mshindi. Na sisi TZ lazima tuweke mikakati kama hiyo au inayolinganalingana.
 
Mwanasiaa na wengine nakubaliana nanyi madai ya Katiba ni muhimu . Wapinzani naona hawako makini na hili kila mara hata sijui sababu kubwa ni kitu gani . Viongozi wa dini Tanzania kusema mabadiliko hapana hawawezi maana wote wako mfukoni mwa Rais na wote wanatumikia Chama cha Mapinduzi kuanzia Wakatoliki na Waislam na madhehebu mengine. Na Sasa Lowasa ana ndoto za Urais ndiyo kabisa ana hangaika na Walutheri wake kila kona .

Haja ya ujenzi wa demokrasia ni yetu sote na si wapinzani maana wanao umia wengi ni wananchi wa kawaida wakati Viongozi wakiwemo wa dini wanapeta .
 
kichwamaji, unayoyasema kuhusu CCM yaweza kusema dhidi yavyama upinzani na yatakuwa kweli!! Hivi wapinzani hawatangulizi Matumbo yao?

Sikiliza Mwanakijiji,

Watu corrupt wako pote kwenye CCM na kwenye upinzani. Hata nje ya taasisi hizo, wamo. Hoja hapa ni kwamba si corruption yao inayowapeleka kwenye upinzani. Lakini hulka hiyo hiyo ndiyo inayowapeleka CCM, kwa sababu there is something to reap within CCM! Upinzani hauna cha kuvuna, unahitaji kujengwa. Tena ni bahati nzuri kwamba watu sasa wamefikia kutumia resources zao kujenga upinzani. Wasioona mbali wanawacheka. Ikumbukwe TANU ilijengwa hivyo. Kuna watu walitoa pesa zao kuunga mkono harakati za kuleta mageuzi na mabadiliko ya kimfumo. Jitihada hizo zimekufa baada ya TANU kukamata serikali na kuzaa CCM, ambayo sasa inatumia kodi ya watanzania kufanya mambo yasiyo na maslahi kwa Watanzania.

Tunahitaji kufikiri kama watu wa kizazi tofauti. Upinzani wa leo hauwezi kujengwa kwa kufuatafuata maagizo ya CCM na staili yao ya kufanya siasa. Wakati umefika, sasa yanahitajika mapinduzi ya lazima katika fikra zetu, ili kuathiri mwenendo wetu na utendaji wetu katika masuala ya kisiasa.

CCM sasa kimekuwa kichaka ambamo kina anayetaka kula kwa mikono miwili bila kunawa anajiunga nacho, maana ndiyo maficho. Vijana waadilifu hawendi huko siku hizi. Ukiona mtu ambaye hakuzaliwa CCM, na ni msomi, anatamani kujiunga CCM, ujue kuna mawili. Ama usomi wake haujamwezesha kuijua CCM, au naye anatamani kufanya yale wanayofanya hao tunaowasema - mabovu.

CCM hapa ilipofikia, pa kuongozwa na wasanii wasio na vision, kina JK na EL, wanaojiita wajamaa huku wakiishi ubepari, wanaofadhiliwa na wahindi na waarabu wanaozengea mikataba na migodi minono - rejea suala la Patel na Mchuchuma - CCM inayoongozwa na Makamba...ujue sasa tumefika mahali nchi imo mikononi mwa wajinga! The country has gone to the dogs!

Watu wenye uchungu na nchi yao wanapaswa kujua hilo na kuchukua hatua kuwaimarisha wapambanaji katika opposition, si kuwapiga mawe. Kila element nzuri inayochomoza kwenye opposition inafaa itumike kujenga hatima ya taifa letu...

Wakati unakaribia kwa ufalme wa CCM kung'oka. Historia inaonyesha kuwa falme zote duniani zilivuma, lakini ilifika mahali zikaanguka kwa sababu kama hizi ninazoziona ndani ya CCM. Wasiokubaliana na mtazamo huu, waendelee kuamini watakavyo. Siku ukweli ukidhihirika tutaambizana na kukumbiushana haya. Lazima tuangalie mbali ya pua zetu, kama kweli tunataka kujiita wachambuzi.
 
Maneno mazito haya Kichwamaji na jina lako libadilike liwe Kichwakuzuri na wengine hao wawe vichwa maji maana unamwaga hoja nzito .
 
Hakuna cha hoja nzito wala nini. Ni maneno yenye kuonekana na hekima lakini ndani yake yamevuja kihoja. Kwanini Wapinzani wameendelea kupoteza mvuto kwenye jamii ya watu wa kawaida? Kwanini Wapinzani wamepoteza viti kwenye uchaguzi uliopita? Je ni watu wangapi wanahama CCM na kujiunga na upinzani ukilinganisha na wapinzani kujiunga na CCM? Bila ya shaka majibu yako yatakuwa, tatizo ni CCM, tatizo ni Serikali ya CCM, tatizo ni kuibiwa kura, tatizo ni vyombo vya dola n.k!! Yawezekana kuwa hayo ni sehemu ya tatizo!!

Hata hivyo, badala ya kwenda mbali kumtafuta mchawi wa upinzani Tanzania, kwanini msiangalie ndani ya nyumba zenu (vyama). Katiba ni tatizo moja, lakini siyo tatizo pekee, kama mngeweza kutilia mkazo kuchukua Bunge badala ya Urais mngekuwa na uwezo mkubwa wa kufanya mabadiliko kuliko kuliacha Bunge limezwe na CCM! Au mtadai pia kuwa mlishindwa kuchukua viti vingi vya Ubunge kwa sababu Katiba ina mapungufu!

Lets be real! kama upinzani wataendelea kufanya mambo yale yale, kwa namna ile ile, wakitarajia matokeo tofauti (ambayo ni mazuri) basi vizazi vitapita wao wakibakia kuwa wasindikizaji.
 
Hakuna cha hoja nzito wala nini. Ni maneno yenye kuonekana na hekima lakini ndani yake yamevuja kihoja. Kwanini Wapinzani wameendelea kupoteza mvuto kwenye jamii ya watu wa kawaida? Kwanini Wapinzani wamepoteza viti kwenye uchaguzi uliopita? Je ni watu wangapi wanahama CCM na kujiunga na upinzani ukilinganisha na wapinzani kujiunga na CCM? Bila ya shaka majibu yako yatakuwa, tatizo ni CCM, tatizo ni Serikali ya CCM, tatizo ni kuibiwa kura, tatizo ni vyombo vya dola n.k!! Yawezekana kuwa hayo ni sehemu ya tatizo!!

Hata hivyo, badala ya kwenda mbali kumtafuta mchawi wa upinzani Tanzania, kwanini msiangalie ndani ya nyumba zenu (vyama). Katiba ni tatizo moja, lakini siyo tatizo pekee, kama mngeweza kutilia mkazo kuchukua Bunge badala ya Urais mngekuwa na uwezo mkubwa wa kufanya mabadiliko kuliko kuliacha Bunge limezwe na CCM! Au mtadai pia kuwa mlishindwa kuchukua viti vingi vya Ubunge kwa sababu Katiba ina mapungufu!

Lets be real! kama upinzani wataendelea kufanya mambo yale yale, kwa namna ile ile, wakitarajia matokeo tofauti (ambayo ni mazuri) basi vizazi vitapita wao wakibakia kuwa wasindikizaji.

Hoja nzito hizo Mzee Mwanakijiji usikatae; hapo juu mwanangu umepwaya, hujaongea kitu kipya. Umerudia yaleyale yaliyokwisha jibiwa mara kumi na tano!
 
Unajua Mwanakijiji wewe unapotea sasa . U CCM wako unakutoa maana sana ndugu . Watu wamegundua hili na ndiyo watu wamehama radio yako wanaishia Radio Butiama . Unauliza na kusisitiza mambo ambayo hata mkulima wa kawaida mwenye elimu ndogo anajua . Hivi kama kuna FFU kwa mfano ilivyokuwa pale Tarime , Arusha , na majimbo mengine watu wanatanganzwa kwa lazima huko Bukoba wapinzani hawana uwezo wa FFU bado wanaweza kuwapata wabunge wengi Bungeni kivipi ?

Watanzania waliwapwa wapinzani kura nyingi lakini ukisikia yaliyo tokea utashangaa . Wewe hata kadi ya kupigia kura huna na kwenye kampeni ulitegemea nipashe iseme sisi tuko hapa na tumeyaona wenyewe LIVE unataka kusemaje ? Ulitaka wapinzani wachukue silaha za jadi kupambana na CCM wakati wana risasi za moto na wanalamisha matokeo ? Unajua Musoma mjini kulitokea ? Si hata Makamu wa rais kuzomewa na kukosa watu na badala yake FFU waliwavamia wanachi wakirudi toka Mkutanoni na kuwapiga na kuwafungia ndani akiwepo mgombea wao kwa Amri ya Makamu wa Rais kisa kakosa watu ?

ushabiki mwingine unakuwa wa kijinga sana. Toa hoja za kuisifia CCM lakini Nchi inakufa na sote wana CCM na wapinzani tunakufa na hata sisi tusio na vyama .

We need rais mwenye Honesty na Intergrity wa kumweleza Lowasa kwamba wacha watu waaamue .Lakini JK na Lowasa wameshiriki kwa kutumia pesa za umma kuwanunua wapinzani wa Chadema Tarime kisa Mbunge wa Tarime anawatetea wananchi wenye eneno la madini . JK kafanya ziara 2 kule kuhakikisha Chadema inakufa lakini kakuta wakurya wana elewa kachukua viongozi wale . Wanao rudi CCM unajua wanalipwa kiasi gani ? Kama Kaburu kanunulika na kapata Ubunge vipi wengine ?

JK na CCM yenu mnanunua hata Media kusifia leo unaongea nini hapa ?
 
Lunyungu,
Mwaga vitu kaka. Wazungu wanasema "once bitten twice shy." Sasa yale yaliyotokea Musoma na Tarime, wakijaribu tena CCM kufanya hivyo 2010 watakiona. Watu wameanza kuamka.
 
Hoja hujibiwa kwa hoja!

Mnadai hoja nzito, haya ngoja niwanyang'anye tonge mdomoni! Mnaweza kuwaandikia wengine hoja dhaifu kama hizi wakaziamini, bahati mbaya madai yangu kuwa mimi ni "mchambuzi niliyebobea katika masuala ya siasa na jamii" siyo ya bure!! Naweza kuona uongo wa hoja hata kama zipambwe kwa maneno mazuri maili mia moja kabla hazijanifikia!

Sikiliza Mwanakijiji,

Watu corrupt wako pote kwenye CCM na kwenye upinzani. Hata nje ya taasisi hizo, wamo. Hoja hapa ni kwamba si corruption yao inayowapeleka kwenye upinzani.

umesema vizuri kuwa watu corrupt wako pote "kwenye CCM na kwenye Upinzani" halafu unajichanganya unaposema walioko kwenye upinzani "siyo corruption inayowapeleka" kule! Sasa corruption kwenye upinzani imefikaje? Kama wanaoingia CCM wana "Hulka" ya corruption ndio maana wako kwenye CCM, wale watu corrupt walioko upinzani "hulka" yao ni nini? Kitu hakiwezi kuwa na kutokuwa kwa wakati mmoja kikihusisha kitu kilele kizima siyo kama sehemu ya kitu ( It is impossible for a thing to be or not to be concerning the same thing as a whole not as a part!) Kama kuna watu corrupt kwenye CCM na hivyo kufanya CCM kuwa corrupt, basi kama kuna watu corrupt kwenye upinzani, basi kunafanya upinzani kuwa corrupt!

Lakini hulka hiyo hiyo ndiyo inayowapeleka CCM, kwa sababu there is something to reap within CCM! Upinzani hauna cha kuvuna, unahitaji kujengwa.

Upinzani hauna cha kuvuna? are you kidding me? Unachotaka kutuambia ni kuwa walioko upinzani ni malaika wasiovutiwa na pesa, sifa, ukubwa, na heshima! Unataka kutuambia kuwa walioko CCM ndio binadamu pekee ambao wanapenda ujiko na ruzuku za chama! Unataka kutuambia kuwa wapinzani wote (hata wale corrupt) wakipewa msosi wa nguvu watakataa! Ushahidi unao wewe mwenyewe. Kama baadhi ya viongozi wa upinzani na wanachama waliweza kurubuniwa na kununuliwa na CCM hadi kuhamia CCM, je watu hao walikuwa hawana hulka ya corruption walipokuwa upinzani au hulka hiyo waliipata walipojiunga na CCM! Kama viongozi wa CCM wanaweza kununuliwa na watu wenye maslahi fulani wakanunulika na tukawaita wako wafisadi, kwanini wale wa upinzani wanaonunulika wasiitwe wafisadi pia? Kama baadhi ya viongozi wa CCM wako corrupt na hivyo kufanya CCM kuwa chama kibovu, kwanini viongozi corrupt walioko upinzani wasifanye upinzani kuwa mbovu? This is an extreme example of double standard!!

Tena ni bahati nzuri kwamba watu sasa wamefikia kutumia resources zao kujenga upinzani. Wasioona mbali wanawacheka. Ikumbukwe TANU ilijengwa hivyo. Kuna watu walitoa pesa zao kuunga mkono harakati za kuleta mageuzi na mabadiliko ya kimfumo.

Kwa maoni yako ni sawa kwa wapinzani kutumia resource zao kujenga upinzani, na ni sawa waasisi wa TANU kutumia mali zao kujenga chama chao, lakini leo ni dhambi kwa wapenzi na mashabiki wa CCM kutumia mali zao kujenga chama chao! Hili haliingii akilini hata chembe. Kama Mbowe na wenzake wanaweza kutumia majina yao, mali zao kujenga CHADEMA ni dhambi gani kwa Rostam Azizi, na matajiri wengine ambao ni mashabiki wa CCM kutumia mali zao kujenga chama chao! Ni sawa kwa wapinzani kufanya hivyo (wanapewa sifa ya kujitolea) lakini ni vibaya kwa wanaccm kufanya hivyo (wanabezwa)?

Jitihada hizo zimekufa baada ya TANU kukamata serikali na kuzaa CCM, ambayo sasa inatumia kodi ya watanzania kufanya mambo yasiyo na maslahi kwa Watanzania.

Hili hata sitaki kulielezea kwa kina. Hakuna kitu kibaya katika kujenga hoja kama "haste generalization". Madai kuwa CCM inatumia "kodi ya watanzania, kufanya mambo yasiyo na maslahi" yamezidishwa! Ubadhirifu wa mali za umma upo na mimi wa kwanza kukemea, viongozi wabaya wapo majina nimeyataja, viongozi wasio na uwezo wa kuongoza wanajulikana! Lakini kusema kuwa CCM kupitia serikali yake inafanya mambo yasiyo na maslahi kwa Watanzania kwa kutumia kodi zao ni tusi ambalo kila Mtanzania asilikubali! Je wamefanya yote ambayo tungependa wafanye? la hasha! (mifano ya mabadiliko ya Katiba, utekelezaji wa tume wa ya Warioba na ile ya Jaji Kisanga inanijia); Je wamefanya jinsi ile tungependa wafanye? hata kidogo!(mifano ya mikataba mibovu ya nishati na madini ni dhahiri) Je kuna mambo ambayo wameyafanya yenye maslahi kwa watanzania!! jibu ni NDIYO!! (nitajaza vitabu kuanza kuorodhesha). Hili tendo la kudharau na kukebehi mafaniko na mambo mazuri yaliyofanywa na CCM kuliwagharimu wapinzani!! Mwenye macho haambiwi "tazama"!

Huwezi kwenda kijijini na kuwaambia wananchi CCM haijafanya lolote wakati wanaona barabara ya lami! Huwezi kuwaambia CCM haijafanya lolote wakati wanaona shule zinajengwa, visima vinachimbwa, kliniki zinakarabatiwa!! Endeleeni kudai CCM haijafanya lolote muone kama watu watawachagua!

Tunahitaji kufikiri kama watu wa kizazi tofauti. Upinzani wa leo hauwezi kujengwa kwa kufuatafuata maagizo ya CCM na staili yao ya kufanya siasa. Wakati umefika, sasa yanahitajika mapinduzi ya lazima katika fikra zetu, ili kuathiri mwenendo wetu na utendaji wetu katika masuala ya kisiasa.

Tunajaribu kuwasaidia kuwapa "mapinduzi ya fikra" lakini nyinyi wagumu! Mnafikiri kila mtu anayekosoa upinzani basi ni mwana CCM au hautakii mema upinzani! kalaghabao! Wakati mwingine huna budi kuiga mbinu za mpinzani wako. Jifunzeni siasa za nchi nyingine muone ni jinsi gani kutumia mbinu za ushindi za chama tawala zaweza kuwapeleka madarakani! Unafikiri Bill Clinton aliingia madarakani bila kuiga mbinu za chama cha Republican? Nenda wikipedia na tafuta "triangulation politics" utajua nina maana gani!

CCM sasa kimekuwa kichaka ambamo kina anayetaka kula kwa mikono miwili bila kunawa anajiunga nacho, maana ndiyo maficho. Vijana waadilifu hawendi huko siku hizi. Ukiona mtu ambaye hakuzaliwa CCM, na ni msomi, anatamani kujiunga CCM, ujue kuna mawili. Ama usomi wake haujamwezesha kuijua CCM, au naye anatamani kufanya yale wanayofanya hao tunaowasema - mabovu.

Au ameona udhaifu wa upinzani na ameona mahali pekee anakoweza kwenda kuleta mabadiliko ni CCM. Ulimwengu hauna mambo mawili tu ya kuchagua. That is one of the oldest fallacies in the book - you only have two choices! "Kusuka au Kunyoa". no you don't. Labda nataka nizichane tu!

CCM hapa ilipofikia, pa kuongozwa na wasanii wasio na vision, kina JK na EL, wanaojiita wajamaa huku wakiishi ubepari, wanaofadhiliwa na wahindi na waarabu wanaozengea mikataba na migodi minono - rejea suala la Patel na Mchuchuma - CCM inayoongozwa na Makamba...ujue sasa tumefika mahali nchi imo mikononi mwa wajinga! The country has gone to the dogs!

Fanyeni hima mje kututoa utumwani enyi manabii wa ahadi!! Wapinzani wanaofadhiliwa na Wamarekani, Waingereza, na Wajerumani ni bora kuliko CCM inayofadhiliwa na Wahindi na Waarabu! Kama kufadhiliwa na watu wasio weusi ni kosa, Chadema wawe wa kwanza kutupia CCM mawe!

Watu wenye uchungu na nchi yao wanapaswa kujua hilo na kuchukua hatua kuwaimarisha wapambanaji katika opposition, si kuwapiga mawe. Kila element nzuri inayochomoza kwenye opposition inafaa itumike kujenga hatima ya taifa letu...

Tunajaribu kuwaimarisha lakini nyinyi mnafikiri tunawatakia mabaya!!

Wakati unakaribia kwa ufalme wa CCM kung'oka. Historia inaonyesha kuwa falme zote duniani zilivuma, lakini ilifika mahali zikaanguka kwa sababu kama hizi ninazoziona ndani ya CCM. Wasiokubaliana na mtazamo huu, waendelee kuamini watakavyo. Siku ukweli ukidhihirika tutaambizana na kukumbiushana haya. Lazima tuangalie mbali ya pua zetu, kama kweli tunataka kujiita wachambuzi.

yeah right! CCM ing'oke kisa Chadema, CUF, TLP jinsi zilivyosasa!! Endeleeni kutamani nchi ya ahadi!

Unajua Mwanakijiji wewe unapotea sasa . U CCM wako unakutoa maana sana ndugu . Watu wamegundua hili na ndiyo watu wamehama radio yako wanaishia Radio Butiama .

Dues na Radio Butiama naziunga mkono kwa nguvu zote! Wala usidhani linanitia wivu au linanifanya nishtuke. You have no idea how petty that sound! Kusikiliza maoni ya upande mmoja peke yake ni ufinyu wa kisiasa!

Halafu mmeng'ang'ania miye CCM! Niwaambie mara ngapi mimi si mwanachama wa chama hicho! Lakini ukinipa uchaguzi wa vyama upinzani, CCM au mambo mengine pamoja na udhaifu wote! I'll still pick CCM! mamilioni wengine wanakubaliana nami!
 
Mwanakijiji unaonyesha mfano mzuri wa kujibu hoja kwa hoja. Nii matarajio yangu wengi wetu tutafuata mfano huu, bila matusi na kumdhalilisha mwandishi hata kama aliyoandika hukubaliani nayo.

Ingawaje sijaisoma!
 
Mzee Mwanakijiji umesema vema sana!

Mzee Ole umesema vema pia kuhusu umuhimu wa kujibu hoja kwa hoja, na KUPINGANA BILA KUPIGANA!

Let's keep this spirit!
 
Back
Top Bottom