The reason Gaddafi was ousted..he intended to withdraw all of the Libyan oil billions from Europe

Haina mchango kwa watanzania. Inawezekena wewe mleta mada hii ni pro-CCM ambayo imefanya yote haya yashindikane. Upuuzi mtupu kutuleta hapa.

umeshajiuliza kwanini wamarekani,wachina ama mataifa mengine yaliyoendelea huleta watu wao kuja kufanya kazi kwenye nchi hizi zinazoendelea? if you are not learning from others then that's not learning.kujua kuwa Libyans lived such kind of life ni funzo tosha.mchango ni kuongelea kuhusu siasa? huko ni kupotoka na yaonyesha jamii ya watu kama wewe ndiyo kikwazo cha maendeleo.think beyond it not behind it
 

Oh yeah nawakumbuka sana hao jamaa. Ilikuwa miaka ya 86/87. Baadhi yao kama siyo wote, walikuwa wakiishi kwenye guest house moja hivi pande za Sinza.

Walikuwa wakikatiza tulikuwa tunawashangaa sana. Tulikuwa tunawaona sijui ni watu wa wapi tu.
 

ukweli ni kuwa jamii ya Libya inajuta kutokana na kukubali kuwa deceived na Westerns.yaliyotajwa si uongo wala si tambo za walibya ili waonekane wanamaisha bora.demokrasia ndiyo imeizika Libya ni jamii iliyokuwa na kiu ya kumuona mtu aliyekaa kwenye madaraka kwa miongo zaid ya minne akiachia madaraka.muamar alikula na vipofu bila kuwashika mkono ila kelele za majirani tena wale wa mbali zilishambulia maskio ya vipofu wale.walibya hawakujua kuwa gadafi ndiye mpishi wa yale yote,hawakujua kuwa ilihitaji mtu asiyejua kuwa pesa hazina mwisho.

jamii hii haijawahi lalamika juu ya huduma za jamii ilizipata kila ilipohitaji walilalamikia democracy.takwimu zilionyesha raia wa Libya wanaishi vizuri kuliko wa marekani.
 

Watu wanaongelea Libya wewe unaleta habari za South Africa. Mwenzako kapita wiki 1, wewe Jee?
 
Mkongwe umeongea vizuri na kuichambua ripoti ya libya kama vile ulikuwa ukiishi libya. Wanajuta na wameshapoteza dira ya umoja wao, Sasa nchi inayumba yumba "hawako huku wala hawapo kule" marehem col: Gaddafi alilewe utawala.
 
Oh yeah nawakumbuka sana hao jamaa. Ilikuwa miaka ya 86/87. Baadhi yao kama siyo wote, walikuwa wakiishi kwenye guest house moja hivi pande za Sinza.

Walikuwa wakikatiza tulikuwa tunawashangaa sana. Tulikuwa tunawaona sijui ni watu wa wapi tu.
Exactly Nyani Ngabu,kumbe tulikuwa wote UDSM
 

Inamaana wewe ungekuwa mmoja kati ya NTC? Sidhani kama hadi leo usingejutia uamuzi wako.kumbuka serikal ya Libya imejitahidi kuwekeza kuliko karibia serikali zote kama sio zote kabisa ndani ya Africa.gaddafi alijua kunyanyuka bila kushikwa na magharibi inawezekana na ndio maana alitoa wazo la USA kubwa kwa maana ya united states of Africa.hawakupewa elfu 50 kama ulivyosema bali walipewa dola elfu 50 around 75 millions za kitanzania.walipewa mahari kwa kila kijana anaeoa.mambo hayo hata America hawajayafanya.ni nchi ipi iliyofikia hatua yakudistribute wealth directly kiasi hiki kwa raia wake? Hata siku moja sijawahi kusikia walibya wakilalamika kuwa gaddafi alikuwa fisadi...baadhi ya mawazo ni yale yaliyosemwa na midomo ya waamerika kama anavyosemwa hasad leo hii na Obama.tunagesi songosongo tunaye rais kikwete iwapo gesi hiyo itasaidia japo kujenga nyumba ya kuishi wazee nitafute nina zawadi yako.

Yapo mataifa mangapi yaliyoshindwa kufanya aliyoyafanya gadafi? Congo wana utajiri kiasi gani? Nani anaufaidi? Tanzania tuna utajiri kiasi gani na nan anaufaidi?

Nadhani ukimpinga gadafi ni kuwasha taa ya hatari kwa rais wetu..tehtehteh natania utendaji wake n mzuri anatulisha kama gadaffi alivyofanya kwa raia wake
 
Wewe Jamaa inaonekana unaongea vitu kwa ushabiki na hisia tu. Mimi sijawahi ona mtu anayefanya vizuri alafu anashambuliwa na jamii hiyo anayoifanyia mambo mema. Gaddafi unayemsema alikuwa ameigwa libya katika vipande walioajiliwa ni watu wa kabila lake na wengine walipewa viposho tu vya kujikimu huyo ndo mtu unataka kutuaminisha kuwa ni mwema kafanya mazuri.

Hilo siyotatitzo: Ulitakiwa uisome libya then utuambie njia ya kupita ilitufike huko unapopasema na siyo hizi takataka kutoka kwenye magazati ya Udaku.


Ila nimeendelea kuelewa akiri zako zilipo ila sitataja kama mtu mmoja alivyawahi kusema kuhusu wabunge wa dar.
Umekosea jukwaa, ulitakiwa uende jukwaa la mapishi. Huku sio kwako
 
Gaddafi alianza kuongelea US of Africa baada ya kukorofishana na mataifa ya kiarabu kwa hiyo huku ndo palikuwa pa kutokea kwa warafi. Kama unakumbuka vita ya kumtoa mataifa ya kiarabu yalitoa mchango mkubwa sana kuhakikisha anatoka madarakani kwa hiyo alikuwa kero tu. Hajawekeza popote Afrika ila kajenga misikiti.
 
Jifunze kuandika vizuri kwanza kabla hujaanza kuleta hoja zako.
Again, umekosea jukwaa. Ulitakiwa uende jukwaa la mapishi. Hapa sio kwako. Gracias!
 
Watu wa aina yako wana jina kwenye lugha ya wenzetu. Wanaitwa " Penny wise Pound Foolish"
Jifunze kuandika vizuri kwanza kabla hujaanza kuleta hoja zako.
Again, umekosea jukwaa. Ulitakiwa uende jukwaa la mapishi. Hapa sio kwako. Gracias!
 

Unauhakika na unachokisema? Kaiulize Uganda iwapo maneno hayo n yakweli jirani tu hapo.muamar hakuyumbishwa na upepo wa maneno ya watu.sisemi aonekane bora ila nimesimama kwenye upande wa kuonyesha mazuri yake.....wakati gadaffi anatolewa madarakani wengi walitoa mchango na gadaffi hakuuogopa umoja wa waarabu.alidiriki kuwashutumu kwa kukaa kimya baada ya Iraq kuingiliwa na marekani katu hakunyamaza.Arab states unazoziongelea ndiyo hizi zenye viongoz wanaochaguliwa na wamagharibi? Kuna dhana moja ambayo wamagharibi huitumia "destroy his fame before destroying his life" dhana hiyo ndiyo iliyomnyonga sadam Hussein na ndiyo iliyomuua gadaffi.wako wapi wale waliomburuza shujaa wao barabarani? Wamepewa kipi? Gadaffi alikuwa na lengo lakuonyesha ukweli kuwa umoja ni nguvu..
 
Katika miaka ya kati ya tisini nilibahatika kukutana na wanafunzi toka Libya, nikiwa nje ya Tanzania kama mwanafunzi. Kama kawaida ya Watz, tukadadisi jamaa wanalipwa shilingi (dola) ngapi kwa mwezi.

Bila kubana maneno Walibya wale walituambia kuwa wanalipwa dola elfu tatu kwa mwezi. Sie kutoka Tz tukilipwa dola mia tano kwa mwezi, na tena sio kwa wakati kwani muda mwingine ilikuwa inapita hadi miezi mitano bila malipo yoyote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…