The rise and fall of Colonel Muamar Gadaffi

The rise and fall of Colonel Muamar Gadaffi

Ghadafi aliijenga Libya na kwa ulevi wake wa madaraka amebomoa alichojenga! Mimi nikiambiwa nichague mtawala mwenye busara kati ya Ghadafi na Mubarak nitamchagua Mubarak. Hata kama aliondoka baada ya shinikizo kubwa la wananchi wake,lkn angalau aliona Misri ni kubwa kuliko urais wake,familia yake,marafiki zake na chama chake. Na kwa hali halisi ilivyo sioni kama utawala wa Ghadafi utadumu miezi 2 kuanzia sasa. Wanachofanya waasi kwa kusaidiwa na NATO ni kulivuta nje ya Tripol jeshi lake kwa kupigana ktk fronts nyingi. Mwisho waizunguka Tripol. Baada ya hapo mambo mawili yanaweza kutokea. Moja ni kwa wananchi waliopo Tripol kuandamana na kuuangusha utawala wa Ghadafi,pili ni vita ya umwagaji damu mkubwa ktk mitaa ya Tripol kati ya waasi na jeshi la Ghadafi.
<br />
<br />
hupaswi kulaumiwa kwani habari unazopata ni za CNN,BBC na Aljazeera. Kwa taarifa yako Gadaf anakubalika sana Libya kwa misimamo yake ya kutetea rasilimali za nchi, pia yuko vyema sana ground war, hivyo waasi na waroho wa mafuta Nato bado wana kazi kubwa kumng'oa Gadaf.
 
Serikali ya Libya imekanusha madai kuwa kiongozi wa muda mrefu wa nchi hiyo kanali Muammar Gaddafi na familia yake wanapanga kutoroka nchi. Khalid Kaim, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Libya amesema kuwa, Gaddafi na familia yake wataendelea kuwepo nchini humo; na ametupilia mbali madai kwamba familia hiyo imeomba hifadhi katika nchi za Misri, Morocco, Tunisia na Algeria. Baadhi ya duru zinaripoti kuwa, hali ya kiafya ya kanali Gaddafi sio nzuri na tayari mwakilishi wake anafanya mazungumzo na Uingereza na Ufaransa ili wamtoroshe kiongozi huyo kutoka nchini humo hasa baada ya wanamapinduzi kuzidi kusonga mbele siku baada ya siku. Waziri Mkuu wa zamani wa Libya, Abdul Salam Jalloud amerejea nchini humo kuungana na wanamapinduzi wanaoendelea kuudhibiti mji wa kiistratejia wa Brega wenye utajiri wa mafuta. Aidha, wanamapinduzi hao wameripotiwa kuidhibiti miji nyeti ya pwani ya Az Zawiya na Zintan.
 
Wanamapinduzi wa Libya wameripotiwa kudhibiti uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tripoli, huku wakiendelea kuelekea katika makao makuu ya Gaddafi katikati mwa mji mkuu huo. Hii ni katika hali ambayo milipuko kadhaa na milio ya risasi ilisika usiku wa jana katika maeneo kadhaa ya mji huo. Wakati hayo yakiripotiwa Mohamed al Harizi afisa wa ngazi za juu wa wanamapinduzi wa Libya amewaambia waandishi habari kwamba, wanamapinduzi 123 wameuawa katika wilaya ya Tajoura mjini Tripoli. Hata hivyo amesema wilaya hiyo ingali mikononi mwa wanamapinduzi hao pamoja na eneo jingine la mji huo la Souq al Jumaa.
Wakati huo huo Kanali Muammar Gaddafi wa Libya amewataka wanaomuunga mkono kuandamana kwa mamilioni na kusitisha kile alichokiita uasi wa muda mrefu dhidi ya taifa hilo. Pia Gaddafi amezituhumu nchi za Magharibi na wanamapinduzi wa nchi hiyo kuwa wanapigania utajiri wa mafuta wa Libya.
Habari zaidi zinasema kuwa Thabo Mbeki Rais wa zamani wa Afrika Kusini amezikosoa nchi za Magharibi kwa kurefusha vita vya Libya. Mbeki amesema kuwa, kama nchi za Magharibi zingesikiliza mapendekezo ya viongozi wa Kiafrika, kungekuwa na uwezekano wa kusitishwa mapema zaidi vita vya Libya. Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini aidha amesema, Umoja wa Afrika ulitoa mapendekezo ambayo yalikubaliwa na serikali ya Libya lakini vikosi vya nchi za Magharibi vilitoa mashinikizo kwa viongozi wa Afrika kuhusiana na suala hilo.
Katika upande mwingine Tunisia imelitambua Baraza la Kitaifa la Mpito la Libya ambalo linajumuisha viongozi wa upinzani kuwa mwakilishi rasmi wa wananchi wa nchi hiyo. Wizara ya Mambo ya Nje ya Tunisia imetambua baraza hilo lenye makao yake katika mji wa Benghazi hatua inayoifanya nchi hiyo jirani na Libya kujiunga katika safu za nchi zinazompinga Kanali Muammar Gaddafi.
 
Tusubiri tuone! Sidhani kama Qaddaf atakubali kuanguka kirahisi, na kuna hofu (ya taarifa) kuwa amefukia milipuko sehemu nyingi za tripoli na akiona upepo uko kama ulivyo sasa basi analipua.
 
jaman gadaf, wazungu wazungu tu wakitaka utoke utatoka
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
<br />
Alipaswa alitambue hilo mapema. Juzi niliona documentary nadhani ni discovery world inaitwa secret wars jinsi cia walivohusika na kuziondoa madarakani kwa namna mbalimbali tawala kadhaa afrika, latin america na maeneo mengine.
 
source iko wapi? Weka source then tutaendelea kuijadili post vinginevyo hatupotezi muda wetu. Propaganda!
 
nadhani sasa mtaanza kukubaliana na mimi, kwamba Kuna Coordinated MISINFORMATION YA HALI YA JUU ili kuonyesha kwamba WAASI wako on the verge ya kuikamata TRIPOLI wakati infact ni uongo.
Kama Mkiweza Kuprove habari hizi kwamba ni Uongo, basi msiziamini habari zinazoletwa na waasi, kwa sababu ni propaganda zenye lengo la kuudanganya ulimwengu kwamba rebels wanamake progress on the ground ili waendelee kubuy time, na kuendelea kuvumiliwa na wananchi wa nchi za NATO ambao slowly wanaquestion vita hii, na pia kuweka pressure kwa nchi ambazo bado zinaitambua serikali ya Ghadafi, kwamba mtu mnayemsapoti ataanguka karibuni, wakati ngoma bado mbichi kwelikweli huko libya!.
 
Wanamapinduzi wa Libya wameripotiwa kudhibiti uwanja wa ndege wa kimataifa wa Tripoli, huku wakiendelea kuelekea katika makao makuu ya Gaddafi katikati mwa mji mkuu huo. Hii ni katika hali ambayo milipuko kadhaa na milio ya risasi ilisika usiku wa jana katika maeneo kadhaa ya mji huo. Wakati hayo yakiripotiwa Mohamed al Harizi afisa wa ngazi za juu wa wanamapinduzi wa Libya amewaambia waandishi habari kwamba, wanamapinduzi 123 wameuawa katika wilaya ya Tajoura mjini Tripoli. Hata hivyo amesema wilaya hiyo ingali mikononi mwa wanamapinduzi hao pamoja na eneo jingine la mji huo la Souq al Jumaa.
Wakati huo huo Kanali Muammar Gaddafi wa Libya amewataka wanaomuunga mkono kuandamana kwa mamilioni na kusitisha kile alichokiita uasi wa muda mrefu dhidi ya taifa hilo. Pia Gaddafi amezituhumu nchi za Magharibi na wanamapinduzi wa nchi hiyo kuwa wanapigania utajiri wa mafuta wa Libya.
Habari zaidi zinasema kuwa Thabo Mbeki Rais wa zamani wa Afrika Kusini amezikosoa nchi za Magharibi kwa kurefusha vita vya Libya. Mbeki amesema kuwa, kama nchi za Magharibi zingesikiliza mapendekezo ya viongozi wa Kiafrika, kungekuwa na uwezekano wa kusitishwa mapema zaidi vita vya Libya. Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini aidha amesema, Umoja wa Afrika ulitoa mapendekezo ambayo yalikubaliwa na serikali ya Libya lakini vikosi vya nchi za Magharibi vilitoa mashinikizo kwa viongozi wa Afrika kuhusiana na suala hilo.
Katika upande mwingine Tunisia imelitambua Baraza la Kitaifa la Mpito la Libya ambalo linajumuisha viongozi wa upinzani kuwa mwakilishi rasmi wa wananchi wa nchi hiyo. Wizara ya Mambo ya Nje ya Tunisia imetambua baraza hilo lenye makao yake katika mji wa Benghazi hatua inayoifanya nchi hiyo jirani na Libya kujiunga katika safu za nchi zinazompinga Kanali Muammar Gaddafi.

FCK NATO REBELS
<strong><font color="#ff0000"><font size="4">
 
Last edited by a moderator:
Kweli wazungu wameupania utajiri wa Libya!
Ebu tupe source ya izo news maana kama nia Al jazeera itakuwa ndo wale wale maagent wa NATO
 
Huu ni uongo mtupu hakuna ukweli hata kidogo katika hizi habari hawa wanapika uzushi tu waonekana wanashinda lakini hamna kitu
 
cjaona wanamapinduzi hapo zaidi ya vibaraka wa western Europe wanajichinja bila wao kujua, wait and see what will happen after Ghadaff's fall
 
cjaona wanamapinduzi hapo zaidi ya vibaraka wa western Europe wanajichinja bila wao kujua, wait and see what will happen after Ghadaff's fall

After Gaddafi's fall the nation will be similar to Somalia,Iraq, or Afghanstan..

Mwenyezi Mungu atuepushe na janga kama hilo....aaameeeeen
 
Source please.
<br />
<br />
source ya nini wakati jamaa anakibarua kigumu kupigana na wagomvi wa dunia ila mi naona hurumu kwa watakaobaki hai libya watamkumbuka gaddafih mpaka itabidi wamlaani mungu pasipo na sababu yoyote.

we subiri baada ya vita kuisha ndo mtajua jamaa alikuwa hataki kutoka kuonesha ni jinsi gani anawapenda wa libya. wazungu wa us na uk hawapendi kuona afrika inaendelea ndo maana hawamalizi vita..

Mungu ibariki libya
Mungu ibariki Afrika
Amina!..
 
Back
Top Bottom