The story of my life: Ukweli mchungu baada ya kugundua mtoto tulie naye hakuwa mtoto wangu

The story of my life: Ukweli mchungu baada ya kugundua mtoto tulie naye hakuwa mtoto wangu

Mtoa mada, Kuna watu hapa Duniani Kwa sababu ya Ubaya wao Huwa ama hawatakiwi uwape huruma au hawastahili kabisa kuishi... Hi ndio kanuni ya Asili ikiwa Unahitaji Furaha na Mafanikio.

Kwann nimesema haya.....


Kakusaliti, Kabeba mimba, mbaya zaidi kuendelea kudanganya mpaka hatua ya mwisho ya kuomba Msamaha.


Alafu Et bado, Ukamwachia Kila kitu, Ukamwachia na Gari [emoji1787][emoji1787][emoji1787].

Kwamba ndo Ugud Guy??? ... Wee ni mpuuzi tu.


Kwahiyo ukayaacha hayo yote ukaenda kulala chini ? ???. Wee ni mjinga.



What if , Taasisi uliyopo katika kupunguza wafanyakazi ,nawee ungepunguzwa?.

Hya Bidada , anaolewa na Mwanaume mwingine, au Huyo Mzeee alozaa naye , Gari linakua la Mzee [emoji1787][emoji1787], Kitandan ulichoanzia Maisha , anatombewa hapohapo.



Vipi Mama yako ana gari?? Vipi thamn za kwenu za ndan Kwa Mama yako? Mama yako anakitanda kizuri??

Hayo maswali yatoshe kukupimisha kama wee ni mpuuzi au Lah !!.



Itoshe tu kusema haya, Inawezekana ni tukio la kweli ila umeongezea chumvi Kwa sehem baadhi au Stori kama zingine !!.



Kwa namna nilivyo mbinafsi , Mwanamke anifanyie ivooo[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] labda kama Mimi sio wa Kanda ya ziwa !!.
Nakazia huyu Jamaa ni mpuuuuziii sana
 
Mtoa mada, Kuna watu hapa Duniani Kwa sababu ya Ubaya wao Huwa ama hawatakiwi uwape huruma au hawastahili kabisa kuishi... Hi ndio kanuni ya Asili ikiwa Unahitaji Furaha na Mafanikio.

Kwann nimesema haya.....


Kakusaliti, Kabeba mimba, mbaya zaidi kuendelea kudanganya mpaka hatua ya mwisho ya kuomba Msamaha.


Alafu Et bado, Ukamwachia Kila kitu, Ukamwachia na Gari 🤣🤣🤣.

Kwamba ndo Ugud Guy??? ... Wee ni mpuuzi tu.


Kwahiyo ukayaacha hayo yote ukaenda kulala chini ? ???. Wee ni mjinga.



What if , Taasisi uliyopo katika kupunguza wafanyakazi ,nawee ungepunguzwa?.

Hya Bidada , anaolewa na Mwanaume mwingine, au Huyo Mzeee alozaa naye , Gari linakua la Mzee 🤣🤣, Kitandan ulichoanzia Maisha , anatombewa hapohapo.



Vipi Mama yako ana gari?? Vipi thamn za kwenu za ndan Kwa Mama yako? Mama yako anakitanda kizuri??

Hayo maswali yatoshe kukupimisha kama wee ni mpuuzi au Lah !!.



Itoshe tu kusema haya, Inawezekana ni tukio la kweli ila umeongezea chumvi Kwa sehem baadhi au Stori kama zingine !!.



Kwa namna nilivyo mbinafsi , Mwanamke anifanyie ivooo🤣🤣🤣🤣 labda kama Mimi sio wa Kanda ya ziwa !!.
hayaja kukuta mzee
 
Hongera kwa kuwa Mungu amekujalia hekima ya kuamua vema, Pamoja na yote aliyokutendea huyo mwanamke, hujampiga wala kumdhalilisha, Ubarikiwe sana.
 
Umesema kisa chako ni miaka 9 mpaka 10 iliyopita alafu tena huo mwaka baada ya manzi yako kupata mimba ukanunua gari ukaanza kupiga na mishe za uber na uber imekuwa established bongo 2016??

CHAI
2016 mpaka leo ni miaka saba tayari, chai iko wapi?
 
Ni kweli usemalo, ila kwenye maisha progress ni muhimu sana. Hakuna anayependa kuanza upya, tena baada ya jitihada kubwa sana alizofanya.

Jamaa kalea mimba mpaka imekuwa mtoto, fanya kazi usiku na mchana, ila mwishowe ikabidi aachie vyote. It's not easy kaka mkubwa.
Very very true [emoji109]
 
Huuu uniceboy unawaharibu sana aisee,,,yaan mm apo nilivyokauzu na roho mbaya anageondoka na nguo tu asieee
 
-Kwanini ulimwachia vitu vyote hivyo?

-Alitoa asilimia 8 tu kwenye kununua gari. Angeenda kuanza upya na huo mchepuko wake. Alikudanganya sana hakustahili huruma ya kuachiwa vitu.

-Ila karma is a good teacher, yatamrudi ipo siku.

-Kama mwanaume mwenzio nimeumia roho sana. Umepitia mazito na magumu.

-Pole sana kaka.
Kabisa, ni changamoto kubwa sana hii

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
MWANZO WA MAISHA MENGINE





Baada ya kuja na dada yake pale kukawa na kikao mwenyewe akaniomba aniambie kila kitu,me nikamwambia aniambie tu ukweli

Akaniambia ni kweli alikuwa anadate na yule mzee na walianza nae kitambo alikuwa kama sugar dady wake na alikuwa anasafiri nae sana kwasbabu huyo mzee nature ya kazi yake ni kusafiri sana alikuwa anampa hela na nini vitu vingi hapo kati kati alikuwa anamsaidia sana.

Hapo tulikuwa wawili dada mtu alitupisha nikamuuliza swali nikamwambia niambie ukweli kuhusu mtoto na naomba usinidanganye ili nirudishe imani kwako na kwa ufupi tu nimeshachukua sample ya nywele nataka kupeleka kupima DNA(hii nilimdanganya),so naomba ukweli niupate kwako nisiende kuupata sehem nyingine

Nikaona mtu akapiga magoti huku analia akanii jina langu kiukweli huyu mtoto ni wa flani akamtaja yule mzee

Nikamuuliza what happened ilikuaje hadi ukapata mimba ya yule mzee

Akaniambia yule mzee ni mtu mwenye mke na watoto wakubwa tu na mimi niliona kwenye picha ya yule mkwe wa yule mzee facebook

Akasema baada ya kudate nae akiwa side chick akaja kukutana na mimi badae yule mzee aligundua kuwa anadate na mimi kwa sababu alikuwa ratiba zake zikawa hazieleweki kama zamani kumbe kipindi hicho yupo na mimi

Yule mzee anasema akamuuliza kuhusu kupata mtu mwingine akasema ndio anaye mtu mwingine akulizwa kama ananipenda akasema ni kweli ananipenda

Yule mzee akampa option kuwa kama akiniona nafaa basi aendelee na mimi,basi kumbe kipindi hicho huku mapenzi yamenoga kwangu story niyingi company nzur na akasema kwangu akaona kuna feature kule ye alikuwa kama side chick tu

so akamwambia mzee , mzee akawa mbishi kumwachia aende mara amtishie kuwa atanifata aniambie kuhusu uhusiano wao sasa sijui alikuwa anaona angeharibiwa kotekote sasa dada akawa anatumanage wote kwa pamoja.

Akaniambia kipindi flani nilisafiri kama miezi 2 hv hatukuonana nikiwa narud dar yeye anakuwa amesafiri kumbe dada alikuwa ameshakata shauri la kuachana na mzee ili aje kwangu kwa hiyo alikuwa kama amempa mzee mara ya mwisho kama ndio ya kuagana na mzee alikuwa hawez kuwithdraw since wako pamoja ndio mana kama unakumbuka kule mwanzon aliniuliza ninawezaje kumbe mzee ilikuwa hivyo na anhisi hicho kipindi ndio alipata ujauzito coz alichanganya siku zake na mzee kama alimfanyia kusudi kwasababu alivyomwambia mzee akamwambia atalea.

Me baada ya kurudi tulionana almost after miezi miwili kwa hiyo huyo mtoto sio wa kwangu ila naomba sana nimsamhehe yeye alishaachana nae.

Nikamuuliza mbona anakupigia kila siku kama umeachana nae?akasema anamsumbua kujuli hali mtoto

Nikamuuliza mbona kuna transactions anakutumia naona unazipokea akawa hana jibu ansisitiza nimsamehe.

tukarud nyumbani nikamwambia naomba nitafakari na naomba usije ukawapigia simu nyumbani kwetu kuwalilia kwa sasa kwani wamesikitishwa sana ka hili (nilimwambia hivyo ili asipige simu home kwani alikuwa amekubaliuka sana asilete complications zingine ila kiukweli hapo home sikusema chochote)

Basi nikaondoka nikaenda nikaenda kwa mshkaji wangu mmoja usiku ule nikamzuga gheto kuna wageni kesho nikaamkia job nikarud tena kwa mshakji,yeye alikuwa anapiga simu sipokei namtumia tu sms niko salama.

Baada ya kutafakari sana nikaona siwez kuishi kwenye uhusiano ni bora nikae pembeni basi siku ya tatu nikarudi nyumbani nikamsalimia nikambeba mtoto nikamwangia sana kwa huruma malaika yule hana hata hatia na alikuwa maeshanizoe kama baba yake coz kila jion nikirud lazima nicheze sana ndio alale, nikasema wacha niwapishe wawe na maisha yenye amani nikalala nyumbani,

Kipindi hicho pale tulipokuwa tunakaa ilikuwa kama miez miwili hv kodi kuisha kulivyokucha nikaenda bank tulikuwa na saving zetu kidogo nikampigia mwenye nyumba nikamwomba nimwekee kodi mana miez michache iajyo naweza nisiwe vzur alikubali nikmwekea kodi ya miezi 6 na kiasi kilichobaki kidogo nilichukua.

nilivyotoka bank nikarud mtaa flani nikamwomba dalali anitafutie chumba kimoja,kufika jion akawa amekipata nikaenda nikalipia mwenye nyumba akaniambia hata kesho niende kuhamia.

Nikatoka hapo jioni nikaarud nyumbani mud huo mi nalala sebuleni

Kesho yake nikaenda mwenge nikanunua godoro na ndoo moja na kopo la kujimwagilia,nikanunua na pasi ya philips nakumbuka,nikaenda kwenye chumba kipya nikanunua taa nikanunua na net na kamba nikfunga tok =a kwenye dari

Jioni nikarud home pale nikamwita nikamwambia mimi nimekusamehe ila siwezi kuendelea na wewe tena na pia hili pia sijawaambia watu maana ni aibu yetu sote naomba iwe hivi me naomba niondoke hapa nyumbani nakuachia kila kitu vitu vya ndani hadi gari naomba nikuachie kwasababu tulilinunuan sababu ya huyu mtoto me nitaenda kuanza upya basi nikaingia nikachukua vyeti vyangu,mashrt na trousers za kuvaa ofisini na viatu vyangu na slipers nikaweka kwenye bag dogo niakondoka

hakuamini akawa anaivuta huku analia me niakondoka zangu nikaenda kwenda kuanza upya kwenye kagheto changu.

Na huo ndio ukawa mwisho wa uhusiano wetu,alinitafuta sana badae akawa hadi anakuja kunisuburia ofisini akaja kuona nimeamua hivyo basi na yeye akaamua aanze maisha yake

Hatukuwasiliana kwa muda kidogo kuna muda hapo kati kati tuliwasiliana kidogo na yule mtoto anaendelea vzur sasa hv kakuwa mkubwa huwa namwona kweye status akimpost na kwa upande wangu nashkuru naendelea vizur



Ahsanteni



Mwisho.

kaka bonge moja la story...kwa sisi warusi tunasema больше спасибо...
 
kmmae kapigwa na kitu kizoto, haya mambo ya kuoa mwenye kijiajira ati "msaidiane maisha" mara akusaidie kununua kigari ndio ukubali pia kuna wanaume watakusaidia kuchokonoa, ati anasafiri kikazi nye nye nye. Qmmae haya lete simulizi usituchoshe
Hahaha
 
KUANZA KUUJUA UKWELI

Naomba tuendelee sisi tulikuwa na group la tuliomaliza primary miaka hiyo ya 90's mwishoni, sasa kama mnavyojua mkiwa na group halafu wote mnajuana toka utotoni kunakuwa na utani mwingi sana,na me nilikuwa miongoni mwa wachangia mada maarufu kwenye group, sasa siku hiyo mada ilikuwa NDOA,wakawa tunasemwa watu ambao hatujaoa katika story kuchanganya ukatoka mkeka pale yakawekwa majina ya watu wote ambao hawajaoa na nini utani uakawa mwingi sana na mimi nikiwepo kwenye list.Badae kidogo yule Rafiki yangu nurse akanitext inbox

Nurse: mambo vp

Mimi: nikamwambia poa

Nurse: Huonekani siku hz?

Mimi: Nikamwambia nipo huwa nakuja ofisini kwako lakini tunapishana

Nurse: akasema poa, nimeona jina lako hapo kweye mkeka kwani we bado hujaoa?

Mimi: Nikamwambia ndio ni kweli bado sijaoa

Nurse: Yule unayekuje nae ni nani kwako sasa?

Mimi: Nikamwambia yule ni mchumba wangu bado hatujaoana tutaanza mchakato soon tukitulia.

Akanijibu tu okay, ikaisha hivyo

Kumbe yale maswali alikuwa anuliza vile kwa sababu kuna kitu alikinotice kitambo na aliambiwa na nurse mwenzake ambaye mara Nyingi alikuwa anamuattend yule mchumba wangu pale clinic na siku za mwanzo alinitambulisha kwake na walituona nilivyokuwa naenda pale hospital na mchumba wangu.

Baada ya kumjibu vile aliondoka kutafakari mwenyewe nakuomba ushauri huko (hii alikuja kuniambia badae sana kwamba anikaushie mshakaji wake au anisanue ukweli), kwasabau alikuwa anajua sisi ni wanandoa Tayari na yeye kumbe yule Rafiki yake nurse mwingine akamwambia mbona huyu mkwe wa Rafiki anakuja na card mbili alikuwa anawatoa kidogo wanajaza detail kwenye card zote mbili.na hizo card 2 za clinic zina majina mawili ya baba tofauti moja langu lingine la huyo baba mwingine sasa yeye aliogopa hapo mwanzo kusema alihisi mayb tumeshaoana akaja kuvunja ndoa ya watu akaona akaushe sasa nilivyomwambia hatujaoana ni kama nikampa mawazo mengine ya kuomba ushauri nakutafakari aniambie au aendelee kukausha kingine akawa hana uhakika kama kati yetu pale nani ndio mwenye mtoto.

Ukapita kama mwezi na siku kadhaa hv nikaja kuonana nae tukasalimiana nae fresh badae jioni akanitumia text akaniambia naomba utafute time tuongee na nakumbuka aliniandia baadhi ya maneno nayakumbuka hadi leo "naomba uje ukiwa peke yako ukiwa na utulivu na akili za kiutu uzima"

Me sikutilia umakini sana hayo maneno coz me ni mtu wa utani sana kwenye class letu so nikahisi tu nipunguze utani na nini basi,siku ikafika ilikuwa wekend j2 nakumbuka nikaonana nae baada ya story 2 3 anakaniuliza una kifua nikamwambia ndio, akaniambia bwana kuna kitu amekiona kwa mchumba wangu aliambiwa na staff mwenzake pale ofisini kwao na kuna siku aliitwa kwenda kuangalia mchumba wangu alivyoenda pale clicni ckuwa mchumba wangu inaonyesha ana card 2 za clinic zenye majina mawili tofauti hivyo akaniomba nifanye utafiti wangu kama ni kweli.

Sasa alivyoniambia hivyo me sikumwelewa mana nilikuwa sina kabisa huo utaalamu na by then nilikuwa sijazisikia sana hizo story, akanielewesha kuwa card zina majina ya baba wawili tofauti moja ni wewe nyingine ni mtu mwingine naomba uwe mtulivu ukafatilie hili.Me moyoni nilishtuka ila sikutaka kumwonyesha pale, basi nikamshukuru pale tukaagana.Nikarud home nilikuwa na mawazo kweli nikajikaza pale nikazuga tu issue za kazi na nini,nikawa nafikiria jinsi ya kutafuta nafasi ya kuangalia hiyo card yingine ipo wapi na nilishindwa kucheck kwa haraka coz yeye bado alikwa kwenye ile ya kuwah kutoka job kwasababu ya kutoka martenity karibuni so nikawa natafuta upenyo wa kuweza kuitafuta hiyo card nyingine.Sikumwonyesha kama nimenotice chochote ila nikawa nidigest tu mwenyewe kindani ndani inawezekanaje hili basi nikawa natafakari.

Bahati nzuri week ile ile kukawa na nasafari katikati ya week ilikuwa siyo siku ya kazi aliniomba nimpeleke mahali wanaenda na dada anayetusaidia kazi na bahati nzur yule mkwe wangu alikuwa ameondoka mara moja then atarud so ikawa tunaondoka wote me nikawa na funguo kuwa nawapeleka huko then wakimaliza nitaenda kuwafata.

Basi baada ya kuwafikisha tu chap nikurudi fasta nikaaza kutafuta taratibu kwenye vitu pale nyumbani kwenye documents ambapo najua card huwa inawekwa ikawa hola, nikaona ile card moja yenye jina langu badae nikaenda kwenye kabati la nguo zake nikatoa zote hadi chini sikuiona kitu nikawa naanza kukata tamaa nikasema nirudishe nguo moja moja sasa nikawa nakung'uta naicheck nikaenda nikakuta kwenye vitenge flani vilikuwa vipya havijavaliwa alipewa zawad ya kujifungua alivipanga pamoja katikati nikakuta bahasha na nilivyoifungua ndio nikaiona hiyo card.

Kiukweli nilishtuka sana yani mikono ikawa inatetemeka hivi kuifungua, kweli baada ya kufungua nikaona hiyo kwenye jina la baba lipo lingine nakumbuka kichwa kilikuwa kizito sanaa ile unaskia "nziiiiii",nakumbuka nilijilaza kwenye kitanda naangalia ceiling kama 1hr hv mawzo mengi kichwani kichwa Kizito.

Likanijia wazo hili swala ni zito ngoja nisali kwanza nipate hekima ya kudeal nalo, huwa nakuwa huivyo nikipata kitu kizito sana huwa nasali ili niweze kudeal na jambo lolote linaloniendesha.Baada ya kusali nakumbuka nilirudi kitandani kichwa kinauma nilisinzia kama nusu saa hv then nikashtuka nikarudisha vile vile vitu ila kabla ya kurudisha kitu kikniambia nikipige picha then nikachukua na kile chenye jina langu nikachukua boda nikaenda stationary ya za maeneo ya chuo nikavitoa copy nikaweka kwenye bahasha nikarud navyo home ili kesho yake nikavifiche ofisini.nikarud tena kitandani kutafakari na kuamua nisimuulize chochote kwa sasa nifatilie vitu vingine kwa umakini,badae nikawafata nikawarudisha home.

Sikumwonyesha chochote ila kichwa na moyo wangu uliingiwa na uzito flani wa ajabu sana kuna muda nikiwa nacheza na mtoto namwangalia moyo unauma namwomba Mungu anipe busara na uvumilivu nitajua tu.

Zikapita siku 2 3 nikawa bado natafakari chakula hakipandi,nikapungua ghafla.nikiwa najiuliza nitapataje evidence nyingine kwasababu mchumba wangu alikuwa anaongea sana so nikataka sababu ya uhakika zaidi na mtoto sina access nae ya full time ya kusema umchukue ukapime DNA,kuna wazo likanijia kama card nyingine ipo na ina information inamaana huyo mzazi mwengine pia ana mawasiliano nae nikasema ngoja niangalie simu yake kwasababu nilikuwa sina mazoea ya kushika simu yake kabisaaa.

Nikawa namfatilia ili nipate nafasi ya kuishika simu yake ilikuwa na password ya pattern nilifanikiwa kumfatilia hadi nilijua password yake na ,nikafanikiwa siku moja alikuwa nje nikafanikiwa nikaijua kwenda kwenye message hamna kitu nikasema niende kwenye call history nikaona kuna no.kama kwa siku 4 mfulukizo inapiga asubuh na jioni mida ya saa tisa au 10 jioni.Nikaichukua hiyo no na zingine 2 zilizotokea kwenye call history mara nyingi hv niakenda kutest kuchek jina ikaleta jina moja kama la yule kwemye card.

-Siku moja nikachukua tena nikasema kama kuna issue inawezekana kuna ndugu yake mmoja walichat nae, nikaenda kuserch kuangalia conversation ya ndugu zake nikaja kukuta conversation ya muda mrefu ya yule sister ake waliokuwa wanakaa nae kwenda huko nikakuta conversation za kuna muda anamtaja yule jamaa anamuulizia anaendeleaje ,huyu anajibu hajambo kuna text akawa namuuliza sasa utafanyaje mchumba wangu akawa anajibu yani amechanganyikiwa sijui it seems jamaa alikuwa anasumbua kiaina.Nikazipiga picha zile text nikarudisha simu.

Kipindi hicho kulikuwa na mshakaji mmoja alikuwa nafanyia kazi mtandao wa simu ya ile no nikamwomba anichekia hiyo no ya huyo jamaa huwa inapiga saa ngapi kwenda no ya mchumba wangu na location ya hiyo no mara nyingi inaonekana inapiga ikiwa wapi?jamaa alikuwa mtata kidogo kunipa hizo info coz kuwa wanabanwa sana kutoa taarifa ilibidi nimdanganye kwa kutengeneza story flani ya uongo na nikamwomba anisaidie kindugu me sitaweza kusema nimetoa wapi me nataka nipate info za kuanzia tu,basi nikapata taarifa kuwa jamaa mara nyingi anapiga asubuh na jioni mida ile ile kabla sijarud na pia huwa anamtumia mpunga kidogo na kujua jamaa kumbe yupo dar hapa hapa,kingine yule mshkaji wamtandao akanipa no nyingine inayowasiliana sana na ile no ya jamaa kuchukua ile no kuchek ni jina la kike nikajua huwa itakuwa kazi yake nyingine.

Muda wote huo ilikuwa kama week imepita since nijue ila sikumwambia chochote ila alinotice siku hz nakuwa na mawazo nikawa namdanyanga kuna kazi ofisini zina presurre kubwa sana na chakufanya kwasababu huwa narud usiku nikifika kuoga na kulala halafu usingizi hauji hadi ile kazi ya uber nikastop kufanya nikawa sirud home mapema nasema kuna kazi nyingi ila haikuwa hivyo nilikuw anatoka ofisini nafika mahali napaki gari naanza kufikiri.

nikaingia mission nyingine ya kutaka kufaham sura ya mshkaji, nikaingia facebook nikaanza kuseach jina la yule jamaa nikakosa nikasema nitest jina la ile no nyingine ya mwanamke niliyopewa na yule jamaa yangu ya mtandao nikamwona na picha zake nikaona ni mmama amabye anafamilia na watoto wakubwa tu na pia kunapicha zingine yupo na muwe wake ambaye ni mtu mzima kidogo akiwa amemtag kwa jina la sirname ambayo halipo facebook ila linaendana na kwenye ile card basi name then nikaichukua screenshot ya picha yake.

Then siku moja kuna time nilichukua simu ya mchumba wangu nikaisave ile no nikaenda whatsapp kucheck dp ni no ya yule yule jamaa anaoenakana ni mtu mzima mwenye umri kama 46-50 hv basi nikajirisha nikachuka na picha ya kwenye dp, ila kiukweli ilikuwa ni tukio la wiki kama moja na nusu - 2 ila nilikwisha yani nilikongoroka kabisa.

Wekend iliyofata nikamwomba twende mahali tutoke out,me kabla ya kwenda kule nilichukua ile copy ya vyeti nikaweka kwenye bag la laptop nikampitia tukafika pale piga story mbili tatu me nikachomekea mada kwasasa toka tumefahamiana kuna kitu gani ambacho yeye hajaniambia aua amenificha?akaniambia hamna kila kitu nakijua hajanificha kitu,akaniuliza kwann nauliza nikamwambia nataka kufaham akasema hakuna.

Nikamtajia jina la jamaa unamfaham flan

Yeye:flani yupi?

Mimi:Nikamtajia full name yake lote

Yeye: akasita akasema hamjui ila usoni nikawa namuona ameshachange kabisa

Mimi:Nikachukua picha nika mwonyesha, akasema hamjui,no ya yule jamaa nilikuwa nimeisave nikamwonyesha ile no akasema hajui chochote huku uso wa hofu

Yeye:Hajui chochote

Mimi:nikamwomba simu yake akasita badae akanipa nikmwomba atoe password,moja kwa moja nikaenda kwenye call list yake nikamwonesha ile no nikamuuliza ile no imefata nini kwenye simu yake na huwa anapigiwa mara kwa mara?

Yeye:akasema ni mtu ambaye anamfatilia kumuaproach

-Baada ya kumbana sana na evidence akasema yule ni ex wake,nikamwambia kama ni ex mbona mnawasiliana hadi sasa hv?

-akawa hana majibu

-Badae nikatoa zile copy za vyeti nikamuonyesha nikamuuliza hiki ni nini mbona mtoto wetu ana card mbili na moja wapo ina jina la huyo unayesema ni ex wako?

I see yule dada aliishiwa nguvu kidogo azimie akaanza kulia kwa sauti na kuomba msamaha analia kwa sauti nikaona hapa balaa watu wakawa wanashangaa kuna nini palee ikabidi nimwombe anyamze tuondoke pale alikuwa haelewi.

Nilichofanya nilimbeba nikaondoka nae nikamrudisha nyumbani nikampeleka ndani bado analia anaomba msamaha anatamka kila neno unalolijua wewe hapa duniani.

-nikamake sure ameingia ndani ilikuwa usiku kidogo me nikaondoka zangu nikaenda sehem kuna baa nikapaki gari nikalaza kiti nikawa natafakari tu peke yangu.

-akaanza kunipigia simu sikupokea missed call kibao me nikamute simu, badae dada ake huo usiku nae akawa nanipigia me sikupokea simu badae nikaizima.

-Nilikaa pale nje hadi kukakucha nikarud zangu nyumbani nikakuta ameondoka na mtoto ameenda kwa dada yake pale wamemuacha dada wa kazi,nilivyofika nadhan aliwaambia badae kidogo wakaja na dada yake



Itaendelea …….
Hahaha
 
Back
Top Bottom