The Voices From Within: "Mahakamani Watashindwa Tena!" Sababu ni Mawakili! Jee Tanzania Tuna Mawakili wa Calibre ya Murtaza Lakha?Jitokezeni Kusaidia!

Mimi sio wakili, mimi ni Mwandishi tuu wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, na amini usiamini hivi ninavyo wasaidia humu jf ni msaada mkubwa sana!.
P
Ushauri : Pascal Mayalla kwa uwezo na uzoefu wako wa uchambuzi na uandishi ukichanganya na elimu yako ya sheria , huoni ipo haja ya kuanzisha taasisi yako ya ushauri wa kisheria?

Ili watu kama akina Halima wangekuja kupata ushauri kabla ya kukurupuka kwenda kufungua jalada la kesi ambayo kwa jicho lako la kibobezi tayari washashindwa hata kabla ya kusikilizwa.
 
Mkuu Sexless, hili neno!..
Asante
P
 
Pascal Mayalla

1976 kulikuwa na DSO,RSO? Ebu fafanua kidogo
 

Naona unajifanya kunipaka mafuta kwa mgongo wa chupa, kuwa nachangia post zako with objectivity ili uonekane mstaarabu, mimi sio wa sifa nyepesi za hivyo bro. Sifa za hivyo wape wasiojitambua.

Huyo Murtaza Lakha unayesema alikuwa bora, ni kwakuwa enzi hizo mahakama zilikuwa hazijaingizwa siasa chafu kama sasa. Kadiri CCM inavyozidi kukaa madarakani kwa shuruti, ndivyo Mihimili ya mahakama na bunge inavyozidi kupoteza uwezo wake.

Ushahidi uliokuwa unatolewa kwenye kesi ya Mbowe, na maamuzi ya mahakama pale ndio nilijua hatuna tena mahakama, bali majengo ya mahakama yanayosimamiwa na Makada wa CCM. Kama pamoja na huo unaosema uwezo wako hujafanikiwa kuona ombwe hilo la mifumo yetu ya kiutawala na mihimili yake, basi kazi iko. Hayo maelezo yako mengine yote ni porojo as usual.
 
Eti hawakutendewa haki!
Kwa hiyo wewe ni mahakama inayoamua mwenye haki?
 

Mbowe kakutwa na kesi ya kujibu kwakuwa mahakama zilikuwa zinachukua maagizo huko ikulu. Kwa mahakama zilizo huru, ule upuuzi usingepata nafasi. Kwakuwa ww ni muumini wa siasa chafu, ni haki yako kuamini ule uhayawani uliokuwa ukiendelea mahakamani.
 
Pascal na kujiita kwake muandishi nguli ila ukimuuliza "ubatili wa maamuzi ya kamati kuu" ni upi kwa mujibu wa katiba ya CDM atabaki kimya kama vile anakunbukia kile kitendo 'fiche' alichofanywa na paroko enzi akiwa anatumikia kanisani.
 
Pascal Mayalla

1976 kulikuwa na DSO,RSO? Ebu fafanua kidogo
Mkuu Liga Lugano5 Hierarchy ya mabosi wa mkoa kiusalama ni
  1. RC - Regional Commissioner
  2. RSO- Regional Security Officer
  3. RPC- Regional Police Commander
  4. DSO - District Security Officer
  5. OCD- Officer in Charge of District
Kosa lao kuna watuhumiwa wawili wa mauaji ya vikongwe Mwanza, walikufa mikononi mwa polisi baada ya mahojiano eneo la Kigoto huko Mwanza

Watuhumiwa hao ni Masanja Makhulla Mazengenuka na Issac Mwana Mkoboko.

Kosa la Mzee wangu ni huruma iliponza Kwa kuwaonea huruma kwenye kuhojiwa, akasimamisha zoezi, polisi wakamgomea, akawabeba kwenye gari yake kuwapeleka Bugando, wakiwa njiani wakamweleza mzee hawajala chochote for 3 days hata tone la maji!. Akawapitisha kwenye kihoteli fulani na kuwanunulia soda coke, kumbe kosa!. Walishindwa kushuka kwenye gari ya mzee, wakapelekewa soda kwenye gari. Walipokunywa zile soda walipomeza tuu fundo la kwanza, walitapika damu naku faint.

Mzee akawakimbiza Bugando kule wakakataliwa kupokelewa bila PF3, hata baada ya Mzee kuwaeleza who he is bado walimgomea, akampandia kwa simu (gari ina simu kama ya mezani na Radio Call) Mkurugenzi wa Bugando, Dr. Nkulila ndipo wakapolewa, the next day they were both dead!.

Kumbe kuna a special arrangements za polisi na government hospitals, vifo vyote vya mikononi mwa polisi vinaandaliwa two post mortem Reports, the real one, and the official version. The real one ilisimamiwa na Mkurugenzi Mkuu mwenyewe Dr. Nkulila na Mzee alikuwepo, polisi wakagoma kuhudhuria.

Kisha polisi wakatoa maelekezo ya the official one ionekane watuhumiwa wamekufa kwa a lethal poison iliwekwa kwenye soda, polisi wana ushahidi!.

Mzee akageuziwa kibao kuwa aliwazuia polisi kutimiza wajibu wao na kuzuia watuhumiwa hao wasihojiwe, kisha aliwachukua mahabusu kwa nguvu na kinyume cha sheria kutoka mikononi mwa polisi bila remove order na kwenda nao uraiani kwenye starehe hotelini ndipo akawatilia sumu kwenye soda, hizi soda ni Mzee ndio aliwapa polisi, hivyo polisi walizitia sumu kwanza ndipo zikapelekwa kwa mkemia Mkuu wa Serikali.

Polisi wakakana kufanya mahojiano yoyote na watu hao!.
Mzee ndio alituhumiwa kuwaponza, kila siku watuhumiwa kibao wanakufa mikononi mwa polisi and issues zinakwishwa kimya kimya. Kama Mzee asingewaokoa wale watuhumiwa mikononi mwa polisi, they were both left to die na taarifa ya Polisi ingesema natural death, na kukikabidhi tuu miili mortuary and it would end up there.

Wema na huruma ya mtu mmoja, imelichafua jeshi letu safi la polisi.

Wakili Murtaza Lakha akamshauri Mzee aseme only the truth and it's only the truth will set you free. He did na kusema kila kitu, and that he as a government official was part and parcel ya mahojiano hayo but he as human being, was not a part ya mbinu zilizotumiwa. He was the only one set free!.

Ndio maana mimi naumia sana kila nikisikia kifo chochote mikononi mwa polisi because I know the games people plays
  1. , Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa!, Polisi Wako Ni Wauaji!. P'se Stop This,
  2. IGP Kamanda Sirro, Usiruhusu Vifo Vya Uzembe Kama Huu Kuchafua Jeshi Letu Safi la Polisi!.,
  3. Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know!,
  4. IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality!. Utampeleka JK The Hague-Part II!,
  5. Ombi Muhimu Kwa Jeshi Letu La Polisi."Nyinyi ni Wenzetu, September Mosi, Please Msigeuke Makaburu!".,
  6. Wito Jeshi Letu la Polisi, Stop This Sensesionalism!. Udhalilishaji, na Kuingilia The Right to Privacy!. Kumbe PT Inafanyia Kazi Taarifa za Mitandao!,
  7. Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?,
  8. Jaji Mkuu na Mahakama, Kemeeni Tabia Ya Jeshi la Polisi Kujigeuza Mahakama na Kuhukumu Watuhumiwa kwa Kutumia Media
  9. Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.
  10. Pongezi Jeshi la Polisi. Japo Nabii hakubaliki nyumbani, Jeshi sasa ni Sikivu, Most friendly na very hospitable
  11. Jeshi la polisi likifanya vyema, lipongezwe, hongera FFU kusambaratisha maandamano bila virungu, mabomu ya machozi, risasi za moto, bila maafa!
P
 
Wewe kila siku unajinasibu hapa umesomea sheria na Betina alikuwa Mwl wako UDSM,huu ndiyo ulikuwa muda wako muafaka wa kuonyesha kile ulichopata UDSM kwa kuwatetea hawa COViD 19.

Alf suala la Karma kuna jamaa aliwahi kukuita njaa, aliondoka akaiacha Chadema, sasa usipende sana kutumia hilo neno.
Sasa hii Karma ni kwa Chadema tu.
 
Hivi ni umri umekufanya akili kudumaa au ni nini
Wewe ni mwanasheria kwanini usijitokeze kuwasaidia.
Hivi wewe si CCM ya chadema yanakuwasha nini


Sasa umepiga U TURN na kuanza kusema watashindwa tena


Paskali paskali paskali.
Nakuita paskali[emoji849][emoji849][emoji849]
 
Acha kuwadhalilisha wanasheria wenzako
No sijadhalilisha mwanasheria yoyote, japo kazi kutunga sheria ni kazi ya Mhimili wa Bunge, mahakama pia inatunga sheria kwa maamuzi yake mbalimbali yanayoitwa presedents, jinsi Halima Mdee alivyotinuliwa Chadema ni jinsi hiyo hiyo alivyotimuliwa Zitto, CC ya Chadema haina mamlaka ya kumvua uanachama NKM au Mwenyekiti wa Bawacha. Hivyo Zitto hakutendewa haki, akafile kesi kwa makosa, ikatupwa!. Tulitegemea Mdee ambaye ni mwanasheria kutumia more competent Lawyers ambao watatumia precedence ya hukumu ya Zitto kutorudia makosa!.
P
 
Paskali zimemtoka baada ya mjombake mwendazake kwenda zake
 
Uko sahihi mkuu.

Viwango duni.

Ila sikutaka kusema hayo maana wale wanabiashara na wanawateja.

Nahisi si suala la viwango vya Mawakili wao bali haki.

Ikiwa hapakuwepo kikao cha kuwapitisha.
Hakuna barua au form rasmi ya kupeleka majina yao mjengoni.

Taasisi zote mbili yaani Bunge na NEC hawana documents rasmi na halali za kuthibisha uhalali wa ubunge wao !.

Labda Nabii & Mtume Geodav angeweza kuwasaidia si uhodari wa mawakili.

Haki uinua Taifa.
 
Wewe kila siku unajinasibu hapa umesomea sheria na Betina alikuwa Mwl wako UDSM,huu ndiyo ulikuwa muda wako muafaka wa kuonyesha kile ulichopata UDSM kwa kuwatetea hawa COViD 19.
Japo nimesoma sheria lakini mimi sio wakili, mimi ni Mwandishi tuu wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, huku tuu ninakoandika humu na magazetini ni msaada tosha
Alf suala la Karma kuna jamaa aliwahi kukuita njaa, aliondoka akaiacha Chadema,
Jee unajua huyo jamaa yangu aliondoshwa na nini?. Karma is real!.
sasa usipende sana kutumia hilo neno.
Sasa hii Karma ni kwa Chadema tu.
Karma sio kwa Chadema only, kuna karma za aina nyingi kuna institutional karma ambayo inakitandika chama na kuna individual karma inayowatandika viongozi wake individually.

Sio Chadema tuu, hizi hapa ni karma mbalimbali za vyama na Viongozi.
  1. Bora Katiba tuikubali, tusiichukie CCM kwa sababu CCM itahukumiwa na Karma kwa Uovu wake
  2. Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!
  3. Tuacheni ramli chonganishi: Tusihukumu tusije tukahukumiwa. Karma ndio pekee hutoa hukumu ya haki hapa duniani!
  4. Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!
  5. Angalizo kwa Wanasiasa hamahama; Japo ni haki yenu lakini msisahau fadhila. Kuweni watu wa shukrani, mtabarikiwa sana, vinginevyo karma Itawahusu!
  6. Membe, Japo Umeonewa, Usifanye Kosa la Lowassa!, Ila CCM ya Ajabu!, Uamuzi based on Illegal Evidence ni Void Ab Initial!.
  7. Wito Kwa Zitto , Maalim Seif, na ACT, Please Don't Loot Mali Halali za CUF!, Msifanye Kama CCM Iliyowafanyia Watanzania, Zitawaletea Laana ya Karma.
  8. Kama tuhuma hii ni kweli, then this is The End of Zitto. Karma Ndio Itamaliza Kila Kitu!
  9. Opinion: Kung'atuka Kwa Zitto, CHADEMA, Msishangilie, Mkajisahau, Jiandaeni kwa "Karma!"
  10. Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu
P
 

Bila shaka Wewe ndio mbulula wa viwango vya SGR.

Kesi yote ya Mbowe ingekuwa na mashiko iwapo Lt Urio angeweza kuithibitia Mahakama pasipo shaka ushiriki wa Mbowe katika kupanga ugaidi.

ACP Kingai ndio aliharibu kila kitu.Kifupi Jaji Kiongozi alishindwa kuimaliza kesi mapema kwakuwa alihongwa cheo na Serekali.

Majaji wote hasa aliyempokea Jaji Kiongozi walionyesha upendeleo wa wazi.Kadri kesi ilivyo endelea Jamhuri walizidi kujichosha kwa kuendeleo na kesi ambayo haikuwepo.
 
Hatujui cha Murtaza wala nani! Unashindwaje kusema mawakili wa calbre ya Kibatala?! Ungetakiwa umalize unafiki ujanani, saa hizi ungekuwa mchawi, Pasco! Karma ni kwa aliye sababisha uchafuzi, yakapatikana haya mazao yaitwayo covid-19, na wafuasi wake wote, wewe ukiwa mmojawao, Kangaruu jike!
 
Mkuu Paskali, nilikuwa nje ya DSM ndiyo naweza ku comment sasa baada ya kutulia.
Inaelekea una some sort of personal attraction to Mdee and the 18.
Tatizo lililopo kisheria ni jinsi Mdee and the 18, walivyofika pale walipo.
Sasa mwanasheria anayeweza kutetea forgery ya nyaraka zilizowakilishwa bungeni kwa Ndugai, naye akazikubali, huyo mwanasheria atakuwa kiboko.

Kwa jinsi ndugu yangu Paskali unavyoliweka syala inaelekea ume kuwa subjective, na siyo objective.
 

Hili nalo neno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…