Nakwambia hivi viongozi wengi wa kiafrika wanafaidika sana na hii COVID19, tena kuna wengine wanaomba labda isiishe kwani ni sehemu ya kupiga pesa kutoka kwa mabeberu, na kuzifanyia mambo mengine tu, ila wananchi ndio wanaumia!!ukiangalia , vipimo unalipia, gesi unalipia, mask mnanunua, sanitizer, hivyo hivyo, hayo mabilioni yanatumika wapi?mfano uganda nako mtu akilazwa siku moja tu karibia dola 1000!!!hospitali binafsi, anaulizwa waziri anasema" jamani tusiumizane hivyo sisi wote ni Waganda"wao wanachowaza ni kushindana kwa kutoa takwimu tu za vifo na maambukizi ili mpunga uzidi kuingia tu!!mfano mzuri hapa kwetu yale mabilioni ya IMF, kipindi kile ndio imeanza, huku taasisi kibao binafsi zikawa zinachangia kila leo mabilioni, na vifaa tiba, lakini kwenda kupima corona ulikuwa unachajiwa pesa!!!