Binafsi, nilibahatika kukutana na msanii wa kike wa kurap aliyewahi kutamba enzi hizo (jina nalisitiri), maana alihamia kwa muda jirani na nyumba niliyokuwa naishi last year. She is too talkative, na ni aina fulani ya watu ambao ni rahisi sana kuzoeana nao, so tulizoeana na nilifanikiwa kumuuliza masuala flani flani hivi kuhusu Muziki na wasanii...
Katika maelezo ya bidada huyu, alisema wasanii wengi wanatumia ngada. Wengi sana. Na alisema muda ukifika tutawaona dhahiri. Nikamuuliza kwani wewe hujawahi kushtua? Akakataa kata kata, akadai yeye ana vitu vyake tu, ila ngada anaiheshimu kupindukia, anaiogopa kama Ukoma!
Hakuishia hapo, alisema wengi pia ni waathirika wa HIV, na alinitajia mpaka majina (nayahifadhi), na akasema muda ukifika kila kigawe lazima kitaguswa. Alikuwa akisisitiza Muda tu. Kwamba kila kitu kitakuwa wazi muda ukifika!
Kuhusu TID pia nilimuuliza...Hakunijibu, lakini akasema 'Kinondoni haifai'.. Alinitolea mifano mingi na ushahidi mwingi kuhusu wasanii wa Kinondoni coz yeye mwenyewe alitokea huko. Alitaja historia na matukio. Aliwataja mpaka wanasiasa wakubwa na wafanyabiashara wakubwa wenye majina (huwezi kuamini) ambao wamechangia kwa kiwango kikubwa kuwaharibu wasanii..
Itoshe!