Timu ya Taifa ya wanawake ni tishio

BETONY

Senior Member
Joined
Apr 4, 2012
Posts
188
Reaction score
170
Katika michuano inayoendelea sasa hivi ya CECAFA SENIOR WOMEN CHAMPIONSHIP, Kilimanjaro Queen's imekuwa na muunganiko mzuri. Ukiwa unaiangalia timu hii unaona ule muunganiko mzuri.

Pia unaona usahihi wa pasi ambapo mara nyingi timu zetu zimekuwa zinapata shida.

Kuanzia golini mpaka bench la ufundi unaona muunganiko huo.

Mpaka sasa wachezaji waliotia fora ni Donisia, Double Aisha,Amina na kule nyuma ni balaaa. Mwalimu na benchi zima la ufundi wanastahili pongezi.

Pia timu nzima imekuwa ni nzuri sana. Mungu awasaidie wabakishe kombe nyumbani.

Mungu ibariki The Kilimanjaro Queens. Mungu ibariki Tanzania
 
Pale Mbele kuna makosa madogo madogo
Ila wapo Vizuri
Ndio mkuu. Timu inatengeneza nafasi nyingi. Bado Opa na Mwanahamisi hawajaweza kucheza pamoja. Ngoja tuone mwalimu atatoka vipi katika mechi zijazo
 
Tuki-invest hawa mabinti watatuwakilisha vyema sana kimataifa shida tupo kwa wale vijeba kwa sababu ya mazoea tu...

D.Minja pekee anauwezo mkubwa wa kufanya maamuzi kuliko strikers wa stars
Huyo Double D ni noma
Pale kati sasa wale kina double asha na amina kama wamezaliwa nao mpira
 
Wanajitahidi,nadhani Zanzibar watakula 15 labda wawaone huruma tu kulinda muungano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…