Timu ya Taifa ya wanawake ni tishio

Timu ya Taifa ya wanawake ni tishio

Kumbuka walimkanyaga Zambia 2-1 wakachukua ndoo ya COSAFA mwanzoni mwaka huu. Kwasasa tuna timu nzuri ya wanawake. Hao Nigeria, Cameroon na Senegal wajipange kweli kweli siku wakikutana na hii timu.
Tunataka mafanikio ya kueleweka bana kama wanajua wafuzu hata world cup ya tuone.
 
Kama vipi Waigeuze hiyo ndio iwe Taifa stars sasa [emoji16][emoji16][emoji16].
 
Tuki-invest hawa mabinti watatuwakilisha vyema sana kimataifa shida tupo kwa wale vijeba kwa sababu ya mazoea tu...

D.Minja pekee anauwezo mkubwa wa kufanya maamuzi kuliko strikers wa stars
Huyu binti anacheza vizuri wing ya kushoto, tatizo ni kua akishawapunguza kule hupenda kupiga krosi zisizo na macho. Yaan hupiga tu krosi kati bila kujua anampigia nani
 
tunawafunga wabovu wenzetu sema kwa afrika mashariki hakuna atakaetufunga ila bado hatuna timu bora ukitaka kujua tuna timu ya kawaida kafatilie ile game ya USA NA FRANCE world cup ya wanawake alafu anagalia game za tanzania
 
Asante sana mkuu kwa hii taarifa muhimu sana kwa sisi wadau nguli wa soccer ngoja nimualike mama soccer Shadeeya
Nimekuja Best.

Jana nilifanikiwa kuiona mechi yao na Burundi wako vizuri japo yule Mwanamisi ana kauchoyo fulani sa sijui ndio uchu wa kutaka awe na mabao mengi mana waeza kuta sehemu ya kutoa pasi mwenzake ascore basi atataka kumpiga chenga kipa mwishowe hamna anachoambulia.

Yule Donisia yuko vizuri na ni mwepesi katika kufanya maamuzi yaliyo sahihi.
 
Nimekuja Best.

Jana nilifanikiwa kuiona mechi yao na Burundi wako vizuri japo yule Mwanamisi ana kauchoyo fulani sa sijui ndio uchu wa kutaka awe na mabao mengi mana waeza kuta sehemu ya kutoa pasi mwenzake ascore basi atataka kumpiga chenga kipa mwishowe hamna anachoambulia.

Yule Donisia yuko vizuri na ni mwepesi katika kufanya maamuzi yaliyo sahihi.

Daa hukuniita! Japo nilikuwa very tight yet kesho nitajitahidi.
 
tunawafunga wabovu wenzetu sema kwa afrika mashariki hakuna atakaetufunga ila bado hatuna timu bora ukitaka kujua tuna timu ya kawaida kafatilie ile game ya USA NA FRANCE world cup ya wanawake alafu anagalia game za tanzania
USA na FRANCE ni habari nyingine, lakini kwa hapa Afrika hawa Twiga Stars/Tanzania Queens wako vizuri.
 
Hii timu haina mpinzani ukanda huu wa Afrika mashariki napendekeza ipelekwe Afrika Magharibi kule itapata washindani wa kueleweka.
 
Back
Top Bottom