Wasalaam wanabodi,
Mimi kama Mwanachama mtiifu wa club ya Simba SC, naishauri club yangu pamoja na harakati za kunyakua ubingwa wa Ligi kuu Tanzania bara, Uongozi uitishe harambee ya kuzikomboa hizo nyasi Bandarini.
Pamoja na ukweli kwamba club nyingi za soka zipo hoi kiuchumi lakini tukumbuke club ina mtaji wa mashabiki ambao wapo tayari kujitoa kwa hali na mali kuona timu inasonga mbele.
Tukiziacha nyasi hizi zikapigwa mnada tutakuwa tumepiga hatua moja kurudi nyuma na ndoto za Kumiliki Simba SC Complex zitakuwa zimefifia.
Naamini club ya Simba inaongozwa na watu wabunifu, wazoefu na wenye ueledi wa kutosha kuweza kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kama hizi. Kuandaa harambee itakuwa rahisi zaidi kuliko club kujitutumua kulipa deni wenyewe.
Ni matumaini yangu mtaufanyia kazi ushauri huu.
Mimi kama Mwanachama mtiifu wa club ya Simba SC, naishauri club yangu pamoja na harakati za kunyakua ubingwa wa Ligi kuu Tanzania bara, Uongozi uitishe harambee ya kuzikomboa hizo nyasi Bandarini.
Pamoja na ukweli kwamba club nyingi za soka zipo hoi kiuchumi lakini tukumbuke club ina mtaji wa mashabiki ambao wapo tayari kujitoa kwa hali na mali kuona timu inasonga mbele.
Tukiziacha nyasi hizi zikapigwa mnada tutakuwa tumepiga hatua moja kurudi nyuma na ndoto za Kumiliki Simba SC Complex zitakuwa zimefifia.
Naamini club ya Simba inaongozwa na watu wabunifu, wazoefu na wenye ueledi wa kutosha kuweza kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kama hizi. Kuandaa harambee itakuwa rahisi zaidi kuliko club kujitutumua kulipa deni wenyewe.
Ni matumaini yangu mtaufanyia kazi ushauri huu.
Simba Nguvu Moja