Nianze ni hilo ka Wema kwamba cku moja moja huwa wananiambukiza... mie siku zote kutokana na mazingira hivyo hawezi mtu yeyote kuniambukiza mtazamo wake! Sina hakika kama ni wewe au Heaven on Earth, nilishawahi kusema mtazamo wangu kwa Wema upo vipi! Kama si wewe, basi ningependa nirudie tena hapa! Sina sababu ya kumpenda Wema wala kumchukia... WHY? Wengi wanampenda Wema kupitia kazi zake za filamu... kwa bahati mbaya, hata leo hii ukiniuliza Wema amecheza filamu gani, sina jibu coz' huwa siangaliagi hizi movie zetu! Aidha, nilisema wazi kwamba, pamoja na yote bado niliipenda couple ya Wema na Chibu!
Na kwa upande mwingine, sina sababu za kumchukia coz', kwa tabia yangu huwa sipendi kuingilia personal life ya yeyote. Home wananiambia nitakuja kuwa mlezi mbaya... I agree with them; manake am certain, hata nikiwa na my own kids, akishafikia umri wa mtu mzima, nitakuwa nimeshanawa mikono! Na mie hapa home ndie kimbelembele wa kuwa-criticize madingi pindi ninapoona wanataka ku-influence maisha ya wadogo zangu ingawaje wengi wao ni wakubwa tayari! Kutokana na hii tabia yangu ya kutopenda kuingilia personal life ya yeyote, utakuta ni ngumu sana kuwa na chuki na mtu hususani hawa ninaoishia kuwaona kwenye TV! Hata kwenye jamvi hili hili si mara moja wala mara mbili nimeshapata kuwahoji wanaosema kwamba Wema ni malaya wao wamemtia mara ngapi au kama umalaya wanaomtangazia ni huu a kuishia kusikia kwenye media za udaku! That's how I am my dear kwahiyo usidhani huwa naambukizwa bali ukiona namponda basi amefanya jambo ambalo anastahili kupondwa na sio personal issue! Kwa hili, hata huyu Diamond ambae huwa namshabikia nilijitokeza wazi wazi kulaani kitendo chake cha kukurupuka kumjibu Davido kabla hajakuwa na uhakika Davido alimaanisha nini... again, that's how i am! It's out of topic but it serves to tell what kind of person I am! Mimi ni Mwislam... huyu
Matola tumesuguana sana enzi hizo kwenye mijadala ya kidini hadi pale tulipojiona kumbe sisi ni wajinga! Lakini pamoja na Uislamu wangu huo, nilijitokeza wazi wazi kumponda Sheikh ILunga (kama uliisikia hii issue) hadi watu ninaowaheshimu wakaniita mimi ni Kafir lakini nikasema heri kuwa kafiri kuliko kutetea upumbavu... that's how I am my dear! Pamoja na Uislamu wangu huo huo, hapa hapa JF niliwahi kusema kwamba kama kweli kuna kitu kinachoitwa Mungu na dini zake basi dini hiyo haiwezi kuwa Uislamu wala Ukristo... that's how i am my dear... kule jukwaa la siasa sina rafiki wa kudumu coz' leo hii wana-CHADEMA wataniita Gamba na kuniambia niende kwa akina Ritz lakini kesho nitacheka nao baada ya kuona nimemponda mwana CCM... Kwenye signature yangu ya nyuma, nilianza maneno "am a free thinker....!"mwisho nikamalizia "If today we
agree with cheers, tomorrow we'd not
disagree with jeers!" Coz', that's how I am my dear...
Hili la watoto na kwamba wapo very vulnerable... wow! it sounds good and beautiful but let's be honest my dear! Hivi hawa watoto tunawahurumia leo baada ya Zari kuwa na Diamond kuliko zamani ambapo walikuwa ni wadogo zaidi as compared to sasa?! Is it all because of these innocent kids? Kama kweli tunawahurumia watoto ni kwanini tunaongoza kutaja mambo machafu ya mama yao? Tell me somethin' MBN... naamua kusimama bega kwa bega na wewe kwa ajili ya kutetea dhidi ya mama yako lakini katika kukutetea huko kazi yangu kubwa na kumchana mama yako mzazi na kutaja all bad things about her... will you really love me na kuniona mtetezi wako? Hivi wale watoto wangekuwa na uwezo wa kuingia JF wangeyajua mangapi ya kuumiza na kuchukiza kuhusu mama yao toka kwa watu wanaosema wana uchungu na watoto? Tungekuwa na huruma na watoto tungehangaika ku-post picha chafu za mama yao huku tukijua kwamba itawaumiza zaidi kuona mtu ana-post picha chafu za mama yao kuliko hilo suala la kuwa na Diamond? Let's not use these small kids as our armors! There's something else lakini sio watoto...
Hilo la IG, am very sorry for that... na ndio maana mie hadi leo sipo IG hasa baada ya kuona kinachoendelea IG ni upuuzi zaidi kuliko facebook!
Kuhusu facts about Zari... hakuna yeyote mwenye uwezo wa kuleta facts zaidi ya zile anazosema mwenyewe! Ni Zari pekee ndie mwenye uwezo wa kuleta Birth Certificate inayoonesha she's 35 (hata kama she's 40) lakini hakuna wa kuleta birth certificate inayoonesha Zari is 40 hata kama kweli she's 40! Hakuna mwenye facts za kuthibitisha kwamba Zari na watoto zaidi ya watatu hata kama ni kweli zaidi ya yeye mwenyewe kuwa na uwezo wa kuthibitisha kwamba ana watoto watatu tu! Mengine tunayoambiwa kwamba ni facts ni Zari kulala na wanaume zaidi ya 50 lakini list inayotolewa kila siku ni ile ile iliyozoeleka ambayo, si tu kwamba haiwezi kuthibitisha chochote kwamba hao ndio amelala nao lakini list yenyewe hata hiyo 50 haijakaribia!
Hapo ulipomalizia kwamba "
Otherwise u r still my friend..." umekosea bhana, ungemalizia na "and i love you too...!"