TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14

Napinga mwongozo huu uliotolewa na TLS, ingawa mimi si mwanasheria nahisi wameisoma hiyo katiba kwa kuharakisha, na wana bias....
Hawana ubavu wa kukutupia mawe!! Sana Sana wanatafuta mahali pa kuficha nyuso zao!! Umewapiga ngumi puani!!
 
Hiyo ni katiba ya CHADEMA hata kama mawaziri wakibadilishwa bado ni wale wale kutoka chama kitukufu cha C C M Nendeni mkagombee Kenya kuna uchaguzi mwakani na demokrasia ya kumwaga mkishindwa sana Lissu atapata u-Governor wa Nairobi
 
19 March 2021
Mh. Rais Samia Suluhu Hassan azungumzia kipindi cha mpito kufuatia kifo cha Rais John Pombe Magufuli, Na kutoa shukrani kwa mihimili ya Mahakama, Bunge na serikali kupitia Kassim Majaliwa Majaliwa kwa kufanya kazi kwa Umoja.

 
Wanadhani mama hajui hayo au ndio wanataka kuanza kumpreshalaizi bimkubwa.
 
Kama nimeelewa vizuri kana kwamba kwa sasa hatuna Waziri Mkuu wala Baraza la Mawaziri! Naomba kusahihishwa tafadhali
1) katika hotuba yake fupi baada ya kuapishwa, Rais SS alim address kassimu kama waziri Mkuu.
2) Baada ya hotuba hiyo alienda kuongoza kikao cha Baraza la mawaziri
 
Mfano akigoma Raisi kuunda baraza jipya TLS watamfanya nini cha maana
 
Kisheria hakupaswa kufanya hivyo maana hana Waziri Mkuu wala mawaziri. Hata makamu wa rais hana kwa sasa!
1) katika hotuba yake fupi baada ya kuapishwa, Rais SS alim address kassimu kama waziri Mkuu.
2) Baada ya hotuba hiyo alienda kuongoza kikao cha Baraza la mawaziri
 
Wamevunja katiba waziwazi wapi?

Katiba inasema endapo Rais aliyepo madarakani anakoma kuwa Rais basi na baraza la mawaziri nalo linavunjika papo hapo?

Kwa kumbukumbu zangu, waziri mkuu akibadilishwa, au akijiuzulu, baraza la mawaziri linavunjika.

Miimi i am learning kwenye kuamini kwamba kukitokea mabadiliko ktk nafasi ya Raisi basi baraza nalo linakuwa limevunjika.

Lakini kwa upande mwingine nahisi nchi hii haiendeshwi kwa katiba, bali vile ccm wanavyojisikia kufanya kwa wakati husika.
 

..Nimeona hata kwenye gwaride askari walikurupushwa wakajipanga harakaharaka wakati Raisi mpya anaelekea kwenye jukwaa la kupokea heshima.

..Pia wakati Raisi mpya anapokea heshima toka kwa askari kukawa kuna magari yanapita nyuma ya jukwaa aliposimama Raisi.

..kwa kweli kulikuwa na vuruguvurugu nyingi ambazo kwa uzoefu wangu hazipaswi kuvumiliwa hata kidogo.
 
Ukishasema hii ni serikali ya awamu ya 6 ina maana kuna mabadiliko ya serikali uliyoikuta. Ukirndeleza serikali ileile bila kuivunja inaonekana bado una kaimu Nafasi ya urais uliyemkuta....
Fatma karume anasema inatakiwa aanze kwanza kumteua mwansheria mkuu.
 
Fatma karume anasema inatakiwa aanze kwanza kumteua mwansheria mkuu.

..nadhani AG huwa anateuliwa kwasababu bunge linakuwa jipya, na siyo kwasababu Raisi ni mpya.

..kwa mfano, Raisi Magufuli alimteua Prof.Kilangi kuwa AG mwezi Nov 2020 kwasababu bunge jipya lilikuwa linaanza.

cc PTER
 
ngoja, mpewe chanjo mtatulia tu, mtakua wapole. mnajidai wajuaji sana
 
Kwenu TLS hongereni sana kwa Kutoa Muongozo hivi na Kutuelimisha pia Sisi Mangumbaru wengine wa Kisheria.

Kwa maana hiyo ( hii ) ni kwamba sasa hatuna Premier wala Cabinet Ministers. Ila kama TLS mpo sahihi hivi Kisheria na bahati nzuri hata Rais Samia Suluhu Hassan Kitaaluma ni Mwanasheria ( kama nilivyodokezwa ) ilikuwaje tena Jana baada tu ya Kuapishwa akafanya Kikao chake cha Kwanza na Baraza la Mawaziri?

Hata hivyo kama TLS mpo sahihi kwa hili na Mabadiliko Kufanyika nitakuwa ni mwenye Furaha kwani najua Wapuuzi na Wanafiki kama akina Majaliwa na Nchemba pamoja na wale waliopata hiyo Nafasi kwa Upendeleo wa Kulipa Fadhila kwa Baba zao waliokuwepo Madarakani katika Tawala zilizopita hawatorudi tena na kama ikitokea wote wakarudi nitaamini kuwa duniani kote Waganga wa Kienyeji wazuri wanatoka Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…