Mnamo tarehe 19 Machi 2021, aliyekuwa Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, aliapishwa kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, kufuatia kifo cha Raisi Dr. John Pombe Joseph Magufuli. Kuapishwa kwake kunaibua suala la msingi la kikatiba juu ya kuendelea au kutoendelea kuwapo kwa Baraza la Mawaziri lililoteuliwa na Hayati Raisi John Magufuli.....
Huu ni upotoshaji uliolenga kitu fulani.
1. Eti rais anapofariki au anaposhindwa kumudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili, baraza la mawaziri linakuwa limevunjika na hivyo makamu wa rais baada ya kuapishwa kuwa rais anawajibika kuunda baraza la mawaziri jipya!
Hii ni kinyume kabisa na katiba. Rais akifariki baraza la mawaziri ambalo alikuwa akiliongoza halivunjiki bali linashikamana zaidi. Makamu wa rais ni miongoni mwa baraza hilo na ataapishwa kwa mjibu wa katiba kuchukua nafasi hiyo ya kuliongoza baraza hilo kwa kipindi kilichobakia.
Rais anaposhindwa kumudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili baraza la mawaziri halivunjiki bali linashikamana zaidi na ndilo linaanzisha mchakato wa makamu wa rais kupewa kiti hicho kwa kumuarifu jaji mkuu ili aunde jopo la madaktari kuthibitisha lililomtokea rais ili hatimaye makamu wa rais aapishwe kumalizia kipindi kilichobakia.
Hivyo katiba iko wazi kabisa kwamba makamu wa rais ataapishwa kuwa rais kumalizia kipindi kilichobakia. Kipindi kilichobakia kinaweza kuwa cha siku chake au miezi fulani au miaka fulani. Ni kipindi kilichobakia kwenye awamu hiyo. Hatuanzishi awamu nyingine. Kuna wengine wanafikiri kwamba sasa tunaanza awamu ya sita, si kweli hata kidogo. Bado tunaendelea na awamu ya tano ya hapa kazi tu hadi 2025.
2. Tusichanganye na masuala ya rais kuondolewa madarakani kwa impeachment au kujiuzuru. Haya utaratibu wake wa kikatiba nao uko wazi. Hapa ndipo bunge lote pamoja na baraza la mawaziri linavunjika. Kinachofuata ni uchaguzi mkuu mpya kupata serikali mpya na bunge jipya.
3. TLS kutoa miongozo kwa serikali, haya madaraka wameyatoa wapi? Halafu miongozo yenyewe kwa serikali inatolewa hadharani. Hapa kunatia wasi wasi wa alichokipandikiza Tundu Lissu pale TLS.
TLS kama tasisi zingine zinaruhusiwa kutoa ushauri kwa serikali kuhusiana na mambo mbali yanayohusu taifa letu. Lakini kwa kawaida ushauri makini huwa una utaratibu wake wa namna ya kuutoa kwa serikali, na kwa kawida huwa umeombwa.