TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14

Inasemekana watanzania huwa wanasoma lakini hawaelimiki

Yani kusoma na kuelimika ni vitu viwili tofauti ndio haya tunayo yaona ya TLS
 
Safi sana TLS kwa mwongozo, nina imani Mh. Rais Samia atafanya mabadiliko kadhaa ndai ya baraza lake jipya ili kuleta msawazo wa mawaziri kwa kuzingatia jinsia,dini,kaila, mikoa na bila kusahau Muungano wetu na ndugu zetu wazanzibar!
Inakosa maana baraza la mawaziri kuwa kujaza watu wa kutoka kabila moja au kanda moja au kujaza watanganyika watupu wakati baraza hilo linaitwa la Jamhuri ya Muungano!
 
KWA NCHI INAYOFUATA KATIBA TLS WAPO SAWA. LAKINI TUJIULIZE, JE, KATIBA BADO INA NAFASI NCHINI MWETU? KWA MIAKA 5 SASA KATIBA NA MIONGOZO MINGINE YA KISHERIA ILITUPWA JALALANI, MTU MMOJA AKAWA NDIYE KATIBA NA NDIYE SHERIA. HII IMETUATHIRI SANA NA KUWA SASA NI KAWAIDA KUVUNJA KATIBA. ANGALIA YAFUATAYO:
1. KATIBA INAAGIZA RAIS AKIUGUA WANANCHI WALIOMCHAGUA NA KUMWAJIRI WAAMBIWE. HILO HALIKUFANYIKA, BADALA YAKE TUKADANGANYWA KWAMBA NI MZIMA WA AFYA NA ANACHAPA KAZI. KWA KOSA HILI KATIKA NCHI INAYOFUATA UTAWALA BORA NA UTAWALA WA SHERIA NA KATIBA KUNA WATU WALIPASWA KUWAJIBIKA AKIWEMO DAKTARI WA RAIS
2. KATIBA INAELEKEZA KWAMBA IKIWA RAIS NI MGONJWA BASI LIUNDWE JOPO LA MADAKTARI BINGWA WA KUISHUGHULIKIA AFYA YA RAIS KIKATIBA. NA HILO JOPO LIJULIKANE WAZI KIKATIBA. HILO HALIKUFANYIKA. KWA KOSA HILI KATIKA NCHI INAYOFUATA UTAWALA BORA NA UTAWALA WA SHERIA NA KATIBA KUNA WATU WALIPASWA KUWAJIBIKA AKIWEMO DAKTARI WA RAIS
3. KWA MUJIBU WA KATIBA, WAZIRI MKUU NA BARAZA LAKE WANAKOMA KUWA KWENYE NAFASI ZAO PALE ALIYEWATEUA ANAPOKUWA HAYUPO OFISINI KWA NAMNA YEYOTE ILE IKIWEMO KUJIUZULU, KUFARIKI AU KUONDOLEWA MADARAKANI. HILO HALIJAFANYIKA NA WANAENDELEA NA NYADHIFA ZAO KANA KWAMBA KIAPO KINADHITHIWA.

NCHI YETU TUNA KAZI YA KUFANYA KUWAFANYA VIONGOZI WETU WAFUATE KATIBA.
 
Bila shaka na msaliti mzee wa MIGA Tundu Lisu atakuwa kwenye baraza jipya la mawaziri.
 
Bila shaka na Tundu Lisu atakuwa kwenye baraza jipya la mawaziri.
Tena akithubutu kufaya hivyo atakuwa amejiwekea mazingira mazuri ya kupita mwaka 2025 maana upinzani utapungua, Tazama Zanzibar hivi sasa kuna mshikamano sana hata kabla Maalim Seif hajafariki yoteilitokana na kuundwa kwa serikali ya mseto!
 
Mimi siyo mwanasheria lakini nafahamu huwezi kuwa na baraza la mawaziri bila Rais.

Saa na dakika aliyofariki Rais Magufuli na Baraza la mawaziri lilivunjika muda ule ule.

Huwezi kusema huyu mtu kafa lakini mkono wake utaendelea kuishi!
Hivi unajua kipindi Hayati yupo ata mapumzikoni Makamo wa Rais ambaye kwasasa ni Rais alikuwa anaendesha Baraza la Mawaziri?
 
Mimi siyo mwanasheria lakini nafahamu huwezi kuwa na baraza la mawaziri bila Rais.

Saa na dakika aliyofariki Rais Magufuli na Baraza la mawaziri lilivunjika muda ule ule.

Huwezi kusema huyu mtu kafa lakini mkono wake utaendelea kuishi!
Kwa tafsiri yako, ni kuwa Rais akifa basi hata jaji mkuu anapoteza haki yake pia, kwa vile huyo pia huchaguliwa na rais.

Halafu pia inaonekana huelewi kuwa Baraza la Mawaziri lina uwezo wa kumwondoa rais madarakani.
 
Kwa tafsiri yako, ni kuwa Rais akifa basi hata jaji mkuu anapoteza haki yake pia, kwa vile huyo pia huchaguliwa na rais.

Halafu pia inaonekana huelewi kuwa Baraza la Mawaziri lina uwezo wa kumwondoa rais madarakani.
Tatizo lako huelewi maana ya Rais.

Baraza la mawaziri ni sehemu ya Rais!
 
Tatizo lako huelewi maana ya Rais.

Baraza la mawaziri ni sehemu ya Rais!
Kwa tafsiri yako hiyo, iwapo baraza la mawaziri ni sehemu ya Rais basi kifungu hiki cha katiba hakina maana yoyote. Je utakuwa unatetea katiba gani wewe? U sehemu ta TLS?

 
Kama wote tunakubaliana kuwa hii ni Selikari ya awamu ya sita basi ni wazi hata baraza la mawaziri linatakiwa kuundwa upya kwa maana la awamu ya tano limevunjika punde baada ya kuapishwa kwa Rais mpya.
 
Kama wote tunakubaliana kuwa hii ni Selikari ya awamu ya sita basi ni wazi hata baraza la mawaziri linatakiwa kuundwa upya kwa maana la awamu ya tano limevunjika punde baada ya kuapishwa kwa Rais mpya.
Wananchi tulipiga kura kuchagua serikali ya awamu ya 5

Sasa ni lini tena wananchi walipiga kura kuchagua serikali ya awamu ya 6?

Hi nchi ina viraza wengi sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…