TLS waungane na Mbowe kuitafakarisha Serikali; nchi bado ina watu wazalendo. Hongera Sungusia

TLS waungane na Mbowe kuitafakarisha Serikali; nchi bado ina watu wazalendo. Hongera Sungusia

Tafuta pesa acheni uhasidi kama wanawake mmejaza chuki kwakuwa tu kuna watu wana maono tofauti na nyinyi wewe toa maoni yako sio kuingia page za watu kutoa picha zao unabaki unaumiza nafsi yako wivu wa nini? shida gani mtu kuwa na rai tofauti wewe unajuwa PSA ya LNG huko Lindi? nchi hii ina watu roho chafu sana bahati nzuri wamejaa huku mitandaoni tu watu safi wako nje wanatafuta pesa tu.
HUjielewi
 
Serikali isipoteze muda wake kuendelea kutengeneza watu au makundi ya watu waje kuutetea ule mkataba wa hovyo unaoutweza utu wa mtanganyika ndani ya ardhi yake.

Huu ni wakati wa serikali kuja na majibu sahihi ya maswali yanayoulizwa juu ya ule mkataba, utakuwa wa muda gani? Tanganyika itafaidika vipi? na mengine.

Kinyume na hapo, serikali itaonekana wazi haipo kulinda mipaka ya nchi yetu, kulinda maslahi ya mtanganyika ndani ya mipaka yake, serikali ya aina hii itadhihirisha inafanya mambo kwa manufaa ya mwarabu, hii itakuwa sawa na serikali ya mkoloni ndani ya Tanganyika.
IBARA 4(2) Kwamba serikali inapopata mwekezaji mwingine maeneo mengine ya bandari inatakiwa iende Dubai kuiomba DPW ili iridhie! Huku kujidhalilisha kwa nchi huruma, ardhi yake iende Dubai kuiomba ridhaa? Lahaullah!
 
Aliposema Mbowe ilionekana upinzani; aliposema Kitima ikaonekana Udini; akasema Warioba ikaonekana uzee unasumbua; akisimama Dr. Slaa akaambiwa alihongwa; Tundu Lisu hakujibiwa kabisa kama ilivyo kwa Lipumba na wazalendo wengine.

Sasa imekuja taasisi ambayo inaundwa na watu wa vyama vyote; dini zote, pande zote za Muungano na rangi tofauti. Taasisi hii inaitwa TLS ( ikumbukwe wapo wazanzibari ambao ni wanachama ndo maana nasema pande zote za Muungano). Taasisi hii ambayo baadhi ya Mawaziri, Wabunge, viongozi waandamizi serikali ni wanachama imesema kwamba MKATABA WA BANDARI UNA DOSARI KUBWA SANA.

Kutokana na uchambuzi wa taasisi hii ambayo asilimia kubwa ya wanasheria hata wa CCM niwanachama inamaanisha kwamba wanasheria wote wa TLS kwa kauli moja wanasema mkataba mbovu. Yawezekana hata AG naye ameunganishwa kwenye hili tamko la kitaaluma kama naye ni mwanachama.

Swali, tunatokaje hapa? Ni kwa namna gani wanasheria watusaidia kusema tena kwamba mkataba hauna matobo? Kwamba leo kwa umoja wao wametamka mbele ya Dunia kwa lugha ya Kiingereza kwamba mkataba una shida....wanachama wanaopingana na hii kauli ya TLS chini ya Sungusia ni wapi? Tuache uchawa na tusiwachanganye wananchi; ni mwanasheria gani anasema mkataba ni mzuri?

Ningependa sana pasiwepo na ukimya; wasiokubaliana na msimamo wa TLS watoke adharani waseme tuwasikie. Wakikaa kimya means wanajua ukweli na ukweli ndio huu wa chama chao.
Waende Mahakamani
 
Back
Top Bottom