TMA: Mikoa 15 kukumbwa na Mvua kubwa zinazoweza kusababisha Mafuriko

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imetoa tahadhari ya uwapo wa mvua kubwa inayotarajiwa kunyesha katika mikoa 15 inayoweza kuleta athari ya mafuriko.

Mikoa iliyotajwa ni Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Tabora, Kigoma, Katavi, Dodoma, Singida, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa na Kusini mwa Mkoa wa Morogoro.

Taarifa iliyotolewa na TMA, ilisema mvua hiyo inaweza kuleta kiwango cha wastani cha athari ikiwamo mafuriko, baadhi ya maeneo kuzungukwa na maji na kuharibu shughuli za kiuchumi.

Aidha, taarifa ilisema mvua ilitarajiwa kunyesha kwa siku tatu kuanzia jana hadi kesho katika mikoa hiyo na kuwambukusha wananchi kuchukua tahadhari na kujiandaa kwa kununua mahitaji ya muhimu na kuweka ndani.

Julai 29, mwaka huu, TMA ilitangaza ujio wa El-Nino katika kipindi cha msimu wa vuli iliyotatarajiwa kunyesha kuanza Oktoba hadi Desemba, mwaka huu na kutoa angalizo kuwa, inaweza kusababisha athari katika maeneo mbalimbali.
 
Kwetu Nyanda za Juu Kusini hakuna Mafuriko hatuishi bondeni Wala Nyanda za tambarare,TMA waache porojo.
 
Halafu utaambiwa hizo mvua hazijaenda kwenye mabwawa ya umeme
 
Kwa kweli TMA saiv taarifa zao zina ukweli fulani tuchukue tahadhari kabisa.
Kwani ni wao basi, Marekani hiyo ndio source ya weather forecast, Angalia hata kwenye simu yako itakuonesha weather forecast ya Kesho hapo ulipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…