TMDA yatoa tahadhari kuhusu taarifa ya Dawa za ARV'S kutumika kunenepesha mifugo

TMDA yatoa tahadhari kuhusu taarifa ya Dawa za ARV'S kutumika kunenepesha mifugo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Snapinsta.app_461068955_18298345987203109_2200242362823949634_n_1080.jpg


TAHADHARI YA MATUMIZI HATARI YA DAWA ZA KUFUBAZA MAKALI YA VIRUSI VYA UKIMWI (ARV'S) KUNENEPESHA MIFUGO

1. Mamlaka imepata taarifa juu ya uwepo wa baadhi ya wafugaji wanaotumia vibaya dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI (ARV's) ili kunenepesha mifugo yao.

2. TMDA inapenda kukemea matumizi hayo kwani yana madhara makubwa kwa afya ya jamii.

3. Dawa hizo zinatakiwa zitumike kwa ajili ya kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI kwa binadamu baada ya mgonjwa kushauriwa na daktari, na hivyo matumizi yake katika kulisha mifugo kuna hatarisha afya ya jamii

4. TMDA inaelekeza wafugaji wote wanaofanya hivyo kuacha mara moja. Aidha, Kuanzia sasa TMDA imeanza uchunguzi wa kina katika mashamba mbalimbali ya mifugo ili kubaini wanaojihusisha na matumizi holela ya dawa na atakayebainika kufanya hivyo, atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kuharibiwa kwa mifugo yake kwani itakuwa mazao ya mifugo husika haifai tena kwa matumizi ya binadamu.

5. Vilevile, TMDA inatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa ofisi za TMDA Makao Makuu na ofisi za Kanda zilizopo Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma, Songea, Tabora na Geita au kupitia barua pepe ya info@tmda.go.tz, ofisi za afya za Halmashauri au kupiga simu bila malipo kupitia Na.0800110084 endapo wataona dalili zozote za matumizi hayo hatari.
 
Njia nzuri ya kupunguza/kutatua hili tatizo ni kuongeza security layer kwa wahadumu wa afya (Mfumo KAZI).

pia, kungekua na update za vigezo sahihi vya utolewaji wa hizo dawa .

Muhimu zaidi Viongozi Mjitathmini !!
 
Wamechelewa Sana mbona ,huku vijijini Kuna manguruwe yanatembea tembea tu njian ni makubwa Kama wadada mabonge ukikutana nalo usiku unaweza kukimbia japo Siri ni hizo njugu
 
Ni baada ya Wana mgambo wa HIZBOLLAH kurusha rocket zaidi ya 100 ndani ya Israel na kujeruhi watu watatu.....
 
Yani awa wafugaji awataki kupata asara angalieni na kuku basi manaake nyama siku izi zime kuwa laini sana
 
Back
Top Bottom