Habari,
Wengi wenu wiki zilizopita mlipokea message kutoka tigo kwamba mmechaguliwa kuingia kwenye kundi muhimu la wateja wa malipo ya baada. Na kwamba mtembelee maduka ya tigo muunganishwe au mpige namba zilizoandikwa kwenye hizo message. Si ndiyo?
Lengo kuu la hii post ni kuwaelezea maana ya hiyo message na kwamba, hakuna kitu cha bure ,kama wengi wa mliopiga simu mnavyofikiria.Ukiwa unataka kununua vocha ili upate huduma lazima utoe pesa yako mfukoni ili uweze kufanya mawasiliano. Hiyo ni inaitwa malipo kabla.
Malipo kabla ni huduma zote kama mini kabang,kabang,bundle za siku,wiki,na mwezi.Ni kwa watu ambao hawaoni shida kununua vocha Mara kwa Mara,watu ambao hawapigi simu nyingi kila siku. Kwa ufupi, mtu ambaye hana matumizi makubwa ya simu.
Lakini kuna jamii nyingine ya watu, mfano kampuni zinazotoa huduma za kukusanya madeni(wanasheria Mara nyingi wanatoa hizi huduma).Simu zao muda mwingi huwa ziko busy kuwapigia simu wateja kuwakumbusha kulipa madeni wanayodaiwa. Hawa watu simu zao lazima muda wote ziwe na vocha.
Wengi wao huwa wanaamua kujiunga na huduma ya malipo ya baada-kwamba unapewa bundle(kifurushi cha mawasiliano) chenye muda wa maongezi, meseji, na GB. Ambacho wewe unakilipia baada ya muda wa siku 30. Ni sawa na vifurushi vya kawaida sema unalipa baada ya mwezi au siku 30(inategemea na mwezi).
Lakini wakati unajiunga kwenye hii huduma(malipo baada) lazima uweke kianzio. Amana. Security deposit. Ni kama bondi hivi. Ni sawa na unapotaka kuchukua mkopo Benki. Lazima uweke bondi, ili utakaposhindwa kulipia madeni yako,ile bondi itatumika kama fidia. Sio bure.
Wewe kama sio mtumiaji mkubwa wa simu nikimaanisha kwamba, muda mwingi hulazimiki kwenda kupiga simu ili ufanye biashara, au labda wewe sio mtu unayesafiri mara nyingi kwenda mikoani kwenye sehemu ambazo hakuna maduka ya vocha,usipoteze muda wako kujiunga. Hii huduma ni kwa watu wenye matumizi MAKUBWA ya simu na wale ambao hawapendi KERO za kuishiwa na vocha Mara kwa Mara.
Lakini kama matumizi yako(ununuaji wako wa vocha) ni wa kawaida(tshs 1000-2000 kwa siku),usipoteze muda wako kujiunga. Tigopesa yako itakidhi mahitaji yako yote.
Naitwa Ian niko tigo. Kama una maswali yeyote kuhusiana na hii hizi huduma mbili. Usisite kuuliza.
Wengi wenu wiki zilizopita mlipokea message kutoka tigo kwamba mmechaguliwa kuingia kwenye kundi muhimu la wateja wa malipo ya baada. Na kwamba mtembelee maduka ya tigo muunganishwe au mpige namba zilizoandikwa kwenye hizo message. Si ndiyo?
Lengo kuu la hii post ni kuwaelezea maana ya hiyo message na kwamba, hakuna kitu cha bure ,kama wengi wa mliopiga simu mnavyofikiria.Ukiwa unataka kununua vocha ili upate huduma lazima utoe pesa yako mfukoni ili uweze kufanya mawasiliano. Hiyo ni inaitwa malipo kabla.
Malipo kabla ni huduma zote kama mini kabang,kabang,bundle za siku,wiki,na mwezi.Ni kwa watu ambao hawaoni shida kununua vocha Mara kwa Mara,watu ambao hawapigi simu nyingi kila siku. Kwa ufupi, mtu ambaye hana matumizi makubwa ya simu.
Lakini kuna jamii nyingine ya watu, mfano kampuni zinazotoa huduma za kukusanya madeni(wanasheria Mara nyingi wanatoa hizi huduma).Simu zao muda mwingi huwa ziko busy kuwapigia simu wateja kuwakumbusha kulipa madeni wanayodaiwa. Hawa watu simu zao lazima muda wote ziwe na vocha.
Wengi wao huwa wanaamua kujiunga na huduma ya malipo ya baada-kwamba unapewa bundle(kifurushi cha mawasiliano) chenye muda wa maongezi, meseji, na GB. Ambacho wewe unakilipia baada ya muda wa siku 30. Ni sawa na vifurushi vya kawaida sema unalipa baada ya mwezi au siku 30(inategemea na mwezi).
Lakini wakati unajiunga kwenye hii huduma(malipo baada) lazima uweke kianzio. Amana. Security deposit. Ni kama bondi hivi. Ni sawa na unapotaka kuchukua mkopo Benki. Lazima uweke bondi, ili utakaposhindwa kulipia madeni yako,ile bondi itatumika kama fidia. Sio bure.
Wewe kama sio mtumiaji mkubwa wa simu nikimaanisha kwamba, muda mwingi hulazimiki kwenda kupiga simu ili ufanye biashara, au labda wewe sio mtu unayesafiri mara nyingi kwenda mikoani kwenye sehemu ambazo hakuna maduka ya vocha,usipoteze muda wako kujiunga. Hii huduma ni kwa watu wenye matumizi MAKUBWA ya simu na wale ambao hawapendi KERO za kuishiwa na vocha Mara kwa Mara.
Lakini kama matumizi yako(ununuaji wako wa vocha) ni wa kawaida(tshs 1000-2000 kwa siku),usipoteze muda wako kujiunga. Tigopesa yako itakidhi mahitaji yako yote.
Naitwa Ian niko tigo. Kama una maswali yeyote kuhusiana na hii hizi huduma mbili. Usisite kuuliza.