Tofauti kati ya Tozo na Kodi ni nini?

Tofauti kati ya Tozo na Kodi ni nini?

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Ninaelewa kuwa Kodi ni malipo yasiyo ya hiari ambayo raia analipa serikalini kutokana ama na mapato au kutokana na mali anayomiliki. Kuna Kodi ya Ardhi, Kodi ya Mapato, Kodi ya Gari na kadhali.

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuja neno jipya linalotwa Tozo, ambayo nayo ni malipo yasiyo ya hiarai ambayo raia analipa serikalini kwa kutumia huduma fulani na ambayo ni juu ya zile gharama ambazo anatakiwa alipe ili kupata huduma hiyo kwa mfano huduma za kibenki au huduma za miamala ya simu.

Je, kuna haja gani ya kutumia neno jipya la Tozo ilihali ni malipo ya lazima yanayofanywa na raia serikalini kama KodiI? Kuna faida gani ya kutofautisha Kodi na Tozo?
 
Wanajua fika Kodi haitakiwi kutozwa mara mbili, ndio maana wanajificha kwenye neno tozo. Kila Mara wanataka kutoa ufafanuzi wa tozo na hakuna mtu atawaelewa.
 
Ninaelewa kuwa KODI ni malipo yasiyo ya hiari ambayo raia analipa serikalini kutokana ama na mapato au kutokana na mali anayomilik...
Kodi ni ya Mwenyezi Mungu wa Mbinguni na Tozo ni ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania.
 
Tofauti ya tozo na kodi ni kama tofauti ya chakula na msosi, vikiwa kwenye sahani.
 
Wanajua fika Kodi haitakiwi kutozwa mara mbili, ndio maana wanajificha kwenye neno tozo. Kila Mara wanataka kutoa ufafanuzi wa tozo na hakuna mtu atawaelewa.
Tozo ni kwaajili ya maendeleo ya Tanzania yetu na kodi pia ni kwaajili yamaendeleo hakuna nchi isiyokua na kodi,
Tozo imekuja ili nchi yetu ijitegemee tupunguze mikopo
 
Labda Kodi haitozwi inakatwa !!!!

In Short ni Usanii mwanzo mwisho..., Hawa Jamaa wamejisahau sana dawa ni kuwapiga Chini tu..., Popote wakipita ni kuonyesha kutokuridhika...

Naona sasa wameanza na vitisho kwa kuwafunga baadhi wasiokubaliana na huu uharamia...
 
Tozo ni kwaajili ya maendeleo ya Tanzania yetu na kodi pia ni kwaajili yamaendeleo hakuna nchi isiyokua na kodi,
Tozo imekuja ili nchi yetu ijitegemee tupunguze mikopo

Kama ni kitu kimoja au ni kitu hichohichobkwanini kipewe majina tofauti?

Hakuna mahali nimesema nnapinga kuchangia maendeleo ya nchi, kimsingi ni wajibu wangu kama mwananchi. Shida ni pale utaratibu unapokua haueleweki, pia matumizi mabaya au ufujaji wa hayo mapato.
 
Labda Kodi haitozwi inakatwa !!!!

In Short ni Usanii mwanzo mwisho..., Hawa Jamaa wamejisahau sana dawa ni kuwapiga Chini tu..., Popote wakipita ni kuonyesha kutokuridhika...

Naona sasa wameanza na vitisho kwa kuwafunga baadhi wasiokubaliana na huu uharamia...
 
TOZO, limetokana na neno TOZA. Toza maana yake lipisha/lipishwa.

Ukiliangalia haraka haraka ni kama adhabu ya malipo kwa muda fulani hivi. Sasa tumekosea wapi hadi tulipishwe?

Kodi ni kulipa kulingana na ulichokipata na ipo kisheria inatambulika kuliko tozo ambayo inaweza kuwepo kwa muda fulani na ikaondoka kwa muda huo huo pasipo kuathiri chochote.

Ni kwa mtazamo wangu.
 
Ninaelewa kuwa Kodi ni malipo yasiyo ya hiari ambayo raia analipa serikalini kutokana ama na mapato au kutokana na mali anayomiliki. Kuna Kodi ya Ardhi, Kodi ya Mapato, Kodi ya Gari na kadhali.

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuja neno jipya linalotwa Tozo, ambayo nayo ni malipo yasiyo ya hiarai ambayo raia analipa serikalini kwa kutumia huduma fulani na ambayo ni juu ya zile gharama ambazo anatakiwa alipe ili kupata huduma hiyo kwa mfano huduma za kibenki au huduma za miamala ya simu.

Je, kuna haja gani ya kutumia neno jipya la Tozo ilihali ni malipo ya lazima yanayofanywa na raia serikalini kama KodiI? Kuna faida gani ya kutofautisha Kodi na Tozo?
Kama ulivyoainisha, kodi (tax) huchukuliwa kutokana na kipato, yaani, mshahara, mauzo, ongezeko la thamani n.k.
Tozo (levy), hutozwa kwenye huduma, mfano tunaoona Tz ni huduma za kununua umeme, pesa hasa za mtandaoni n.k

Katika haya, sijaona mantiki ya kuweka tozo katika benki, kama ni mshahara, malipo ya uzeeni, akiba za watu, unaweka tozo ya nini kama sio kuwafuja na kuwahujumu wananchi kwa kidogo chao unachowapunja tayari! Malipo ya uzeeni, wengine Kwa miezi 3 wanalipwa laki moja, mshahara haiongezwi mwaka wa 7 huu bado na tozo juu?

Kama mchangiaji mmoja hapo alichosema, kuwa tunaadhibiwa, kwa kosa gani?
 
Kama ulivyoainisha, kodi (tax) huchukuliwa kutokana na kipato, yaani, mshahara, mauzo, ongezeko la thamani n.k.
Tozo (levy), hutozwa kwenye huduma, mfano tunaoona Tz ni huduma za kununua umeme, pesa hasa za mtandaoni n.k

Katika haya, sijaona mantiki ya kuweka tozo katika benki, kama ni mshahara, malipo ya uzeeni, akiba za watu, unaweka tozo ya nini kama sio kuwafuja na kuwahujumu wananchi kwa kidogo chao unachowapunja tayari! Malipo ya uzeeni, wengine Kwa miezi 3 wanalipwa laki moja, mshahara haiongezwi mwaka wa 7 huu bado na tozo juu?

Kama mchangiaji mmoja hapo alichosema, kuwa tunaadhibiwa, kwa kosa gani?
Maelezo yako siyo sahihi. Tax ni malipo yoyote ya kimabavu ambayo raia anatakiwa kuilipa serikali bila kuwa na hiari nayo. Kodi ya mapato ni aina moja ya kodi, lakini pia kuna kodi nyingine kama kodi ya kumiliki ardhi, kodi ya kumiliki chombo cha usafiri, kodi ya kununua kitu chochote, kodi ya kupita airport na kodi nyinginezo.

Tozo ni kodi iliyopewa jina jingine tu; bado ni malipo ya kimabavu ambayo raia anatakiwa kuilipa serikali bila kuwa na hiari nayo. Siyo kuwa kwa vile inatozwa kwenye huduma basi inakuwa siyo kodi, ni kodi tu kama ilivyo Airport Tax, Property Tax ambazo ni kodi zinazotokana na kutumia huduma fulani
 
Ninaelewa kuwa Kodi ni malipo yasiyo ya hiari ambayo raia analipa serikalini kutokana ama na mapato au kutokana na mali anayomiliki. Kuna Kodi ya Ardhi, Kodi ya Mapato, Kodi ya Gari na kadhali.

Katika miaka ya hivi karibuni kumekuja neno jipya linalotwa Tozo, ambayo nayo ni malipo yasiyo ya hiarai ambayo raia analipa serikalini kwa kutumia huduma fulani na ambayo ni juu ya zile gharama ambazo anatakiwa alipe ili kupata huduma hiyo kwa mfano huduma za kibenki au huduma za miamala ya simu.

Je, kuna haja gani ya kutumia neno jipya la Tozo ilihali ni malipo ya lazima yanayofanywa na raia serikalini kama KodiI? Kuna faida gani ya kutofautisha Kodi na Tozo?
Hivi nchi yetu kwanini isipunguze kodi ya thamani ya 18% ambayo imekaa muda mrefu
Nafikiri wapunguze hadi 16%, hii itasaidia kuongeza idadi ya walipa kodi kwa 18% kuna watu wanaona ni kubwa sana.
 
Kodi ni kutokana (inatozwa) na kipato au Mali, na tozo ni katika huduma
 
Hivi nchi yetu kwanini isipunguze kodi ya thamani ya 18% ambayo imekaa muda mrefu
Nafikiri wapunguze hadi 16%, hii itasaidia kuongeza idadi ya walipa kodi kwa 18% kuna watu wanaona ni kubwa sana.
Siku Mjadala wa Kodi utapokuwa hot mitandaoni na kwny vijiwe kuliko talaka za kina Haji Manara na Mimba za wabongo movies ndio siku Serikali itaweza ku consider reaction za Raia wakiwaza kupandisha au kuanzisha kodi au tozo mpya

sasa hivi jambo la kikodi linaanzishwa na ikihojiwa a atumwa Steve Nyerere, Mwijaku na Baba levo kutoa ufafanuzi na tunaridhika
 
Tozo ni kwaajili ya maendeleo ya Tanzania yetu na kodi pia ni kwaajili yamaendeleo hakuna nchi isiyokua na kodi,
Tozo imekuja ili nchi yetu ijitegemee tupunguze mikopo
UMECHEKESHA TU, WALA HAKUNA LA MAANA ULILOELEZA..!!
 
Tozo ni kwaajili ya maendeleo ya Tanzania yetu na kodi pia ni kwaajili yamaendeleo hakuna nchi isiyokua na kodi,
Tozo imekuja ili nchi yetu ijitegemee tupunguze mikopo
Jibu swali.
 
Hivi nchi yetu kwanini isipunguze kodi ya thamani ya 18% ambayo imekaa muda mrefu
Nafikiri wapunguze hadi 16%, hii itasaidia kuongeza idadi ya walipa kodi kwa 18% kuna watu wanaona ni kubwa sana.
Sio 16% kwanini isiwe 5% tuone je tutakufa maskini au bidhaa zitashuka Bei hivyo serikali itaingiza sana? Tatizo wanapupa na Mambo matokeo yake yanakua hafifu halafu tunaanza kupigizana kelele Sasa li VAT ya Nini 18 yote?
 
Back
Top Bottom