Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Hilo linasaidia vipi mamilioni ya watu waliopo vijijini Kwa mfano. Na je una uhakika Hilo tu kitakufanya uamini kweli magufuli ni rais wa wanyonge.. Jukumu Hilo umeliona ni gumu Sana na ni muhimu Sana kutekelezwa??? Upo serious
... Let's be honest, yaani wewe unaona ni sawa kuwa na kiongozi ambaye amefanya udanganyifu kuhusu elimu yake? Huyu atakuwaje na moral authority Kukemea wenzake kama alivyosema mukulu??
 
BUNGE LIVE. BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.BUNGE LIVE.
 
... Let's be honest, yaani wewe unaona ni sawa kuwa na kiongozi ambaye amefanya udanganyifu kuhusu elimu yake? Huyu atakuwaje na moral authority Kukemea wenzake kama alivyosema mukulu??
Mkuu IROKOS huyu ndege JOHN nadhani amekaimu nafasi ya Pascal Mayalla kutetea ujinga tu mbele ya watu wanaojitambua, yaani hata mishipa ya aibu hawana hawa watu.
 
Kujiuzulu kwa kushindwa kuongoza nchi.

Taja moja tu moja Kwa moja Bila kuzunguka tuone tatizo liko wapi? Taja moja ambalo Kwa mujibu wa katiba lipo ndani ya uwezo wa rais na halihitaji nguvu nyingi zaidi ya maamuzi tu Bila kujali siasa. Jambo lenyewe liwe linagusa kweli kweli Maslahi ya wanyonge liwe linasaidia mamilioni ya watu na unahisi bado halijafanyika na tatizo liko ndani ya mamlaka hio kuu. Moja tu likifanyika utapata Imani kuwa rais magufuli anamaanisha na labda pengine ni changamoto fulani zinatatiza. Moja tu
 
Hakuna moja, kuna elfu moja na moja.

Magufuli hataki mjadala, ana hulka ya udikteta, anajiona anajua kila kitu, kasema watu watalimia meno. Kasema wasio na nauli watapiga mbizi.

Anafuga mtu aliyeiba mpaka jina na kufoji vyeti, huku akijinadi anapiga vita waliofoji vyeti.

Hana muelekeo wa kisiasa unaoleweka. Leo anaweza kuvunjia nyumba watu mabondeni bila simile (si mtetezi wa wanyonge) kesho akaachia Wamachinga wafanye biashara bila mipango (anatetea wanyonge bila mpango endelevu).

Magufuli haheshimu uhuru wa bunge, kalipangia bunge jinsi ya kutumia fedha za tafrija bila hata makubaliano na Spika.

Magufuli haheshimu uhuru wa bunge. Kaapisha wabunge wa kuteuliwa wawe mawaziri kabla hawajaapishwa kuwa wabunge.

Magufuli haheshimu uhuru wa mahakama. Kahutubia mahakama na kuzielekeza jinsi ya kufanya kazi wakati mahakama ni mhimili unaojitegemea.

Magufuli hathamini utenganifu wa serikali na kanisa. Anahutubia habari za kisiasa makanisani. Hili linaweza kuleta mtafaruku na mpasuko wa nchi kidini. Nyerere alikuwa anasali St. Peters kila siku akiwa Dar. Mwinyi aliswali sana Msikiti wa Tambaza. Mkapa alisali sana kanisa la St. Immaculata. Kikwete naye pia motto wa Bagamoyo msikiti anaujua. lakini wote hawa hawakuwahi kuhutubia siasa kwenye madhabahu ya dini to my knowledge, ukiondoa maneno machache tu ya shukurani labda.

Huyu Magufuli anatoa hotuba ya siasa kabisa, kanisani!

Magufuli hatahamini utawala wa sharia. Kawaambia Polisi wakiona gari la kawaida linaenda kwenye lane ya mwendokasi, walichukue, walipeleke polisi, watoe matairi, mwenyewe akija kuulizia matairi wamwambie lilikuja hivyo hivyo bila matairi.

Magufuli hana heshima hata kwa mawaziri wake. Anawaruka bila hata uchunguzi. Mke wa Waziri wake wa karibu kaonewa/ wamepishana maneno kidogo na trafiki, jibaba kaingilia issue na kuvunja utaratibu wa mtu kupandishwa cheo polisi.

Magufuli hataki hata kusoma hotuba anazoandikiwa, matokeo yake anasema madudu.

Magufuli anapenda maamuzi ya ghafla na jazba ambayo hayajachekechwa vizuri na mara nyingine yana athari kwa taifa.

Magufuli ana kauli za kijinga kama motto anayebalehe, ona alivyomdhalilisha Mama Kikwet, mke wa bosi wake wa zamani, kwa kumwambia maneno yasiyo staha hadharani.

Magufuli hawezi mijadala ya kisiasa. Ndiyo maana kapiga marufuku mikutano ya siasa ya wapinzani kinyume na katiba.

I could go on and on and on. kwa nini unataka niseme moja tu?

Msingi mkubwa ni kwamba Mgufuli hana uwezo wa kuwa rais.

Mtu kama huyu hafai kuwa kiongozi.

Post Yako imenisisimua and it's very true Mkulu yuko hivo....

Nikumbushe kidogo aseee alivyomdhalilisha Mke wa Rais mstaafu maana cjasikia hyo aseee




Lo
 
Taja moja tu moja Kwa moja Bila kuzunguka tuone tatizo liko wapi? Taja moja ambalo Kwa mujibu wa katiba lipo ndani ya uwezo wa rais na halihitaji nguvu nyingi zaidi ya maamuzi tu Bila kujali siasa. Jambo lenyewe liwe linagusa kweli kweli Maslahi ya wanyonge liwe linasaidia mamilioni ya watu na unahisi bado halijafanyika na tatizo liko ndani ya mamlaka hio kuu. Moja tu likifanyika utapata Imani kuwa rais magufuli anamaanisha na labda pengine ni changamoto fulani zinatatiza. Moja tu
Hojaze zikibadilika kutoka watu kuwa issue kama kuendeleza kilimo.....
 
Taja moja tu moja Kwa moja Bila kuzunguka tuone tatizo liko wapi? Taja moja ambalo Kwa mujibu wa katiba lipo ndani ya uwezo wa rais na halihitaji nguvu nyingi zaidi ya maamuzi tu Bila kujali siasa. Jambo lenyewe liwe linagusa kweli kweli Maslahi ya wanyonge liwe linasaidia mamilioni ya watu na unahisi bado halijafanyika na tatizo liko ndani ya mamlaka hio kuu. Moja tu likifanyika utapata Imani kuwa rais magufuli anamaanisha na labda pengine ni changamoto fulani zinatatiza. Moja tu
Kwanza kabisa, aliache jeshi la polisi lifanye kazi yake kwa mujibu wa sheria badala ya kutumika kisiasa. Yaani kulinda chama tawala na kuwanyanyasa upinzani.

Pili, aruhusu mikutano ya siasa kwani ipo kisheria na katiba inaruhusu

Tatu, aliache bunge liwe huru

Nne, aziache mahakama zifanye kazi yake pasipo kufuata maagizo kutoka juu

Tano, awakanye wateule wake waache kutoa matamko yasiyo na tija kwa raia. Mfano ni katazo la bodaboda kutifanya shughuri zake usiku. Badala yake aboreshe ulinzi hasa nyakati za usiku kwa kuhakikisha wazee wa matukio hawafanikiwi kufanya uharifu

Sita, anapoteua viongozi, asiteue kwa mapenzi binafsi. Bali ateue kwa vigezo ili mtu akikosea iwe rahisi kumuwajibisha

Saba, awe na lugha za hekima badala ya kuwa na kauri za command wakati watu wanaumia kweli

Nane, maamuzi yake yawe ya busara ili kila mtu aridhike japo hataweza kuwafurahisha wote kutokana na itikadi za kisiasa

Tisa na mwisho, watanzania tunataka freedom of speech ili akikosea tumwambie hapo sio sawa.

NOTE: mimi ni mtanzania wa kawaida wala sina chama. Nimeandika ninayoyaona hayako sawa kwa upeo wangu
 
"Ukielewa kwa nini baba yako alikuwa harudi na mkate kila siku. ..ujue umekuwa "
 
Amruhusu mzee Mbowe aendelee na biashara yake ya ngada tubwie, tulewe,tusizi sisi tusiomudu bia.
 
Alivunje bunge turudi kwenye uchaguzi mkuu ili turudie kuchagua bila kuangalia mihemko ya pushapu.
 
Watumishi wanamwangalia tu,watakachomfanyia na kumtolea ktk kila sekta hataamini.
 
Hilo linasaidia vipi mamilioni ya watu waliopo vijijini Kwa mfano. Na je una uhakika Hilo tu kitakufanya uamini kweli magufuli ni rais wa wanyonge.. Jukumu Hilo umeliona ni gumu Sana na ni muhimu Sana kutekelezwa??? Upo serious

Kwa ujumla yupo bagalashagala kiasi hafahamiki anasimamia lipi na kwa mtindo upi. Ni mtu aliyeweka itakadi za chama mbele na mihemko mpaka kuona wenye umuhimu nchi hii ni wanaccm. Kwake mtu aliye na mtazamo tofauti hana nafasi naye. Kwa maneno marahisi wanyonge kwake ni wale wanaojijinyekeza, kumuogopa na kujipendekeza. Anachohubiri mdomoni sio anachotekeleza na ni mtu aliyejaa ubinafasi, chuki na visasi. Hivyo anaweza kufanya lolote apendalo kwani ameonyesha kwa kuwa ana madaraka basi anaweza kufanya aonavyo yeye lakini sio kwa ajili ya kutumikia wanyonge kama anavyojinasibu mdomoni.
 
Angechimba canal kuanzia ziwa Tanganyika uunganike na bahari ya Hindi.

Kisha hapo katikati zichimbwe canal nyingine ziungane na hiyo ya mwanzo moja ielekee kuungana na ziwa Victoria na nyingine ziwa nyasa.

Hapo fursa zitakuwa nyingi kwa watanzania. Asante
 
Back
Top Bottom