ROGATH MCHAU
JF-Expert Member
- Jan 17, 2017
- 569
- 1,009
Kama ulishawahi kuforce kuwa mawakala wa chadema walishikiwa bunduki kusaini fomu kwa nini nisicheke.
Mkuu Chagu Wa Malunde, kama nakuona vile, si ajabu ushindi wa mwaka huu ukabeba nguo begani na ukatembea barabarani kwa ushabiki. Naamini uchaguzi 2015 kama ni mpira ulilala na viatu.Islamic brotherhood of Tanzania or Act wazalendo. Nao wanataka nchi?
Mpaka sasa sina mbavu tindo yaani watu wanashikiwa bastola kusaini fomu? Duh hii kali ya mwaka.Sio unacheka, hapo unajichekelesha. Unadhani nilikuambia ili ukubali, nilikuambia ukweli, ukubali ukatae lakini hilo ni juu yako, lakini habari ndio hiyo. Hii kuona watu wengi kutokujitokeza kupiga kura ni sababu ya huo ushenzi. Hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kujitokeza kushiriki uhayawani.
Mpaka sasa sina mbavu tindo yaani watu wanashikiwa bastola kusaini fomu? Duh hii kali ya mwaka.
Hapo sasa unazidi kuforce,mambo ambayo nafikiri yanahitaji mahakama ndio ithibitishe. Tundu Lissu alipigwa risasi eneo la Bunge? Nani alimpiga Akwilina risasi? Mh... Nafikiri ungejikita kwenye hoja upinzani umekosa hoja ya kupambana na JPM na CCM na atashinda 100% basi.Hivi unajifanya unashangaa au huamini nini? Akwilina aliuwawa na hao hao unaojifanya unashangaa kuwa hawawezi. Lisu alipigwa risasi kwenye eneo la bunge katika mazingira hayo hayo unayojifanya unakataa hapa. Acha kufumbia macho uovu dogo kisa ni mahaba niue.
Hapo sasa unazidi kuforce,mambo ambayo nafikiri yanahitaji mahakama ndio ithibitishe. Tundu Lissu alipigwa risasi eneo la Bunge? Nani alimpiga Akwilina risasi? Mh... Nafikiri ungejikita kwenye hoja upinzani umekosa hoja ya kupambana na JPM na CCM na atashinda 100% basi.
Ukilinganisha na uchaguzi wa kwanza nchi yetu ikiwa inafuata mfumo wa vyama vingi mwaka 1995 chama cha upinzani kikubwa wakati huo kilileta upinzani na hata CCM iliogopa maana Nccr mageuzi ilikuwa almanusra wachukue nchi.
Ukaja uchaguzi wa mwaka 2002 CCM walijipanga kivingine hivyo walishinda bila kuwa na misukosuko kama ya mwaka 1995. Maana hata Nccr Mageuzi ilikuwa imeshatetereka.
Na hii ni baada ya CCM kujaribu kurekebisha makosa yake na kutekeleza ilani yake vizuri. Maana hiki ndicho kipindi hata miundo mbinu mingi ilianza kujengwa, mfano barabara ya kuelekea kusini na daraja la mkapa ambalo lilikuwa kwa wananchi kabla ya kujengwa kero.
Na hiki ndio kipindi aliyekuwa waziri wa Ujenzi wakati huo maarufu kama askari wa mwamvuli alidiriki kusema, watu watapanda taxii toka mtwara mpaka Bukoba mkoani kagera.Kwa hiyo CCM ilijrekebisha hadi baadhi ya nchi wahisani walidiriki kufuta madeni ya nchi yetu maana hata uwazi na ukweli katika matumizi ya pesa ya umma ulibadilika tofauti na awamu iliyopita.
Uchaguzi wa 2005 CCM iligawanyika tena sana. Na wajanja wachache wakatengeneza mtandao na mgombea wao akachukua nchi.Na hawakupata upinzani mkali sana.
Uchaguzi wa wa 2010 ulikuwa mgumu kiasi kwa CCM maana sio siri watu walifanya ufisadi mbaya sana. Nchi ilikuwa kama ya kundi fulani ambao wao ni kujichotea pesa tu. Maana stori zilikuwa ni Epa,Escrow n.k
Uchaguzi wa 2015 ulikuwa na ugumu kiduchu kwa CCM maana ilikuwa imechafuliwa na watu wabaya. Na hapo ndipo busara ikatumika ili kumuweka mgombea ambae ni msafi, hata fomu alichukua kimya kimya na hata kuzunguka kwenda kutafuta wadhamini mikoani alienda kimya kimya.
Kwa uzalendo wake alionao alipochaguliwa tu akaanza kudhibiti ubadhirifu na ufisadi,akaanza kujenga Zahanati,vituo vya afya,madaraja na miradi kama Sgr na JNHHP. Na kwa mantiki hiyo akawa ameua kabisa nguvu za upinzani.
Maana wao ili wapate umaarufu ni kuibua ufisadi tu,sasa hizo habari hazipo.
Uchaguzi wa mwaka huu 2020 kwa ngazi ya urais JPM anakwenda kushinda kwa 100%/ ni kama tembo anakanyaga sisimizi.
Sorry mkuu mwaka 2000,ila ujumbe umeupata.Uchaguzi wa 2002 ndio upi huo?
Mlichaguana wewe na nani?
Hukumuelewa vizuri Dk Bashiru fuatilia vizuri alichokuwa anamaanisha.tindo
Umeongea ukweli mtupu......
Huyu jamaa tegemeo lake kubwa lipo kwenye vyombo vya dola, hususani Jeshi la Polisi na TISS
Siku hivyo vyombo vitakapofanya kazi kwa weledi, kama vinavyotakiwa kufanya ndani ya Katiba ya nchi, siku hiyo hiyo CCM ijiandae kukabidhi madaraka........
Hata Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally, alilikiri hilo hadharani!
Sio kujifurahisha ni ukweli wenyewe. Yale mafuriko ya wahuni ambao hawapigi kura sio kipimo cha kusema kulikuwa na upinzani.NILIVYOONA TU UMEANDIKA UCHAGUZI WA 2015 ULIKUA MGUMU KIDUCHU KWA CCM HAPO HAPO NILIACHA KUSOMA SABABU NILIJUA TU UNA NIA YA KUJIFURAHISHA NA CCM YAKO
Sent using Jamii Forums mobile app