Top Ten makabila yenye wazungumzaji wengi Tanzania

Top Ten makabila yenye wazungumzaji wengi Tanzania

masare

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2010
Posts
1,791
Reaction score
1,830
Huu ni utafiti(usiokua rasmi) juu ya uwingi wa wazungumzaji wa makabila yaani wale ambao kiasili ni wenyeji wa kabila husika pamoja na wale ambao wamejifunza makabila husika kutokana na mwingiliano wa shughuli mbalimbali za kimaisha.

1. WASUKUMA
-Idadi yao inakadiriwa kuwa zaidi ya milioni 10. Ni kabila pekee linalopatikana zaidi ya mikoa 6. Wasukuma (ukijumlisha na matawi yake kama Wanyamwezi, Waikizu n.k) wanapatikana mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Simiyu, Tabora na Kigoma pia.

2. WAGOGO
-Wanapatikana kwa wingi mkoani Dodoma. Pia wanapatikana Morogoro/Gairo(huitwa pia Wakaguru). Mkoani Singida wanapatikana wilayani Manyoni (huitwa Wagogo wa Manyoni). Mpakani mwa mikoa ya Dodoma na Iringa pia wanapatikana kwa wingi.

3. WANGONI
Ukijumlisha pamoja na Wandendeule na Wamatengo ambao lughazao huendana sana, basi Wangoni wanafanya kuwa kabila la tatu kwa uwingi Tanzania. Wanapatikana Mkoani Ruvuma.

4. WAMASAI
Hawa wanapatikana Mkoani Arusha pamoja na baadhi ya wilaya za mkoa wa Manyara kama Simanjiro na Kiteto.

5. WARANGI
-Ukiwajumlisha pamoja na matawi yake kama Waburunge na Wanguu hawa nao wanapaswa kuingia kwenye top ten.Wanapatikana kwa wingi wilaya ya Kondoa na Chemba. Pia wanapatikana maeneo ya Mpakani mwa mkoa wa Manyara na Dodoma.

List Itaendelea...

NB: NAJUA UTASHANGAA KUTOYAONA MAKABILA YA WANYAKYUSA, WAHAYA NA WACHAGA HAPO JUU, UKWELI NI KUWA KWA KIPIMO CHA UWINGI WANAPWAYA SANA ILA WAMEFANIKIWA KWENYE UMAARUFU NA ELIMU TU.

Karibuni kwa mjadala
 
Sasa kama Rais anahutubia kwa kisukuma
Kwann wana wasijimwae mwae kuongelea makabila
Ni kosa Hilo Tena kubwa kwa nchi ya makabila 120 hata wahadzabe Wana haki kwa vile wako few basi wasisikilizwe.

Ukabila ni mubaya umezifanya Africa zisipige hatua, na mtu anayejisifia ukabila sio matured enough. I honestly sipendi watu wanao praise ukabila, wakujiona Bora loh, wakati dunia ni village nowdays, Chinese wenyewe Ina user wengi wa lugha yet lugha yao sio international language.
 
Enzi za mwalimu ilikuwa nadra kuongelea ukabila nowdays watu wanaongelea ka fashion. Ukabila ni dhambi ya kuogopwa , so wakishakuwa wengi ni wanapewa hela?
Sio vibaya kuongea makabila, sio vibaya hata kidogo. Ni African inheritance hatuwezi kuikataa wala kuikimbia, muafrika anajitanabaisha kwa ethnicity yake, hivyo kusema sisi wapogoro na wale waluguru is not an issue coz hata zamani makabila yalikuwa yana tamaduni za kutaniana.

Inategemea mtu anaongelea makabila/ukabila kwa minajili gani. Hatuwezi kuwa westernised kiasi cha kusahau ya kwetu, na makabila ni sehemu ya SISI.
 
Sio vibaya kuongea makabila, sio vibaya hata kidogo. Ni African inheritance hatuwezi kuikataa wala kuikimbia, muafrika anajitanabaisha kwa ethnicity yake, hivyo kusema sisi wapogoro na wale waluguru is not an issue coz hata zamani makabila yalikuwa yana tamaduni za kutaniana.

Inategemea mtu anaongelea makabila/ukabila kwa minajili gani. Hatuwezi kuwa westernised kiasi cha kusahau ya kwetu, na makabila ni sehemu ya SISI.
Tunajua Africa watu huongelea ukabila in negative wao always plus nepotism namuunga mkono Nyerere wauliza kabila wataka kutambika hata Tanzania sehemu mtu akijua kabila lako anaanza ukabila though kwa unafiki watu watasema it's normal sijui tusiige wazungu and blah blah kumbe kubebana hata kusikostahili.
 
Wasukuma & Waikizu wawe same tribe group? Fake news!
Matawi ya wasukuma ni wanyamwezi, wasumbwa, wazinza/warongo, siyo waikizu. Hapo mtoa post amechemsha. Aidha, wasukuma wanaishia kwa wingi katika mikoa ya mara, katavi na Singida
 
Ni kosa Hilo Tena kubwa kwa nchi ya makabila 120 hata wahadzabe Wana haki kwa vile wako few basi wasisikilizwe. Ukabila ni mubaya umezifanya Africa zisipige hatua, na mtu anayejisifia ukabila sio matured enough. I honestly sipendi watu wanao praise ukabila, wakujiona Bora loh, wakati dunia ni village nowdays, Chinese wenyewe Ina user wengi wa lugha yet lugha yao sio international language.
Kwa hiyo unataka kumpa Magufuli ujumbe gani ?
 
Enzi za mwalimu ilikuwa nadra kuongelea ukabila nowdays watu wanaongelea ka fashion. Ukabila ni dhambi ya kuogopwa, so wakishakuwa wengi ni wanapewa hela?
Unaelewa maana ya Ukabila au umekaririshwa tu.Soma vizuri hayo maelezo kama kuna itikadi yoyote ya kusifia Ukabila.Hizo ni takwimu na mtoa mada hajazungumzia chembe yoyote ya Ukabila bali makabila kwa maana ya African Inheritance.
 
Sio vibaya kuongea makabila, sio vibaya hata kidogo. Ni African inheritance hatuwezi kuikataa wala kuikimbia, muafrika anajitanabaisha kwa ethnicity yake, hivyo kusema sisi wapogoro na wale waluguru is not an issue coz hata zamani makabila yalikuwa yana tamaduni za kutaniana.

Inategemea mtu anaongelea makabila/ukabila kwa minajili gani. Hatuwezi kuwa westernised kiasi cha kusahau ya kwetu, na makabila ni sehemu ya SISI.
Exactly Mkuu
 
Unaelewa maana ya Ukabila au umekaririshwa tu.Soma vizuri hayo maelezo kama kuna itikadi yoyote ya kusifia Ukabila.Hizo ni takwimu na mtoa mada hajazungumzia chembe yoyote ya Ukabila bali makabila kwa maana ya African Inheritance.
Huo ni ukabila perse na hzo takwimu zako zimedhibitishwa na Takwimu na hyo sensa ya makabila na wazungumzaji kwa wingi ilifanyika lini?
 
Tunajua Africa watu huongelea ukabila in negative wao always plus nepotism namuunga mkono Nyerere wauliza kabila wataka kutambika hata Tanzania sehemu mtu akijua kabila lako anaanza ukabila though kwa unafiki watu watasema it's normal sijui tusiige wazungu and blah blah kumbe kubebana hata kusikostahili.
Tofautisha Kabila na Ukabila
Kabila ni identity ya tamaduni,jamii,desturi,lugha ,ngoma n.k
Ukabila maana yake ni ubaguzi wa kikabila,upendeleo wa kazi,chuki na siasa za kabila.
 
Si
Huu ni utafiti(usiokua rasmi) juu ya uwingi wa wazungumzaji wa makabila yaani wale ambao kiasili ni wenyeji wa kabila husika pamoja na wale ambao wamejifunza makabila husika kutokana na mwingiliano wa shughuli mbalimbali za kimaisha.

1. WASUKUMA
-Idadi yao inakadiriwa kuwa zaidi ya milioni 10. Ni kabila pekee linalopatikana zaidi ya mikoa 6. Wasukuma (ukijumlisha na matawi yake kama Wanyamwezi, Waikizu n.k) wanapatikana mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Simiyu, Tabora na Kigoma pia.

2. WAGOGO
-Wanapatikana kwa wingi mkoani Dodoma. Pia wanapatikana Morogoro/Gairo(huitwa pia Wakaguru). Mkoani Singida wanapatikana wilayani Manyoni (huitwa Wagogo wa Manyoni). Mpakani mwa mikoa ya Dodoma na Iringa pia wanapatikana kwa wingi.

3. WANGONI
Ukijumlisha pamoja na Wandendeule na Wamatengo ambao lughazao huendana sana, basi Wangoni wanafanya kuwa kabila la tatu kwa uwingi Tanzania. Wanapatikana Mkoani Ruvuma.

4. WAMASAI
Hawa wanapatikana Mkoani Arusha pamoja na baadhi ya wilaya za mkoa wa Manyara kama Simanjiro na Kiteto.

5. WARANGI
-Ukiwajumlisha pamoja na matawi yake kama Waburunge na Wanguu hawa nao wanapaswa kuingia kwenye top ten.Wanapatikana kwa wingi wilaya ya Kondoa na Chemba. Pia wanapatikana maeneo ya Mpakani mwa mkoa wa Manyara na Dodoma.

List Itaendelea...

NB: NAJUA UTASHANGAA KUTOYAONA MAKABILA YA WANYAKYUSA, WAHAYA NA WACHAGA HAPO JUU, UKWELI NI KUWA KWA KIPIMO CHA UWINGI WANAPWAYA SANA ILA WAMEFANIKIWA KWENYE UMAARUFU NA ELIMU TU.

Karibuni kwa mjadala
Sipendi ukabila na haina maana ila takwimu rasmi zilizokuwepo miaka 10 iliyopita:
1. Sukuma
2. Nyamwezi
3. Chagga
4. Haya
5. Nyakyusa
 
Back
Top Bottom